Sura Al-Haqqa pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Haqqa pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Haqqa Tafsiri. Sura Al-Haqqa (Makka) 52 Aya.
Related
- Sura Al-Haqqa TafsiriKiswahili
- Sura Al-Haqqa mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Haqqa

ﮯﮰ
69:1
Tukio la haki.
ﮱﯓﯔ
69:2
Nini hilo Tukio la haki?
ﯕﯖﯗﯘﯙ
69:3
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
ﯚﯛﯜﯝﯞ
69:4
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
69:5
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
69:6
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
69:7
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
69:8
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
69:9
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
69:10
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
69:11
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
69:12
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
69:13
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
69:14
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
ﭼﭽﭾﭿ
69:15
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
69:16
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
69:17
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
69:18
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
69:19
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
69:20
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
ﮨﮩﮪﮫﮬ
69:21
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
ﮭﮮﮯﮰ
69:22
Katika Bustani ya juu,
ﮱﯓﯔ
69:23
Matunda yake yakaribu.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
69:24
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
69:25
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
ﯩﯪﯫﯬﯭ
69:26
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
ﯮﯯﯰﯱ
69:27
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
69:28
Mali yangu hayakunifaa kitu.
ﯸﯹﯺﯻ
69:29
Madaraka yangu yamenipotea.
ﯼﯽﯾ
69:30
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
ﯿﰀﰁﰂ
69:31
Kisha mtupeni Motoni!
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
69:32
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
69:33
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
69:34
Wala hahimizi kulisha masikini.
ﰘﰙﰚﰛﰜﰝ
69:35
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
69:36
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
ﭗﭘﭙﭚﭛ
69:37
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
ﭜﭝﭞﭟﭠ
69:38
Basi naapa kwa mnavyo viona,
ﭡﭢﭣﭤ
69:39
Na msivyo viona,
ﭥﭦﭧﭨﭩ
69:40
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
69:41
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
69:42
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
ﭻﭼﭽﭾﭿ
69:43
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
69:44
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
ﮆﮇﮈﮉ
69:45
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
ﮊﮋﮌﮍﮎ
69:46
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
69:47
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
ﮖﮗﮘﮙ
69:48
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
69:49
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
ﮠﮡﮢﮣﮤ
69:50
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
ﮥﮦﮧﮨ
69:51
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
69:52
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







