Sura Al-Hijr
99 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula
ﭿﮀﮁﮂﮃ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Ila waja wako walio safika.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.
ﮦﮧﮨﮩﮪ
Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
ﯛﯜﯝﯞ
(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!
ﰁﰂﰃﰄﰅ
Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,
ﮞﮟﮠﮡﮢ
Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.
ﮫﮬﮭﮮﮯ
Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.
ﯪﯫﯬﯭﯮ
Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
ﭞﭟﭠﭡ
Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.
ﭱﭲﭳﭴ
Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
ﮚﮛﮜﮝ
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.
ﯻﯼﯽﯾﯿ
Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.
ﭖﭗﭘﭙ
Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,
ﭚﭛﭜﭝ
Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.
ﭥﭦﭧﭨ
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema