Sura Maryam
98 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒ
Kaf Ha Ya A'yn S'ad
ﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Huu ni Ukumbusho wa rehema ya Mola wako Mlezi kwa mja wake, Zakariya.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Alipo mwita Mola wake Mlezi kwa siri.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Mafupa yangu yamedhoofika, na kichwa kinameremeta kwa mvi; wala, Mola wangu Mlezi, sikuwa mwenye bahati mbaya kwa kukuomba Wewe.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na hakika mimi nawakhofia jamaa zangu baada yangu. Na mke wangu ni tasa. Basi nipe mrithi kutoka kwako.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Atakaye nirithi mimi na awarithi ukoo wa Yaaqub. Ewe Mola wangu Mlezi! Na umjaalie awe mwenye kuridhisha.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
(Akaambiwa): Ewe Zakariya! Hakika Sisi tunakubashiria mwana; jina lake ni Yahya. Hatujapata kumpa jina hilo yeyote kabla yake.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Vipi nitakuwa na mwana na hali mke wangu ni tasa, na mimi nimesha fikia ukongwe katika uzee?
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
Akasema: Ndio hivyo hivyo amesema Mola wako Mlezi: Haya ni mepesi kwangu. Na hakika Mimi nilikwisha kuumba wewe zamani na hali hukuwa kitu.
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Akasema: Mola wangu Mlezi nijaalie Ishara. Akasema Ishara yako ni kuwa hutasema na watu kwa masiku matatu, na hali ni mzima.
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Basi akawatokea watu wake kutoka mihirabuni. Akawaashiria: Msabihini Mwenyezi Mungu asubuhi na jioni.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Ewe Yahya! Kishike Kitabu kwa nguvu! Nasi tulimpa hikima angali mtoto.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Na tukampa huruma itokayo kwetu, na utakaso, na akawa mchamungu.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Na akawa mwema kwa wazazi wake, wala hakuwa jabari mua'si.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na amani iwe juu yake siku ya kuzaliwa, na siku ya kufa, na siku ya kufufuliwa.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Na mtaje Maryamu katika Kitabu, pale alipo jitenga na jamaa zake mahali upande wa mashariki;
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea Roho wetu, akajifananisha kwake sawa na mtu.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
(Maryamu) akasema: Hakika mimi najikinga kwa Mwingi wa Rehema aniepushe nawe, ukiwa ni mchamngu.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
(Malaika) akasema: Hakika mimi ni mwenye kutumwa na Mola wako Mlezi ili nikubashirie tunu ya mwana aliye takasika.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
Akasema: Nitampataje mwana hali mwanaadamu yeyote hajanigusa, wala mimi si kahaba?
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
(Malaika) akasema: Ndio hivyo hivyo! Mola wako Mlezi amesema: Haya ni mepesi kwangu! Na ili tumfanye kuwa ni Ishara kwa watu, na Rehema itokayo kwetu, na hilo ni jambo lilio kwisha hukumiwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Kisha uchungu ukampeleka kwenye shina la mtende; akasema: Laiti ningeli kufa kabla ya haya, na nikawa niliye sahaulika kabisa!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Pakatangazwa kutoka chini yake: Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji!
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Akenda naye (mwanawe) kwa jamaa zake amembeba. Wakasema: Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Ewe dada yake Harun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Akawaashiria (mtoto). Wakasema: Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi?
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
(Mtoto) akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu, na amenifanya Nabii.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia Sala na Zaka maadamu ni hai,
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
Na amani iko juu yangu siku niliyo zaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
Huyo ndiye Isa mwana wa Maryamu. Ndiyo kauli ya haki ambayo wanaifanyia shaka.
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Haiwi kwa Mwenyezi Mungu kuwa na mwana, Subhanahu, Yeye ametakasika! Anapo lihukumia jambo basi huliambia tu: Kuwa! Likawa.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Lakini makundi yakakhitalifiana wao kwa wao. Basi ole wao hao walio kufuru kwa kuhudhuria Siku iliyo kuu!
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
Watasikia na wataona vizuri vilioje Siku watakayo tufikia! Lakini madhaalimu sasa wamo katika upotofu ulio dhaahiri.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Na waonye siku ya majuto itapo katwa amri. Nao wamo katika ghafla, wala hawaamini.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Hakika Sisi tutairithi ardhi na walio juu yake. Na kwetu watarejeshwa.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Na mtaje katika Kitabu Ibrahim. Hakika yeye alikuwa mkweli, Nabii.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Alipo mwambia baba yake: Ewe baba yangu! Kwa nini unaabudu visivyo sikia, na visivyo ona, na visivyo kufaa chochote?
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Ewe baba yangu! Kwa yakini imenifikia ilimu isiyo kufikia wewe. Basi nifuate mimi, nami nitakuongoza Njia Iliyo Sawa.
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Ewe baba yangu! Usimuabudu Shet'ani. Hakika Shet'ani ni mwenye kumuasi Mwingi wa Rehema.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Ewe baba yangu! Hakika mimi naogopa isikupate adhabu inayo toka kwa Mwingi wa Rehema ukaja kuwa mwenziwe Shet'ani.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
(Baba) akasema: Unaichukia miungu yangu, ewe Ibrahim? Kama huachi, basi lazima nitakupiga mawe. Na niondokelee mbali kwa muda!
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
(Ibrahim) akasema: Salamun a'laika! Amani iwe juu yako! Mimi nitakuombea msamaha kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ananihurumia sana.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Nami najitenga nanyi na hayo mnayo yaabudu badala ya Mwenyezi Mungu. Na ninamwomba Mola wangu Mlezi; asaa nisiwe mwenye kukosa bahati kwa kumwomba Mola wangu Mlezi.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Basi alipo jitenga nao na yale waliyo kuwa wakiyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu, tulimpa Is-haq na Yaaqub, na kila mmoja tukamfanya Nabii.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
Na tukawapa rehema zetu na tukawajaalia kupewa sifa za kweli tukufu.
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
Na mtaje Musa katika Kitabu. Hakika yeye alikuwa ni mwenye kuchaguliwa, na alikuwa Mtume, Nabii.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Na tulimwita upande wa kulia wa mlima na tukamsogeza kunong'ona naye.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Nasi kwa rehema zetu tukampa nduguye, Harun, awe Nabii.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Na mtaje katika Kitabu Ismail. Bila ya shaka yeye alikuwa ni mkweli wa ahadi, na alikuwa Mtume, Nabii.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Na alikuwa akiwaamrisha watu wake Sala na Zaka, na alikuwa mbele ya Mola wake Mlezi mwenye kuridhiwa.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Na mtaje katika Kitabu Idris. Hakika yeye alikuwa ni mkweli Nabii.
ﮂﮃﮄﮅ
Na tulimuinua daraja ya juu.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Hao ndio alio waneemesha Mwenyezi Mungu miongoni mwa Manabii katika uzao wa Adam, na katika uzao wa wale tulio wapandisha pamoja na Nuhu, na katika uzao wa Ibrahim na Israil, na katika wale tulio waongoa na tukawateuwa. Wanapo somewa Aya za Mwingi wa Rehema huanguka kusujudu na kulia.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Lakini wakaja baada yao walio wabaya, wakaacha Sala, na wakafuata matamanio. Basi watakuja kuta malipo ya ubaya.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Isipo kuwa walio tubu, wakaamini, na wakatenda mema. Hao, basi, wataingia Peponi wala hawatadhulumiwa chochote.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
Bustani za milele alizo waahidi Rahmani waja wake katika siri. Hakika ahadi yake hapana shaka itafika.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Humo hawatasikia upuuzi, ila Salama tu. Na watapata humo riziki zao asubuhi na jioni.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Hiyo ndiyo Pepo tutayo warithisha katika waja wetu walio kuwa wachamngu.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘﰙﰚ
(Nao watasema:) Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako Mlezi. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu, na yaliyomo katikati ya hayo. Na Mola wako Mlezi si mwenye kusahau.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake. Basi muabudu Yeye tu, na udumu katika ibada yake. Je, mnamjua mwenye jina kama lake?
