Surah Assaaffat aya 5 , Swahili translation of the meaning Ayah.

  1. Arabic
  2. tafsir
  3. mp3
  4. English
Quran in Swahili QUR,ANI TUKUFU na tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili - Ali Muhsen Alberwany & English - Sahih International : Surah Assaaffat aya 5 in arabic text(Those Who Set The Ranks).
  
   

﴿رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ﴾
[ الصافات: 5]

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

Surah As-Saaffat in Swahili

Swahili Translation - Al-Barwani

English - Sahih International


Lord of the heavens and the earth and that between them and Lord of the sunrises.


Tafsiri ya maana yake kwenye lugha ya Kiswahili


Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.


Yeye - peke yake - ndiye Muumba mbingu na ardhi na viliomo baina yao, na ndiye Mwenye kupanga mambo, na ndiye Mwenye kutawala mashariki za kila chenye mashariki. Mwenyezi Mungu ndiye Muumba mbingu saba na viliomo baina yao, navyo ni hivyo vyombo vya mbinguni na nyota zake. Naye ndiye Mwenye kusimamisha, Mwenye kulinda vile vile juu ya mwahali zinapo chomozea jua na nyota zote. Na Yeye ndiye anaye vionyesha hivyo kila siku katika pahala huko upeo wa macho, kila siku pahala mbali na vilipo dhihiri siku iliyo tangulia. Na hayo ni kwa mwendo wa mpango wa jua maalumu kwa inavyo zunguka dunia juu ya msumari-kati wake kutoka magharibi kwendea mashariki kila siku na wakati huo huo inavyo lizunguka jua katika njia yake katika falaki. Na jua na nyota huonekana na wakaazi wa ardhi kila siku kama zinachomoza mwahala mbali mbali. Na kila ardhi ikigeuza mahala pake katika safari yake katika mbingu linaonekana jua linachomoza pahala pengine. Ukiliangalia jua kwa utulivu kuanzia mwishoni wa mwezi wa Machi, yaani linapo kuwa jua lipo kati ya mstari wa Ikweta mwanzo wa musimu wa Rabii, yaani Spring, kwa nusu ya kaskazini ya dunia, utaliona linachomoza pahala katika mashariki juu ya upeo wa macho. Kwa mwenye kupeleleza kila siku ikipita ataona kuchomoza kwake kunajongelea kaskazini. Na mwishoni mwa mwezi wa Juni utaona linachomozea mwisho wa kukaribia kaskazini. Kisha baada ya hapo utaliona jua linarejea linafuata kugeuka kule kule mpaka mwisho wa Septemba (wakati wa kuwa sawa wakati wa Khariif yaani Autumn) utaliona jua linachomoza pale pale lilipo chomoza mwanzo wa Machi. Kisha litaendelea kuelekea kusini kuchomoza kwake mpaka mwisho wa Desemba linakuwa linachomoza karibu kabisa na kusini. Baada ya hapo huanza tena kurejea kuelekea kaskazini mpaka limalize safari yake ya kufika kati sawa katika Rabii ya pili. Na safari hii yote inachukua siku 365 na robo siku. Na inaonekana kuwa nyota nazo zinachomoza mwahala mbali mbali katika upeo wa macho inapo kuwa dunia imo katika safari yake ya mbinguni, na khasa nyota za buruji (au vituo) 12 vinavyo pitiwa na jua katika mwendo wake wa mwaka.

English Türkçe Indonesia
Русский Français فارسی
تفسير Bengali Urdu

listen to Verse 5 from Assaaffat


Ayats from Quran in Swahili


    Quran Surah in Swahili :

    Al-Baqarah Al-'Imran An-Nisa'
    Al-Ma'idah Yusuf Ibrahim
    Al-Hijr Al-Kahf Maryam
    Al-Hajj Al-Qasas Al-'Ankabut
    As-Sajdah Ya Sin Ad-Dukhan
    Al-Fath Al-Hujurat Qaf
    An-Najm Ar-Rahman Al-Waqi'ah
    Al-Hashr Al-Mulk Al-Haqqah
    Al-Inshiqaq Al-A'la Al-Ghashiyah

    Download Surah Assaaffat with the voice of the most famous Quran reciters :

    Surah Assaaffat mp3 : choose the reciter to listen and download the chapter Assaaffat Complete with high quality
    Surah Assaaffat Ahmed El Agamy
    Ahmed Al Ajmy
    Surah Assaaffat Bandar Balila
    Bandar Balila
    Surah Assaaffat Khalid Al Jalil
    Khalid Al Jalil
    Surah Assaaffat Saad Al Ghamdi
    Saad Al Ghamdi
    Surah Assaaffat Saud Al Shuraim
    Saud Al Shuraim
    Surah Assaaffat Abdul Basit Abdul Samad
    Abdul Basit
    Surah Assaaffat Ammar Al-Mulla
    Ammar Al-Mulla
    Surah Assaaffat Abdullah Basfar
    Abdullah Basfar
    Surah Assaaffat Abdullah Awwad Al Juhani
    Abdullah Al Juhani
    Surah Assaaffat Fares Abbad
    Fares Abbad
    Surah Assaaffat Maher Al Muaiqly
    Maher Al Muaiqly
    Surah Assaaffat Muhammad Siddiq Al Minshawi
    Al Minshawi
    Surah Assaaffat Al Hosary
    Al Hosary
    Surah Assaaffat Al-afasi
    Mishari Al-afasi
    Surah Assaaffat Yasser Al Dosari
    Yasser Al Dosari


    Tuesday, June 24, 2025

    Please remember us in your sincere prayers