45 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔﭕ
50:1 Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
50:2 Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
50:3 Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
50:4 Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
50:5 Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
50:6 Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
50:7 Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
50:8 Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
50:9 Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
50:10 Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
50:11 Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
50:12 Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
ﯤﯥﯦﯧﯨ
50:13 Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
50:14 Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
50:15 Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
50:16 Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
50:17 Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
50:18 Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
50:19 Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
50:20 Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
50:21 Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
50:22 (Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
50:23 Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
50:24 Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
ﮨﮩﮪﮫﮬ
50:25 Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
50:26 Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
50:27 Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
50:28 (Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
50:29 Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
50:30 Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
50:31 Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
50:32 Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
50:33 Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea-
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛﰜ
50:34 (Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
ﰝﰞﰟﰠﰡﰢﰣ
50:35 Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
50:36 Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
50:37 Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
50:38 Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
50:39 Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
50:40 Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
50:41 Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
50:42 Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
50:43 Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
50:44 Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
50:45 Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema