PDF —
99 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Hijr pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Hijr pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Hijr Tafsiri. Sura Al-Hijr (Makka) 99 Aya.



99 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
15:1 Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
15:2 HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
15:3 Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
15:4 Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
15:5 Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
15:6 Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
15:7 Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
15:8 Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
15:9 Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
15:10 Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
15:11 Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
15:12 Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
15:13 Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
15:14 Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
15:15 Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
15:16 Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
15:17 Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
15:18 Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
15:19 Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
15:20 Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
15:21 Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
15:22 Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
15:23 Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
15:24 Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
15:25 Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
15:26 Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
15:27 Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
15:28 Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
15:29 Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
15:30 Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
15:31 Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
15:32 (Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
15:33 Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
15:34 (Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
15:35 Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
15:36 Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
15:37 (Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
ﭿﮀﮁﮂﮃ
15:38 Mpaka siku ya wakati maalumu.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
15:39 Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
15:40 Ila waja wako walio safika.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
15:41 Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
15:42 Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
ﮦﮧﮨﮩﮪ
15:43 Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
15:44 Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
15:45 Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
ﯛﯜﯝﯞ
15:46 (Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
15:47 Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
15:48 Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
15:49 Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
15:50 Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
ﰁﰂﰃﰄﰅ
15:51 Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
15:52 Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
15:53 Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
15:54 Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
15:55 Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
15:56 Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
15:57 Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
15:58 Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
15:59 Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
15:60 Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
15:61 Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
ﮞﮟﮠﮡﮢ
15:62 Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
15:63 Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
ﮫﮬﮭﮮﮯ
15:64 Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
15:65 Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
15:66 Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
ﯪﯫﯬﯭﯮ
15:67 Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
15:68 Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
15:69 Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
15:70 Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
15:71 Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
15:72 Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
ﭞﭟﭠﭡ
15:73 Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
15:74 Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
15:75 Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
ﭱﭲﭳﭴ
15:76 Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
15:77 Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
15:78 Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
15:79 Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
15:80 Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
15:81 Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
15:82 Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
ﮚﮛﮜﮝ
15:83 Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
15:84 Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
15:85 Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
15:86 Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
15:87 Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
15:88 Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
15:89 Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
ﯻﯼﯽﯾﯿ
15:90 Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
ﭑﭒﭓﭔﭕ
15:91 Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
ﭖﭗﭘﭙ
15:92 Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
ﭚﭛﭜﭝ
15:93 Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
15:94 Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
ﭥﭦﭧﭨ
15:95 Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
15:96 Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
15:97 Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
15:98 Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
15:99 Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema