Sura Al-A'la
19 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮟﮠﮡﮢﮣ
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
ﮤﮥﮦﮧ
Aliye umba, na akaweka sawa,
ﮨﮩﮪﮫ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
ﮬﮭﮮﮯ
Na aliye otesha malisho,
ﮰﮱﯓﯔ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
ﯕﯖﯗﯘ
Tutakusomesha wala hutasahau,
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
ﯤﯥﯦ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
ﯧﯨﯩﯪﯫ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
ﯬﯭﯮﯯ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
ﭑﭒﭓ
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
ﭔﭕﭖﭗﭘ
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
ﭠﭡﭢﭣﭤ
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
ﭪﭫﭬﭭﭮ
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
ﭯﭰﭱﭲ
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
ﭹﭺﭻﭼ
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema