PDF —
19 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-A'la pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-A'la pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-A'la Tafsiri. Sura Al-A'la (Makka) 19 Aya.



19 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮟﮠﮡﮢﮣ
87:1 Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
ﮤﮥﮦﮧ
87:2 Aliye umba, na akaweka sawa,
ﮨﮩﮪﮫ
87:3 Na ambaye amekadiria na akaongoa,
ﮬﮭﮮﮯ
87:4 Na aliye otesha malisho,
ﮰﮱﯓﯔ
87:5 Kisha akayafanya makavu, meusi.
ﯕﯖﯗﯘ
87:6 Tutakusomesha wala hutasahau,
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
87:7 Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
ﯤﯥﯦ
87:8 Na tutakusahilishia yawe mepesi.
ﯧﯨﯩﯪﯫ
87:9 Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
ﯬﯭﯮﯯ
87:10 Atakumbuka mwenye kuogopa.
ﭑﭒﭓ
87:11 Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
ﭔﭕﭖﭗﭘ
87:12 Ambaye atauingia Moto mkubwa.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
87:13 Tena humo hatakufa wala hawi hai.
ﭠﭡﭢﭣﭤ
87:14 Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
87:15 Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
ﭪﭫﭬﭭﭮ
87:16 Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
ﭯﭰﭱﭲ
87:17 Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
87:18 Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
ﭹﭺﭻﭼ
87:19 Vitabu vya Ibrahimu na Musa.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema