Sura Al-Inshiqaq
PDF —
25 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Inshiqaq pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Inshiqaq pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Inshiqaq Tafsiri. Al-Inshiqaq (Makka) 25 Aya.



Sura Al-Inshiqaq
25 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭣﭤﭥﭦ
Itapo chanika mbingu,
ﭧﭨﭩﭪ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
ﭫﭬﭭﭮ
Na ardhi itakapo tanuliwa,
ﭯﭰﭱﭲﭳ
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
ﭴﭵﭶﭷ
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
ﮇﮈﮉﮊﮋ
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
ﮌﮍﮎﮏﮐ
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
ﮘﮙﮚﮛ
Basi huyo ataomba kuteketea.
ﮜﮝﮞ
Na ataingia Motoni.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
ﯔﯕﯖﯗ
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
ﯘﯙﯚﯛ
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
ﯜﯝﯞﯟ
Na kwa mwezi unapo pevuka,
ﯠﯡﯢﯣﯤ
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
ﯥﯦﯧﯨﯩ
Basi wana nini hawaamini?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
ﯲﯳﯴﯵﯶ
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
ﯷﯸﯹﯺﯻ
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
ﯼﯽﯾﯿ
Basi wabashirie adhabu chungu!
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema