135 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭵﭶ
T'AHA!
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Hatukukuteremshia Qur'ani ili upate mashaka.
ﭽﭾﭿﮀﮁ
Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Materemsho yatokayo kwa aliye umba ardhi na mbingu zilizo juu.
ﮉﮊﮋﮌﮍ
Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi.
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na duni kuliko siri.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Mwenyezi Mungu! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa.
ﮭﮮﮯﮰﮱ
Na je! Imekufikia hadithi ya Musa?
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto.
ﯦﯧﯨﯩﯪ
Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Musa!
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Hakika Saa itakuja bila ya shaka. Nimekaribia kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Kwa hivyo asikukengeushe nayo yule ambaye haiamini na akafuata pumbao lake ukaja kuhiliki.
ﭹﭺﭻﭼﭽ
Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine.
ﮌﮍﮎﮏ
Akasema: Itupe, ewe Musa!
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Na uambatishe mkono wako kwenye ubavu. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine.
ﮫﮬﮭﮮﮯ
Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,
ﯝﯞﯟﯠ
Na unifanyie nyepesi kazi yangu,
ﯡﯢﯣﯤﯥ
Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,
ﯦﯧﯨ
Wapate kufahamu maneno yangu.
ﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
Na nipe waziri katika watu wangu,
ﯯﯰﯱ
Harun, ndugu yangu.
ﯲﯳﯴﯵ
Kwake yeye niongeze nguvu zangu.
ﯶﯷﯸﯹ
Na umshirikishe katika kazi yangu.
ﯺﯻﯼﯽ
Ili tukutakase sana.
ﯾﯿﰀ
Na tukukumbuke sana.
ﰁﰂﰃﰄﰅ
Hakika Wewe unatuona.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
Akasema: Hakika Umepewa maombi yako, ewe Musa!
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
Na hakika tulikwisha kufanyia hisani mara nyengine...
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Pale tulipo mfunulia mama yako yaliyo funuliwa,
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Ya kuwa mtie katika kisanduku, na kisha kitie mtoni, na mto utamfikisha ufukweni. Atamchukua adui yangu naye ni adui yake. Na nimekutilia mapenzi yanayo tokana kwangu, na ili ulelewe machoni mwangu.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Dada yako alipo kwenda na akasema: Je! Nikujuulisheni mtu wa kuweza kumlea? Basi tukakurejesha kwa mama yako ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike. Na ulimuuwa mtu, nasi tukakuokoa katika dhiki, na tukakujaribu kwa majaribio mengi. Ukakaa miaka kwa watu wa Madyana. Kisha ukaja kama ilivyo kadiriwa, ewe Musa!
ﮖﮗﮘ
Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Nenda, wewe na ndugu yako, pamoja na ishara zangu, wala msichoke kunikumbuka.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Nendeni kwa Firauni. Hakika yeye amepindukia mipaka.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
Mwambieni maneno laini, huenda akazingatia au akaogopa.
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tunaogopa asije akapindukia mipaka juu yetu au kufanya jeuri.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Akasema: Msiogope! Hakika Mimi ni pamoja nanyi. Nasikia na ninaona.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Basi mwendeeni, na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola wako Mlezi! Basi waache Wana wa Israili watoke nasi, wala usiwaadhibu. Sisi tumekuletea ishara itokayo kwa Mola wako Mlezi. Na amani itakuwa juu ya aliye fuata uwongofu.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
Hakika tumefunuliwa sisi kwamba hapana shaka adhabu itamsibu anaye kadhibisha na akapuuza.
ﰉﰊﰋﰌﰍ
(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
Akasema: Mola wetu Mlezi ni yule aliye kipa kila kitu umbo lake, kisha akakiongoa.
ﰘﰙﰚﰛﰜﰝ
Akasema: Nini hali ya karne za kwanza?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Akasema: Ilimu yake iko kwa Mola wangu Mlezi katika Kitabu. Mola wangu Mlezi hapotei wala hasahau.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Ambaye amekufanyieni ardhi kuwa tandiko, na akakupitishieni humo njia, na akakuteremshieni kutoka mbinguni maji. Na kwa hayo tukatoa namna mbali mbali za mimema.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Kuleni, na mchunge wanyama wenu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa wenye akili.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Na hakika tulimwonyesha ishara zetu zote. Lakini alikadhibisha na akakataa.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Akasema: Ewe Musa! Hivyo umetujia kututoa katika nchi yetu kwa uchawi wako?
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Basi sisi hakika tutakueletea uchawi kama huo. Basi weka miadi baina yetu na wewe, ambayo tusiivunje sisi wala wewe, mahali patapo kuwa sawa.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Akasema: Miadi yenu ni siku ya Sikukuu; na watu wakusanywe kabla ya adhuhuri.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Basi Firauni akarudi na akatengeneza hila yake, kisha akaja.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Musa akamwambia: Ole wenu! Msimzulie Mwenyezi Mungu uwongo, asije akakufutilieni mbali kwa adhabu. Na mwenye kuzua lazima ashindwe!
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Basi wakazozana kwa shauri yao wenyewe kwa wenyewe, na wakanong'ona kwa siri.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Wakasema: Hakika hawa wawili ni wachawi, wanataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wao, na waondoe mila zenu zilizo bora kabisa.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Kwa hivyo kusanyeni hila zenu zote, kisha mfike kwa kujipanga safu, na kwa yakini atafuzu kweli kweli leo atakaye shinda.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
Wakasema: Ewe Musa! Je! Utatupa wewe, au tutakuwa sisi wa kwanza kutupa?
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Akasema: Bali tupeni nyinyi! Tahamaki kamba zao na fimbo zao zikaonekana mbele yake, kwa uchawi wao, kuwa zinapiga mbio.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Basi Musa akaingia khofu nafsi yake.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Tukasema: Usikhofu! Hakika wewe ndiye utakaye shinda.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Na kitupe kilicho katika mkono wako wa kulia; kitavimeza walivyo viunda. Hakika walivyo unda ni hila za mchawi tu, na mchawi hafanikiwi popote afikapo.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Basi wachawi wakaangushwa wanasujudu. Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa Harun na Musa!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
(Firauni) akasema: Oh! Mnamuamini kabla sijakupeni ruhusa? Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliye kufundisheni uchawi. Basi kwa yakini nitakukateni mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakutundikeni misalabani katika vigogo vya mitende, na hapo kwa yakini mtajua ni nani katika sisi aliye mkali wa kuadhibu na kuiendeleza adhabu yake.
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Wakasema: Hatutokukhiari wewe kuliko ishara waziwazi zilizo tujia, na kuliko yule aliye tuumba. Basi hukumu utavyo hukumu; kwani wewe unahukumu haya ya maisha ya duniani tu.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Hakika sisi tumemuamini Mola wetu Mlezi ili atusamehe makosa yetu na uchawi ulio tulazimisha kuufanya. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mbora na Mwenye kudumu zaidi.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Hakika ataye mjia Mola wake Mlezi naye ni mkhalifu, basi kwa yakini, yake huyo ni Jahannamu. Hafi humo wala haishi.
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
Na atakaye mjia naye ni Muumini aliye tenda mema, basi hao ndio wenye vyeo vya juu.
ﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘﰙﰚﰛﰜﰝﰞ
Bustani za milele zipitazo mito kati yake, wadumu humo. Na hayo ni malipo ya mwenye kujitakasa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Na tulimfunulia Musa: Toka usiku na waja wangu, na uwapigie njia kavu baharini. Usikhofu kukamatwa, wala usiogope.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Firauni akawafuata pamoja na majeshi yake. Basi kiliwafudikiza humo baharini kilicho wafudikiza.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na Firauni aliwapoteza watu wake wala hakuwaongoa.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Enyi Wana wa Israili! Hakika tulikuokoeni na adui yenu, na tukakuahidini upande wa kulia wa mlima. Na tulikuteremshieni Manna na Salwa.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Kuleni katika vitu vizuri hivyo tulivyo kuruzukuni, wala msiruke mipaka katika hayo, isije ikakushukieni ghadhabu yangu. Na inaye mshukia ghadhabu yangu basi huyo ameangamia.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Na hakika Mimi ni Mwingi wa Kusamehe kwa anaye tubia, na akaamini, na akatenda mema, tena akaongoka.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Na nini kilicho kutia haraka ukawaacha watu wako, ewe Musa?
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Akasema: Hao wapo nyuma yangu wananifuatia. Na nimefanya haraka kukujia, Mola wangu Mlezi, ili uridhike.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Sisi tumewatia mtihani watu wako baada yako, na Msamaria amewapoteza.
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Musa akarudi kwa watu wake kwa ghadhabu na kusikitika. Akasema: Enyi watu wangu! Kwani Mola wenu Mlezi hakukuahidini ahadi nzuri? Je, umekuwa muda mrefu kwenu au mmetaka ikushukieni ghadhabu ya Mola wenu Mlezi, ndio maana mkavunja miadi yangu?
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
Wakasema: Sisi hatukuvunja miadi yako kwa khiari yetu, lakini tulibebeshwa mizigo ya mapambo ya watu, basi tukaitupa. Na hivyo ndivyo alivyo toa shauri Msamaria.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Na akawaundia ndama, kiwiliwili chenye sauti. Na wakasema: Huyu ndiye mungu wenu, na mungu wa Musa, lakini alisahau.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Je! Hawakuona kuwa hakuwarudishia neno, wala hakuweza kuwadhuru wala kuwafaa?
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Na hakika Harun alikwisha waambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihanini tu kwa kitu hiki. Na kwa yakini Mola wenu Mlezi ni Arrahmani, Mwingi wa Rehema. Basi nifuateni mimi, na t'iini amri yangu!
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Wakasema: Hatutaacha kumuabudu mpaka Musa atapo rejea kwetu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
(Musa) akasema: Ewe Harun! Ni nini kilicho kuzuia, ulipo waona wamepotea,
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Hata usinifuate? Je, umeasi amri yangu?
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
Akasema: Ewe mwana wa mama yangu! Usinishike ndevu zangu, wala kichwa changu. Kwa hakika naliogopa usije sema: Umewafarikisha Wana wa Israil, na hukungojea kauli yangu.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
(Musa) akasema: Ewe Msamaria! Unataka nini?
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Akasema: Niliona wasiyo yaona wao, nikashika gao katika unyao wa Mtume. Kisha nikalitupa. Na hivi ndivyo ilivyo nielekeza nafsi yangu.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
(Musa) akasema: Basi ondoka! Na kwa yakini utakuwa katika maisha ukisema: Usiniguse. Na hakika una ahadi kwako isiyo vunjwa. Na mtazame huyo mungu wako uliye endelea kumuabudu - Sisi kwa hakika tutamchoma moto, kisha tutamtawanya baharini atawanyike.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Hakika Mungu wenu ni Allah, Mwenyezi Mungu, tu. Hapana Mungu isipo kuwa Yeye. Ujuzi wake umeenea kila kitu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Namna hivi tunakuhadithia katika khabari za yaliyo tangulia. Na hakika tumekuletea kutoka kwetu mawaidha ya kukumbukwa.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Atakaye jitenga nayo, basi kwa yakini Siku ya Kiyama atabeba mzigo.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Wadumu humo. Na ni mzigo muovu kwao kuubeba Siku ya Kiyama!
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Siku litakapo pulizwa barugumu, na tukawakusanya wakhalifu Siku hiyo, hali macho yao ya kibuluu.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Watanong'onezana wao kwa wao: Hamkukaa ila siku kumi tu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Sisi tunajua zaidi watakayo yasema, atakapo sema mbora wao katika mwendo: Nyinyi hamkukaa ila siku moja tu.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Na wanakuuliza khabari za milima. Waambie: Mola wangu Mlezi ataivuruga vuruga.
ﮘﮙﮚﮛ
Na ataiacha tambarare, uwanda.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Hutaona humo mdidimio wala muinuko.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Siku hiyo watamfuata muitaji asiye na upotofu. Na sauti zote zitamnyenyekea Arrahmani Mwingi wa Rahema. Basi husikii ila mchakato na mnong'ono.
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Siku hiyo uombezi haufai kitu, ila wa aliye mruhusu Arrahmani Mwingi wa Rehema na akamridhia kusema.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Yeye anajua yaliyo mbele yao, na yaliyo nyuma yao. Wala wao hawawezi kumjua Yeye vilivyo.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Na zitadhalilika nyuso mbele ya Aliye Hai Milele, Mwangalizi Mkuu. Na atakuwa ameharibikiwa mwenye kubeba dhulma.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Na anaye tenda mema, naye ni Muumini, basi hatakhofu kudhulumiwa wala kupunjwa.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
Na namna hivi tumeiteremsha Qur'ani kwa Kiarabu, na tumekariri humo maonyo ili wapate kuogopa na kujilinda na iwaletee makumbusho.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki. Wala usiifanyie haraka hii Qur'ani, kabla haujamalizika ufunuo wake. Na sema: Mola wangu Mlezi! Nizidishie ilimu.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Na hapo zamani tuliagana na Adam, lakini alisahau, wala hatukuona kwake azma kubwa.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! Wakasujudu, isipo kuwa Iblisi, alikataa.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Tukasema: Ewe Adam! Hakika huyu ni adui yako na wa mkeo. Basi asikutoeni katika Bustani hii, mkaingia mashakani.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Hakika humo hutakuwa na njaa wala hutakuwa uchi.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Na hakika hutapata kiu humo wala hutapata joto.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Lakini Shet'ani alimtia wasiwasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujuulishe mti wa kuishi milele na ufalme usio koma?
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Basi wakaula wote wawili, na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Bustani. Na Adam akamuasi Mola wake Mlezi, na akapotea njia.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Kisha Mola wake Mlezi akamteuwa, naye akamkubalia toba yake, naye akamwongoa.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Akasema: Ondokeni humu nyote, hali ya kuwa ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Na ukikufikieni uwongofu kutoka kwangu basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
Aseme: Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona umenifufua kipofu, nami nilikuwa nikiona?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo vivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika leo unasahauliwa.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Na hivi ndivyo tutakavyo mlipa kila apitaye kiasi, na asiye amini ishara za Mola wake Mlezi. Na hakika adhabu ya Akhera ni kali zaidi, na inadumu zaidi.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Je! Haikuwabainikia tu; vizazi vingapi tuliviangamiza kabla yao, nao wanatembea katika maskani zao? Hakika katika hayo zimo ishara kwa wenye akili.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi na muda ulio wekwa, bila ya shaka inge fika adhabu (hapa hapa).
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Yavumilie haya wayasemayo. Na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu kabla ya kuchomoza jua, na kabla halijachwa, na nyakati za usiku pia umtakase, na ncha za mchana ili upate ya kukuridhisha.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Wala usivikodolee macho tulivyo wastareheshea baadhi ya watu miongoni mwao, kwa ajili ya mapambo ya duniani, ili tuwajaribu. Na riziki ya Mola wako Mlezi ni bora na inadumu zaidi.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo. Sisi hatukuombi wewe riziki, bali Sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema ni kwa mchamngu.
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Na walisema: Kwa nini hakutuletea muujiza kutoka kwa Mola wake Mlezi? Je! Haikuwafikilia dalili wazi ya yaliyomo katika Vitabu vya kale?
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃ
Na lau kuwa tuliwaangamiza kwa adhabu kabla yake, wangeli sema: Ewe Mola wetu Mlezi! Kwa nini usituletee Mtume tukazifuata ishara zako kabla hatujadhilika na kuhizika.
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
Sema: Kila mmoja anangoja. Basi ngojeni! Hivi karibuni mtajua nani mwenye njia sawa na nani aliye ongoka.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema