Sura Al-Haqqa
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Haqqa pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Haqqa pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Haqqa Tafsiri. Al-Haqqa (Makka) 52 Aya.
Related
- Al-Haqqa TafsiriKiswahili
- Al-Haqqa mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Haqqa

ﮯﮰ
Tukio la haki.
ﮱﯓﯔ
Nini hilo Tukio la haki?
ﯕﯖﯗﯘﯙ
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
ﯚﯛﯜﯝﯞ
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
ﭼﭽﭾﭿ
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
ﮨﮩﮪﮫﮬ
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
ﮭﮮﮯﮰ
Katika Bustani ya juu,
ﮱﯓﯔ
Matunda yake yakaribu.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨ
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
ﯩﯪﯫﯬﯭ
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
ﯮﯯﯰﯱ
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Mali yangu hayakunifaa kitu.
ﯸﯹﯺﯻ
Madaraka yangu yamenipotea.
ﯼﯽﯾ
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
ﯿﰀﰁﰂ
Kisha mtupeni Motoni!
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
Wala hahimizi kulisha masikini.
ﰘﰙﰚﰛﰜﰝ
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
ﭗﭘﭙﭚﭛ
Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
ﭜﭝﭞﭟﭠ
Basi naapa kwa mnavyo viona,
ﭡﭢﭣﭤ
Na msivyo viona,
ﭥﭦﭧﭨﭩ
Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
ﭻﭼﭽﭾﭿ
Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
ﮆﮇﮈﮉ
Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
ﮊﮋﮌﮍﮎ
Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
ﮖﮗﮘﮙ
Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.
ﮠﮡﮢﮣﮤ
Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
ﮥﮦﮧﮨ
Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







