Sura An-Najm
62 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔ
Naapa kwa nyota inapo tua,
ﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
ﭛﭜﭝﭞﭟ
Wala hatamki kwa matamanio.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
ﭦﭧﭨﭩ
Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
ﭪﭫﭬﭭ
Mwenye kutua, akatulia,
ﭮﭯﭰﭱ
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
ﭲﭳﭴﭵ
Kisha akakaribia na akateremka.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
ﮈﮉﮊﮋﮌ
Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
ﮍﮎﮏﮐﮑ
Na akamwona mara nyingine,
ﮒﮓﮔﮕ
Penye Mkunazi wa mwisho.
ﮖﮗﮘﮙ
Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
ﮭﮮﮯﮰ
Je! Mmemuona Lata na Uzza?
ﮱﯓﯔﯕ
Na Manaat, mwingine wa tatu?
ﯖﯗﯘﯙﯚ
Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
ﯛﯜﯝﯞﯟ
Huo ni mgawanyo wa dhulma!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
ﯼﯽﯾﯿﰀ
Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
ﰁﰂﰃﰄ
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘ
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.
ﯢﯣﯤﯥ
Je! Umemwona yule aliye geuka?
ﯦﯧﯨﯩ
Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
ﯸﯹﯺﯻ
Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?
ﰉﰊﰋﰌﰍ
Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
ﰎﰏﰐﰑﰒ
Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.
ﰓﰔﰕﰖﰗ
Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.
ﰘﰙﰚﰛﰜ
Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.
ﰝﰞﰟﰠﰡ
Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
ﭗﭘﭙﭚﭛ
Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
ﭜﭝﭞﭟﭠ
Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
ﭡﭢﭣﭤﭥ
Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
ﭦﭧﭨﭩﭪ
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
ﭫﭬﭭﭮﭯ
Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
ﭰﭱﭲﭳ
Na Thamudi hakuwabakisha,
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
ﭿﮀﮁ
Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
ﮂﮃﮄﮅ
Vikaifunika vilivyo funika.
ﮆﮇﮈﮉﮊ
Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
ﮑﮒﮓ
Kiyama kimekaribia!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
Je! Mnayastaajabia maneno haya?
ﮠﮡﮢﮣ
Na mnacheka, wala hamlii?
ﮤﮥﮦ
Nanyi mmeghafilika?
ﮧﮨﮩﮪﮫ
Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema