Sura Ya-Sin
83 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭬﭭ
Ya-Sin (Y. S.).
ﭮﭯﭰ
Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!
ﭱﭲﭳﭴ
Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
ﭵﭶﭷﭸ
Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
ﭹﭺﭻﭼ
Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema