Nuh suresi çevirisi Svahili

  1. Suresi mp3
  2. Başka bir sure
  3. Svahili
Kuranı Kerim türkçe meali | Kur'an çevirileri | Svahili dili | Nuh Suresi | نوح - Ayet sayısı 28 - Moshaf'taki surenin numarası: 71 - surenin ingilizce anlamı: Noah.

إِنَّا أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ أَنْ أَنذِرْ قَوْمَكَ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ(1)

 Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.

قَالَ يَا قَوْمِ إِنِّي لَكُمْ نَذِيرٌ مُّبِينٌ(2)

 Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,

أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ(3)

 Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.

يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ(4)

 Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!

قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوْتُ قَوْمِي لَيْلًا وَنَهَارًا(5)

 Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,

فَلَمْ يَزِدْهُمْ دُعَائِي إِلَّا فِرَارًا(6)

 Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.

وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوْتُهُمْ لِتَغْفِرَ لَهُمْ جَعَلُوا أَصَابِعَهُمْ فِي آذَانِهِمْ وَاسْتَغْشَوْا ثِيَابَهُمْ وَأَصَرُّوا وَاسْتَكْبَرُوا اسْتِكْبَارًا(7)

 Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!

ثُمَّ إِنِّي دَعَوْتُهُمْ جِهَارًا(8)

 Tena niliwaita kwa uwazi,

ثُمَّ إِنِّي أَعْلَنتُ لَهُمْ وَأَسْرَرْتُ لَهُمْ إِسْرَارًا(9)

 Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.

فَقُلْتُ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا(10)

 Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.

يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا(11)

 Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا(12)

 Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.

مَّا لَكُمْ لَا تَرْجُونَ لِلَّهِ وَقَارًا(13)

 Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?

وَقَدْ خَلَقَكُمْ أَطْوَارًا(14)

 Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?

أَلَمْ تَرَوْا كَيْفَ خَلَقَ اللَّهُ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا(15)

 Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?

وَجَعَلَ الْقَمَرَ فِيهِنَّ نُورًا وَجَعَلَ الشَّمْسَ سِرَاجًا(16)

 Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?

وَاللَّهُ أَنبَتَكُم مِّنَ الْأَرْضِ نَبَاتًا(17)

 Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.

ثُمَّ يُعِيدُكُمْ فِيهَا وَيُخْرِجُكُمْ إِخْرَاجًا(18)

 Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.

وَاللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ بِسَاطًا(19)

 Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.

لِّتَسْلُكُوا مِنْهَا سُبُلًا فِجَاجًا(20)

 Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.

قَالَ نُوحٌ رَّبِّ إِنَّهُمْ عَصَوْنِي وَاتَّبَعُوا مَن لَّمْ يَزِدْهُ مَالُهُ وَوَلَدُهُ إِلَّا خَسَارًا(21)

 Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.

وَمَكَرُوا مَكْرًا كُبَّارًا(22)

 Na wakapanga vitimbi vikubwa.

وَقَالُوا لَا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلَا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلَا سُوَاعًا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا(23)

 Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.

وَقَدْ أَضَلُّوا كَثِيرًا ۖ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا ضَلَالًا(24)

 Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.

مِّمَّا خَطِيئَاتِهِمْ أُغْرِقُوا فَأُدْخِلُوا نَارًا فَلَمْ يَجِدُوا لَهُم مِّن دُونِ اللَّهِ أَنصَارًا(25)

 Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.

وَقَالَ نُوحٌ رَّبِّ لَا تَذَرْ عَلَى الْأَرْضِ مِنَ الْكَافِرِينَ دَيَّارًا(26)

 Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!

إِنَّكَ إِن تَذَرْهُمْ يُضِلُّوا عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوا إِلَّا فَاجِرًا كَفَّارًا(27)

 Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.

رَّبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَلَا تَزِدِ الظَّالِمِينَ إِلَّا تَبَارًا(28)

 Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.


Svahili diğer sureler:

Bakara suresi Âl-i İmrân Nisâ suresi
Mâide suresi Yûsuf suresi İbrâhîm suresi
Hicr suresi Kehf suresi Meryem suresi
Hac suresi Kasas suresi Ankebût suresi
As-Sajdah Yâsîn suresi Duhân suresi
fetih suresi Hucurât suresi Kâf suresi
Necm suresi Rahmân suresi vakıa suresi
Haşr suresi Mülk suresi Hâkka suresi
İnşikâk suresi Alâ suresi Gâşiye suresi

En ünlü okuyucuların sesiyle Nuh Suresi indirin:

Surah Nuh mp3: yüksek kalitede dinlemek ve indirmek için okuyucuyu seçerek
Nuh Suresi Ahmed El Agamy
Ahmed El Agamy
Nuh Suresi Saad Al Ghamdi
Saad Al Ghamdi
Nuh Suresi Saud Al Shuraim
Saud Al Shuraim
Nuh Suresi Abdul Basit Abdul Samad
Abdul Basit
Nuh Suresi Abdullah Basfar
Abdullah Basfar
Nuh Suresi Abdullah Awwad Al Juhani
Abdullah Al Juhani
Nuh Suresi Ali Al Hudhaifi
Ali Al Hudhaifi
Nuh Suresi Fares Abbad
Fares Abbad
Nuh Suresi Maher Al Muaiqly
Maher Al Muaiqly
Nuh Suresi Muhammad Jibril
Muhammad Jibril
Nuh Suresi Muhammad Siddiq Al Minshawi
Al Minshawi
Nuh Suresi Al Hosary
Al Hosary
Nuh Suresi Al-afasi
Mishari Al-afasi
Nuh Suresi Nasser Al Qatami
Nasser Al Qatami
Nuh Suresi Yasser Al Dosari
Yasser Al Dosari


Friday, May 10, 2024

Bizim için dua et, teşekkürler