Sura Al-Ghashiya
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Ghashiya pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Ghashiya pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Ghashiya Tafsiri. Al-Ghashiya (Makka) 26 Aya.
Related
- Al-Ghashiya TafsiriKiswahili
- Al-Ghashiya mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Ghashiya

ﭽﭾﭿﮀﮁ
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
ﮂﮃﮄﮅ
Siku hiyo nyuso zitainama,
ﮆﮇﮈ
Zikifanya kazi, nazo taabani.
ﮉﮊﮋﮌ
Ziingie katika Moto unao waka -
ﮍﮎﮏﮐﮑ
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
ﮠﮡﮢﮣ
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
ﮤﮥﮦ
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
ﮧﮨﮩﮪ
Katika Bustani ya juu.
ﮫﮬﮭﮮﮯ
Hawatasikia humo upuuzi.
ﮰﮱﯓﯔ
Humo imo chemchem inayo miminika.
ﯕﯖﯗﯘ
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
ﯙﯚﯛ
Na bilauri zilizo pangwa,
ﯜﯝﯞ
Na matakia safu safu,
ﯟﯠﯡ
Na mazulia yaliyo tandikwa.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
ﯩﯪﯫﯬﯭ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
ﯮﯯﯰﯱﯲ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
ﯳﯴﯵﯶﯷ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
ﯸﯹﯺﯻﯼ
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
ﯽﯾﯿﰀ
Wewe si mwenye kuwatawalia.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
ﭖﭗﭘﭙﭚ
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
ﭛﭜﭝﭞ
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







