Sura Qaf
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Qaf pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Qaf pdf Kiswahili — Pakua Sura Qaf Tafsiri. Qaf (Makka) 45 Aya.
Related
- Qaf TafsiriKiswahili
- Qaf mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Qaf

ﭑﭒﭓﭔﭕ
Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
ﯤﯥﯦﯧﯨ
Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
(Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
ﮨﮩﮪﮫﮬ
Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
(Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea-
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛﰜ
(Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
ﰝﰞﰟﰠﰡﰢﰣ
Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







