Sura Ar-Rahman pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Ar-Rahman pdf Kiswahili — Pakua Sura Ar-Rahman Tafsiri. Sura Ar-Rahman (Madina) 78 Aya.
Related
- Sura Ar-Rahman TafsiriKiswahili
- Sura Ar-Rahman mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Ar-Rahman

ﭷﭸ
55:1
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
ﭹﭺﭻ
55:2
Amefundisha Qur'ani.
ﭼﭽﭾ
55:3
Amemuumba mwanaadamu,
ﭿﮀﮁ
55:4
Akamfundisha kubaini.
ﮂﮃﮄﮅ
55:5
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
ﮆﮇﮈﮉ
55:6
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
55:7
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
55:8
Ili msidhulumu katika mizani.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
55:9
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
ﮛﮜﮝﮞ
55:10
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
55:11
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
ﮥﮦﮧﮨﮩ
55:12
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
55:13
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
55:14
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
55:15
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
ﯝﯞﯟﯠﯡ
55:16
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
ﯢﯣﯤﯥﯦ
55:17
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
ﯧﯨﯩﯪﯫ
55:18
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭑﭒﭓﭔ
55:19
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
ﭕﭖﭗﭘﭙ
55:20
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
ﭚﭛﭜﭝﭞ
55:21
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭟﭠﭡﭢﭣ
55:22
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
55:23
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
55:24
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
55:25
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭵﭶﭷﭸﭹ
55:26
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
55:27
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
ﮁﮂﮃﮄﮅ
55:28
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
55:29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
ﮒﮓﮔﮕﮖ
55:30
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮗﮘﮙﮚﮛ
55:31
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
ﮜﮝﮞﮟﮠ
55:32
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
55:33
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
ﯔﯕﯖﯗﯘ
55:34
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
55:35
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
ﯢﯣﯤﯥﯦ
55:36
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
55:37
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
ﯮﯯﯰﯱﯲ
55:38
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
55:39
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
ﯼﯽﯾﯿﰀ
55:40
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
55:41
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
55:42
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
55:43
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
55:44
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
ﭣﭤﭥﭦﭧ
55:45
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
55:46
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
55:47
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭳﭴﭵ
55:48
Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
ﭶﭷﭸﭹﭺ
55:49
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭻﭼﭽﭾ
55:50
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
ﭿﮀﮁﮂﮃ
55:51
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
55:52
Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
55:53
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
55:54
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
ﮚﮛﮜﮝﮞ
55:55
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
55:56
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
55:57
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮮﮯﮰﮱ
55:58
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
55:59
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
55:60
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
ﯞﯟﯠﯡﯢ
55:61
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯣﯤﯥﯦ
55:62
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
ﯧﯨﯩﯪﯫ
55:63
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯬﯭ
55:64
Za kijani kibivu.
ﯮﯯﯰﯱﯲ
55:65
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯳﯴﯵﯶ
55:66
Na chemchem mbili zinazo furika.
ﯷﯸﯹﯺﯻ
55:67
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯼﯽﯾﯿﰀ
55:68
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
ﰁﰂﰃﰄﰅ
55:69
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭑﭒﭓﭔ
55:70
Humo wamo wanawake wema wazuri.
ﭕﭖﭗﭘﭙ
55:71
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭚﭛﭜﭝﭞ
55:72
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
55:73
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
55:74
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
ﭫﭬﭭﭮﭯ
55:75
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
55:76
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
ﭷﭸﭹﭺﭻ
55:77
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
55:78
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







