Sura Al-Muddaththir
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Muddaththir pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Muddaththir pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Muddaththir Tafsiri. Al-Muddaththir (Makka) 56 Aya.
Related
- Al-Muddaththir TafsiriKiswahili
- Al-Muddaththir mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Muddaththir

ﮪﮫﮬ
Ewe uliye jigubika!
ﮭﮮﮯ
Simama uonye!
ﮰﮱﯓ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
ﯔﯕﯖ
Na nguo zako, zisafishe.
ﯗﯘﯙ
Na yaliyo machafu yahame!
ﯚﯛﯜﯝ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
ﯞﯟﯠ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
ﯡﯢﯣﯤﯥ
Basi litapo pulizwa barugumu,
ﯦﯧﯨﯩﯪ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
ﯫﯬﯭﯮﯯ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
ﯰﯱﯲﯳﯴ
Niache peke yangu na niliye muumba;
ﯵﯶﯷﯸﯹ
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
ﯺﯻﯼ
Na wana wanao onekana,
ﯽﯾﯿﰀ
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
ﰁﰂﰃﰄﰅ
Kisha anatumai nimzidishie!
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
ﰍﰎﰏ
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
ﰐﰑﰒﰓ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
ﭑﭒﭓﭔ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
ﭕﭖﭗﭘﭙ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
ﭚﭛﭜ
Kisha akatazama,
ﭝﭞﭟﭠ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
ﭡﭢﭣﭤ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
ﭲﭳﭴ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
ﭵﭶﭷﭸﭹ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
ﭺﭻﭼﭽﭾ
Haubakishi wala hausazi.
ﭿﮀﮁ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
ﮂﮃﮄﮅ
Juu yake wapo kumi na tisa.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
ﯥﯦﯧ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
ﯨﯩﯪﯫ
Na kwa usiku unapo kucha!
ﯬﯭﯮﯯ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
ﯰﯱﯲﯳ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
ﯴﯵﯶ
Ni onyo kwa binaadamu,
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
ﰅﰆﰇﰈ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
ﰉﰊﰋﰌ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
ﰍﰎﰏ
Khabari za wakosefu:
ﰐﰑﰒﰓﰔ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
ﰕﰖﰗﰘﰙﰚ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
ﰛﰜﰝﰞﰟ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
ﰠﰡﰢﰣﰤ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
ﰥﰦﰧﰨﰩ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
ﰪﰫﰬﰭ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
ﭜﭝﭞﭟ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
ﭠﭡﭢﭣ
Wanao mkimbia simba!
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
ﭵﭶﭷﭸ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
ﭹﭺﭻﭼ
Basi anaye taka atakumbuka.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







