Sura Al-Ghashiya
PDF —
26 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Ghashiya pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Ghashiya pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Ghashiya Tafsiri. Al-Ghashiya (Makka) 26 Aya.



Sura Al-Ghashiya
26 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭽﭾﭿﮀﮁ
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
ﮂﮃﮄﮅ
Siku hiyo nyuso zitainama,
ﮆﮇﮈ
Zikifanya kazi, nazo taabani.
ﮉﮊﮋﮌ
Ziingie katika Moto unao waka -
ﮍﮎﮏﮐﮑ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
ﮠﮡﮢﮣ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
ﮤﮥﮦ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
ﮧﮨﮩﮪ
Katika Bustani ya juu.
ﮫﮬﮭﮮﮯ
Hawatasikia humo upuuzi.
ﮰﮱﯓﯔ
Humo imo chemchem inayo miminika.
ﯕﯖﯗﯘ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
ﯙﯚﯛ
Na bilauri zilizo pangwa,
ﯜﯝﯞ
Na matakia safu safu,
ﯟﯠﯡ
Na mazulia yaliyo tandikwa.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
ﯩﯪﯫﯬﯭ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
ﯮﯯﯰﯱﯲ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
ﯳﯴﯵﯶﯷ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
ﯸﯹﯺﯻﯼ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
ﯽﯾﯿﰀ
Wewe si mwenye kuwatawalia.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
ﭖﭗﭘﭙﭚ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
ﭛﭜﭝﭞ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema