Sura Al-Waqi'a
PDF —
96 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Waqi'a pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Waqi'a pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Waqi'a Tafsiri. Al-Waqi'a (Makka) 96 Aya.



Sura Al-Waqi'a
96 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮃﮄﮅﮆ
Litakapo tukia hilo Tukio
ﮇﮈﮉﮊ
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
ﮋﮌﮍ
Literemshalo linyanyualo,
ﮎﮏﮐﮑﮒ
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
ﮓﮔﮕﮖ
Na milima itapo sagwasagwa,
ﮗﮘﮙﮚ
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
ﮛﮜﮝﮞ
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
ﮫﮬﮭ
Na wa mbele watakuwa mbele.
ﮮﮯﮰ
Hao ndio watakao karibishwa
ﮱﯓﯔﯕ
Katika Bustani zenye neema.
ﯖﯗﯘﯙ
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
ﯚﯛﯜﯝ
Na wachache katika wa mwisho.
ﯞﯟﯠﯡ
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
ﯢﯣﯤﯥ
Wakiviegemea wakielekeana.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
ﭢﭣﭤﭥ
Na matunda wayapendayo,
ﭦﭧﭨﭩﭪ
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
ﭫﭬﭭ
Na Mahurulaini,
ﭮﭯﭰﭱ
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
ﭲﭳﭴﭵﭶ
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
ﭾﭿﮀﮁﮂ
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
ﮉﮊﮋﮌ
Katika mikunazi isiyo na miba,
ﮍﮎﮏ
Na migomba iliyo pangiliwa,
ﮐﮑﮒ
Na kivuli kilicho tanda,
ﮓﮔﮕ
Na maji yanayo miminika,
ﮖﮗﮘ
Na matunda mengi,
ﮙﮚﮛﮜﮝ
Hayatindikii wala hayakatazwi,
ﮞﮟﮠ
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
ﮡﮢﮣﮤ
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
ﮥﮦﮧ
Na tutawafanya vijana,
ﮨﮩﮪ
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
ﮫﮬﮭ
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ﮮﮯﮰﮱ
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
ﯓﯔﯕﯖ
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
ﯝﯞﯟﯠ
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
ﯡﯢﯣﯤ
Na kivuli cha moshi mweusi,
ﯥﯦﯧﯨﯩ
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
ﰀﰁﰂ
Au baba zetu wa zamani?
ﰃﰄﰅﰆﰇ
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
ﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
ﭝﭞﭟﭠ
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
ﭡﭢﭣﭤﭥ
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
ﭦﭧﭨﭩ
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
ﭪﭫﭬﭭﭮ
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
ﭯﭰﭱﭲﭳ
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
ﭴﭵﭶﭷ
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
ﮗﮘﮙﮚ
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
ﮨﮩﮪ
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
ﮫﮬﮭﮮ
Bali sisi tumenyimwa.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
ﯤﯥﯦﯧﯨ
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
ﭑﭒﭓﭔ
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
ﭕﭖﭗﭘ
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
ﭙﭚﭛﭜﭝ
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
ﭞﭟﭠﭡﭢ
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﭣﭤﭥﭦﭧ
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
ﭨﭩﭪﭫﭬ
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
ﭭﭮﭯﭰﭱ
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
ﭲﭳﭴﭵ
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
ﮄﮅﮆﮇﮈ
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
ﮨﮩﮪﮫ
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
ﮬﮭﮮ
Na kutiwa Motoni.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
ﯖﯗﯘﯙﯚ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema