83 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭬﭭ
36:1 Ya-Sin (Y. S.).
ﭮﭯﭰ
36:2 Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!
ﭱﭲﭳﭴ
36:3 Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
ﭵﭶﭷﭸ
36:4 Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
ﭹﭺﭻﭼ
36:5 Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
36:6 Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
36:7 Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
36:8 Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
36:9 Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
36:10 Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
36:11 Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
36:12 Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
36:13 Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
36:14 Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
36:15 Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
36:16 Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
36:17 Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
36:18 Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
36:19 Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
36:20 Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
36:21 Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
36:22 NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
36:23 Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
36:24 Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
36:25 Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
36:26 Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
36:27 Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
36:28 Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
36:29 Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
36:30 Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
36:31 Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
36:32 Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
36:33 Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
36:34 Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
36:35 Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
36:36 Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
36:37 Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
36:38 Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
36:39 Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
36:40 Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
36:41 Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
36:42 Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
36:43 Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
36:44 Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
36:45 Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
36:46 Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
36:47 Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
36:48 Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
36:49 Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
36:50 Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
36:51 Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
36:52 Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
36:53 Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
36:54 Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
36:55 Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
36:56 Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
36:57 Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
36:58 "Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
36:59 Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
36:60 Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
36:61 Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
36:62 Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
36:63 Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
36:64 Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
36:65 Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
36:66 Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
36:67 Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
36:68 Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
36:69 Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
36:70 Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
36:71 Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
36:72 Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
36:73 Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
36:74 Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
36:75 Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
36:76 Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
36:77 Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
36:78 Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
36:79 Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
36:80 Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
36:81 Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
36:82 Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
36:83 Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema