Sura Al-Waqi'a pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Waqi'a pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Waqi'a Tafsiri. Sura Al-Waqi'a (Makka) 96 Aya.
Related
- Sura Al-Waqi'a TafsiriKiswahili
- Sura Al-Waqi'a mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Waqi'a

ﮃﮄﮅﮆ
56:1
Litakapo tukia hilo Tukio
ﮇﮈﮉﮊ
56:2
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
ﮋﮌﮍ
56:3
Literemshalo linyanyualo,
ﮎﮏﮐﮑﮒ
56:4
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
ﮓﮔﮕﮖ
56:5
Na milima itapo sagwasagwa,
ﮗﮘﮙﮚ
56:6
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
ﮛﮜﮝﮞ
56:7
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
56:8
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
56:9
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
ﮫﮬﮭ
56:10
Na wa mbele watakuwa mbele.
ﮮﮯﮰ
56:11
Hao ndio watakao karibishwa
ﮱﯓﯔﯕ
56:12
Katika Bustani zenye neema.
ﯖﯗﯘﯙ
56:13
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
ﯚﯛﯜﯝ
56:14
Na wachache katika wa mwisho.
ﯞﯟﯠﯡ
56:15
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
ﯢﯣﯤﯥ
56:16
Wakiviegemea wakielekeana.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
56:17
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
56:18
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
56:19
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
ﭢﭣﭤﭥ
56:20
Na matunda wayapendayo,
ﭦﭧﭨﭩﭪ
56:21
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
ﭫﭬﭭ
56:22
Na Mahurulaini,
ﭮﭯﭰﭱ
56:23
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
ﭲﭳﭴﭵﭶ
56:24
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
56:25
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
ﭾﭿﮀﮁﮂ
56:26
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
56:27
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
ﮉﮊﮋﮌ
56:28
Katika mikunazi isiyo na miba,
ﮍﮎﮏ
56:29
Na migomba iliyo pangiliwa,
ﮐﮑﮒ
56:30
Na kivuli kilicho tanda,
ﮓﮔﮕ
56:31
Na maji yanayo miminika,
ﮖﮗﮘ
56:32
Na matunda mengi,
ﮙﮚﮛﮜﮝ
56:33
Hayatindikii wala hayakatazwi,
ﮞﮟﮠ
56:34
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
ﮡﮢﮣﮤ
56:35
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
ﮥﮦﮧ
56:36
Na tutawafanya vijana,
ﮨﮩﮪ
56:37
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
ﮫﮬﮭ
56:38
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ﮮﮯﮰﮱ
56:39
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
ﯓﯔﯕﯖ
56:40
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
56:41
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
ﯝﯞﯟﯠ
56:42
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
ﯡﯢﯣﯤ
56:43
Na kivuli cha moshi mweusi,
ﯥﯦﯧﯨﯩ
56:44
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
56:45
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
56:46
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
56:47
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
ﰀﰁﰂ
56:48
Au baba zetu wa zamani?
ﰃﰄﰅﰆﰇ
56:49
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
ﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
56:50
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
56:51
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
56:52
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
ﭝﭞﭟﭠ
56:53
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
ﭡﭢﭣﭤﭥ
56:54
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
ﭦﭧﭨﭩ
56:55
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
ﭪﭫﭬﭭﭮ
56:56
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
ﭯﭰﭱﭲﭳ
56:57
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
ﭴﭵﭶﭷ
56:58
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
56:59
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
56:60
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
56:61
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
56:62
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
ﮗﮘﮙﮚ
56:63
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
56:64
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
56:65
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
ﮨﮩﮪ
56:66
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
ﮫﮬﮭﮮ
56:67
Bali sisi tumenyimwa.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
56:68
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
56:69
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
56:70
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
ﯤﯥﯦﯧﯨ
56:71
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
56:72
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
56:73
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
56:74
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
56:75
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
56:76
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
ﭑﭒﭓﭔ
56:77
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
ﭕﭖﭗﭘ
56:78
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
ﭙﭚﭛﭜﭝ
56:79
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
ﭞﭟﭠﭡﭢ
56:80
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﭣﭤﭥﭦﭧ
56:81
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
ﭨﭩﭪﭫﭬ
56:82
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
ﭭﭮﭯﭰﭱ
56:83
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
ﭲﭳﭴﭵ
56:84
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
56:85
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
56:86
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
ﮄﮅﮆﮇﮈ
56:87
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
56:88
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
56:89
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
56:90
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
56:91
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
56:92
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
ﮨﮩﮪﮫ
56:93
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
ﮬﮭﮮ
56:94
Na kutiwa Motoni.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
56:95
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
ﯖﯗﯘﯙﯚ
56:96
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