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
Na mwanaadamu husema: Hivyo, nitakapo kufa, ni kweli nitafufuliwa niwe hai tena?
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Je! Hakumbuki mwanaadamu ya kwamba tulimuumba kabla, na hali hakuwa chochote?
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Basi naapa kwa Mola wako Mlezi! Kwa yakini tutawakusanya wao pamoja na mashet'ani; kisha tutawahudhurisha kuizunguka Jahannamu, nao wamepiga magoti!
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Kisha kwa yakini tutawatoa katika kila kundi wale miongoni mwao walio zidi kumuasi Arrahmani, Mwingi wa Rahema..
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Tena hakika Sisi tunawajua vyema zaidi wanao stahiki kuunguzwa humo.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Wala hapana yeyote katika nyinyi ila ni mwenye kuifikia. Hiyo ni hukumu ya Mola wako Mlezi ambayo lazima itimizwe.
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Kisha tutawaokoa wale walio mchamngu; na tutawaacha madhaalimu humo wamepiga magoti.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Na wanapo somewa Aya zetu zilizo wazi, walio kufuru huwaambia walio amini: Lipi katika makundi mawili lenye cheo kizuri na lilio bora barazani?
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Na kaumu ngapi tuliziangamiza zilizo kuwa na mapambo mazuri zaidi na wazuri zaidi kwa kuwatazama!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Sema: Walio katika upotofu basi Arrahmani Mwingi wa Rahema atawapururia muda mpaka wayaone waliyo onywa - ama ni adhabu au ni Saa. Hapo ndipo watapo jua ni nani mwenye makao mabaya na mwenye askari dhaifu.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Na Mwenyezi Mungu huwazidishia uwongofu wenye kushika uwongofu. Na mema yenye kudumu ni bora katika malipo mbele ya Mola wako Mlezi na yana mwisho mwema.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Je, umemwona aliye zikanya Ishara zetu na akasema: Kwa hakika mimi nitapewa mali na wana!
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Kwani yeye amepata khabari za ghaibu, au amechukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema?
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Hasha! Tutaandika anayo yasema, tutamkunjulia muda wa adhabu.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na tutamrithi hayo anayo yasema, na atatufikia mtupu peke yake!
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na wamechukua miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati iwape nguvu.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Sivyo kabisa! Wataikataa hiyo ibada yao, na watakuwa ndio dhidi yao.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Kwani huoni ya kwamba tumewatuma mashet'ani kwa makafiri wawachochee kwa uchochezi?
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Basi usiwafanyie haraka. Sisi tunawahisabia idadi ya siku zao.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Siku tutayo wakusanya wachamngu kuwapeleka kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni wageni wake.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Na tukawachunga wakhalifu kuwapeleka Jahannamu hali ya kuwa wana kiu.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale walio chukua ahadi kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema..
ﮮﮯﮰﮱﯓ
Na wao ati husema kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana!
ﯔﯕﯖﯗﯘ
Hakika mmeleta jambo la kuchusha mno!
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Zinakaribia mbingu kutatuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande.
ﯣﯤﯥﯦﯧ
Kwa kudai kwao kuwa Arrahmani Mwingi wa Rehema ana mwana.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
Wala hahitajii Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa na mwana.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Hapana yeyote aliomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni mtumwa wake.
ﯺﯻﯼﯽﯾ
Yeye hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa.
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Na kila mmoja katika wao atamfikia Siku ya Kiyama peke yake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur'ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wachamngu, na uwaonye kwayo watu wabishi.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Na kaumu ngapi tumezihiliki kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema