PDF —
78 Aya Madina PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Ar-Rahman pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Ar-Rahman pdf Kiswahili — Pakua Sura Ar-Rahman Tafsiri. Sura Ar-Rahman (Madina) 78 Aya.



78 Aya · Madina · Kiswahili
bismillah
ﭷﭸ
55:1 Arrah'man, Mwingi wa Rehema
ﭹﭺﭻ
55:2 Amefundisha Qur'ani.
ﭼﭽﭾ
55:3 Amemuumba mwanaadamu,
ﭿﮀﮁ
55:4 Akamfundisha kubaini.
ﮂﮃﮄﮅ
55:5 Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
ﮆﮇﮈﮉ
55:6 Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
55:7 Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
55:8 Ili msidhulumu katika mizani.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
55:9 Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
ﮛﮜﮝﮞ
55:10 Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
55:11 Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
ﮥﮦﮧﮨﮩ
55:12 Na nafaka zenye makapi, na rehani.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
55:13 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
55:14 Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
55:15 Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
ﯝﯞﯟﯠﯡ
55:16 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
ﯢﯣﯤﯥﯦ
55:17 Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
ﯧﯨﯩﯪﯫ
55:18 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭑﭒﭓﭔ
55:19 Anaziendesha bahari mbili zikutane;
ﭕﭖﭗﭘﭙ
55:20 Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
ﭚﭛﭜﭝﭞ
55:21 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭟﭠﭡﭢﭣ
55:22 Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
55:23 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
55:24 Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
55:25 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭵﭶﭷﭸﭹ
55:26 Kila kilioko juu yake kitatoweka.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
55:27 Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
ﮁﮂﮃﮄﮅ
55:28 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
55:29 Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
ﮒﮓﮔﮕﮖ
55:30 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮗﮘﮙﮚﮛ
55:31 Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
ﮜﮝﮞﮟﮠ
55:32 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
55:33 Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
ﯔﯕﯖﯗﯘ
55:34 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
55:35 Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
ﯢﯣﯤﯥﯦ
55:36 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
55:37 Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
ﯮﯯﯰﯱﯲ
55:38 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
55:39 Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
ﯼﯽﯾﯿﰀ
55:40 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
55:41 Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
55:42 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
55:43 Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
55:44 Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
ﭣﭤﭥﭦﭧ
55:45 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
55:46 Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
55:47 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭳﭴﭵ
55:48 Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
ﭶﭷﭸﭹﭺ
55:49 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭻﭼﭽﭾ
55:50 Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
ﭿﮀﮁﮂﮃ
55:51 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
55:52 Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
55:53 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
55:54 Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
ﮚﮛﮜﮝﮞ
55:55 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
55:56 Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
55:57 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﮮﮯﮰﮱ
55:58 Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
55:59 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
55:60 Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
ﯞﯟﯠﯡﯢ
55:61 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯣﯤﯥﯦ
55:62 Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
ﯧﯨﯩﯪﯫ
55:63 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯬﯭ
55:64 Za kijani kibivu.
ﯮﯯﯰﯱﯲ
55:65 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯳﯴﯵﯶ
55:66 Na chemchem mbili zinazo furika.
ﯷﯸﯹﯺﯻ
55:67 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﯼﯽﯾﯿﰀ
55:68 Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
ﰁﰂﰃﰄﰅ
55:69 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭑﭒﭓﭔ
55:70 Humo wamo wanawake wema wazuri.
ﭕﭖﭗﭘﭙ
55:71 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭚﭛﭜﭝﭞ
55:72 Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
55:73 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
55:74 Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
ﭫﭬﭭﭮﭯ
55:75 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
55:76 Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
ﭷﭸﭹﭺﭻ
55:77 Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
55:78 Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema