Sura Al-Jinn
28 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Sema: Imefunuliwa kwangu ya kuwa kundi moja la majini lilisikiliza, na likasema: Hakika sisi tumeisikia Qur'ani ya ajabu!
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Inaongoza kwenye uwongofu, kwa hivyo tumeiamini, wala hatutamshirikisha yeyote na Mola wetu Mlezi.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu Mlezi umetukuka kabisa; hana mke wala mwana.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na kwa hakika wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema uwongo ulio pindukia mipaka juu ya Mwenyezi Mungu.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Nasi tulidhani kuwa watu na majini hawamzulii uwongo Mwenyezi Mungu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Na kwa hakika wao walidhani, kama mlivyo dhani nyinyi, ya kuwa Mwenyezi Mungu hatamleta Mtume.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Nasi tulizigusa mbingu, na tukaziona zimejaa walinzi wenye nguvu na vimondo.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Na hakika tulikuwa tukikaa humo katika baadhi ya makao ili kusikiliza; lakini sasa anaye taka kusikiliza atakuta kimondo kinamvizia!
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Nasi hatujui kama wanatakiwa shari wale wanao kaa kwenye ardhi au Mola wao Mlezi anawatakia uwongofu.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Na hakika katika sisi wamo walio wema, na wengine wetu ni kinyume na hivyo. Tumekuwa njia mbali mbali.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Nasi tulijua kuwa hatutomshinda Mwenyezi Mungu duniani, wala hatuwezi kumponyoka kwa kukimbia.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Nasi tulipo usikia uwongofu tuliuamini. Basi mwenye kumuamini Mola wake Mlezi basi haogopi kupunjwa wala kudhulumiwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
Na hakika wamo katika sisi Waislamu, na wamo kati yetu wanao acha haki. Basi walio silimu, hao ndio walio tafuta uwongofu.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Na ama wanao acha haki, hao watakuwa kuni za Jahannamu.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Na lau kama wangeli simama sawasawa juu ya njia tungeli wanywesha maji kwa wingi,
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Ili tuwajaribu kwa hayo. Na anaye puuza kumkumbuka Mola wake Mlezi atamsukuma kwenye adhabu ngumu.
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu, basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Na hakika Mja wa Mwenyezi Mungu alipo simama kumwomba, wao walikuwa karibu kumzonga!
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Sema: Hakika mimi namwomba Mola wangu Mlezi, wala simshirikishi Yeye na yeyote.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Sema: Mimi sina mamlaka ya kukudhuruni wala kukuongozeni.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Sema: Hakika hapana yeyote awezae kunilinda na Mwenyezi Mungu, wala sitapata pa kukimbilia isipo kuwa kwake Yeye tu.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Ila nifikishe Ujumbe utokao kwa Mwenyezi Mungu na risala zake. Na wenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannamu wadumu humo milele.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
Hata watakapo yaona wanayo ahidiwa, ndipo watakapo jua ni nani mwenye msaidizi dhaifu, na mchache wa idadi.
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Sema: Sijui kama yapo karibu hayo mnayo ahidiwa, au Mola wangu Mlezi atayawekea muda mrefu.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
Yeye ndiye Mwenye kujua ya siri, wala hamdhihirishii yeyote siri yake,
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Isipo kuwa Mtume wake aliye mridhia. Naye huyo humwekea walinzi mbele yake na nyuma yake.
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘ
Ili Yeye ajue kwamba wao wamefikisha ujumbe wa Mola wao Mlezi, na Yeye anayajua vyema yote walio nayo, na amedhibiti idadi ya kila kitu.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema