Sura Al-Muzzammil
PDF —
20 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Muzzammil pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Muzzammil pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Muzzammil Tafsiri. Al-Muzzammil (Makka) 20 Aya.



Sura Al-Muzzammil
20 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓ
Ewe uliye jifunika!
ﭔﭕﭖﭗﭘ
Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Nusu yake, au ipunguze kidogo.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
ﮜﮝﮞﮟﮠ
Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema