Sura Al-Inshiqaq
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Inshiqaq pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Inshiqaq pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Inshiqaq Tafsiri. Al-Inshiqaq (Makka) 25 Aya.
Related
- Al-Inshiqaq TafsiriKiswahili
- Al-Inshiqaq mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Inshiqaq

ﭣﭤﭥﭦ
Itapo chanika mbingu,
ﭧﭨﭩﭪ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
ﭫﭬﭭﭮ
Na ardhi itakapo tanuliwa,
ﭯﭰﭱﭲﭳ
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
ﭴﭵﭶﭷ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
ﮇﮈﮉﮊﮋ
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
ﮌﮍﮎﮏﮐ
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
ﮘﮙﮚﮛ
Basi huyo ataomba kuteketea.
ﮜﮝﮞ
Na ataingia Motoni.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
ﯔﯕﯖﯗ
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
ﯘﯙﯚﯛ
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
ﯜﯝﯞﯟ
Na kwa mwezi unapo pevuka,
ﯠﯡﯢﯣﯤ
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
ﯥﯦﯧﯨﯩ
Basi wana nini hawaamini?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
ﯲﯳﯴﯵﯶ
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
ﯷﯸﯹﯺﯻ
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
ﯼﯽﯾﯿ
Basi wabashirie adhabu chungu!
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







