Sura Al-Anbiya
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Anbiya pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Anbiya pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Anbiya Tafsiri. Al-Anbiya (Makka) 112 Aya.
Related
- Al-Anbiya TafsiriKiswahili
- Al-Anbiya mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Anbiya

ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
IMEWAKARIBIA watu hisabu yao, nao wamo katika mghafala wanapuuza.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Hayawafikilii mawaidha mapya kutoka kwa Mola wao Mlezi ila huyasikiliza na huku wanafanya mchezo.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Zimeghafilika nyoyo zao. Na wale walio dhulumu hunong'onezana kwa siri: Ni nani ati huyu isipo kuwa ni binaadamu tu kama nyinyi! Mnauwendea uchawi hali nanyi mnaona?
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Alisema: Mola wangu Mlezi anayajua yasemwayo mbinguni na katika ardhi. Na Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Lakini wao walisema: Hizo ni ndoto za ovyo ovyo, bali amezizua tu, bali huyo ni mtunga mashairi. Basi atuletee miujiza kama walivyo tumwa wale wa mwanzo.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Hawakuamini kabla yao watu wa mji tulio uangamiza. Basi, je, wataamini hawa?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
Na kabla yako hatukuwatuma ila watu wanaume tulio wapa wahyi (ufunuo). Basi waulizeni wenye ilimu ikiwa nyinyi hamjui.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Wala hatukuwafanya miili isiyo kula chakula, wala hawakuwa wenye kuishi milele.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Kisha tukawatimizia miadi, na tukawaokoa wao na tulio wataka, na tukawateketeza walio pita mipaka.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Na hakika tumekuteremshieni Kitabu ambacho ndani yake yamo makumbusho yenu. Je! Hamzingatii?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Na mingapi katika miji iliyo kuwa ikidhulumu tumeiteketeza, na tukawasimamisha baada yao watu wengine.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Basi walipo ihisi adhabu yetu, mara wakaanza kukimbia.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
Msikimbie! Na rejeeni kwenye zile zile starehe zenu, na maskani zenu, mpate kusailiwa!
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tulikuwa madhaalimu.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Hakikuacha hicho kuwa kilio chao mpaka tukawafanya kama walio fyekwa, wamezimika.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yao kwa mchezo.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Kama tungeli taka kufanya mchezo tunge jifanyia Sisi wenyewe, lau kwamba tungeli kuwa ni wafanyao mchezo.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Bali tunaitupa kweli juu ya uwongo ikauvunja na mara ukatoweka. Na ole wenu kwa mnayo yazua.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Na ni vyake Yeye tu Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na katika ardhi. Na walioko kwake hawafanyi kiburi wakaacha kumuabudu, wala hawachoki.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Wanamtakasa usiku na mchana, wala hawanyong'onyei.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Au wamepata miungu katika ardhi inayo fufua?
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Lau wangeli kuwamo humo miungu wengine isipo kuwa Mwenyezi Mungu basi bila ya shaka hizo mbingu na ardhi zingeli fisidika. Subahana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu, Bwana wa A'rshi (Kiti cha Enzi), na hayo wanayo yazua.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Yeye hahojiwi kwa ayatendayo, na wao ndio wanao hojiwa kwa wayatendayo.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏ
Au wanawaabudu miungu mingine badala yake? Sema: Leteni ushahidi wenu! Haya ni ukumbusho wa hawa walio nami, na ukumbusho wa walio kabla yangu. Lakini wengi wao hawaijui kweli, na kwa hivyo wanapuuza.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipo kuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi tu.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
Na wanasema: Arrahman, Mwingi wa Rehema, ana mwana! Subhanahu, Ametakasika na hayo! Bali hao (wanao waita wana) ni watumwa walio tukuzwa.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Hawamtangulii kwa neno, nao wanafanya amri zake.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Wala hawamwombei yeyote ila yule anaye mridhia Yeye, nao kwa ajili ya kumwogopa wananyenyekea.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Na yeyote kati yao atakaye sema: Mimi ni mungu, badala yake, basi huyo tutamlipa malipo yake Jahannamu. Hivyo ndivyo tuwalipavyo wenye kudhulumu.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabandua? Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini?
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Na tukaweka katika ardhi milima iliyo thibiti ili isiwayumbishe, na tukaweka humo njia pana ili wapate kuongoka.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa, lakini wanazipuuza Ishara zake.
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga vinaogelea.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Nasi hatukumjaalia mwanaadamu yeyote kabla yako kuwa na maisha ya milele. Basi je! Ukifa wewe, wao wataishi milele?
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Kila nafsi itaonja mauti; na tunakujaribuni kwa mtihani wa shari na kheri. Na kwetu Sisi mtarejeshwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Na wakikuona walio kufuru hawakufanyi wewe ila ni kitu cha maskhara tu, (wakisema): Je! Ndiye huyu anaye itaja miungu yenu? Na hali wao wanakataa kumkumbuka Arrahman, Mwingi wa Rehema!
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Mwanaadamu ameumbwa na haraka. Nitakuonyesheni Ishara zangu. Basi msinihimize.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Lau wangeli jua wale walio kufuru wakati ambao hawatauzuia Moto kwenye nyuso zao wala migongo yao, na wala hawatanusuriwa!
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Bali utawafikia kwa ghafla, na utawashitua na wala hawataweza kuurudisha, wala hawatapewa muhula!
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Na Mitume walio kabla yako walikwisha dhihakiwa. Kwa hivyo wale walio wafanyia maskhara yaliwafika yale waliyo kuwa wakiyafanyia dhihaka.
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Sema: Nani anaye kulindeni usiku na mchana na Arrahmani Mwingi wa Rehema? Bali wao wanapuuza kumkumbuka Mola wao Mlezi.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Au wao wanao miungu watao weza kuwakinga nasi? Hao hawawezi kujinusuru nafsi zao, wala hawatalindwa nasi!
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka umri ukawa mrefu kwao. Je, hawaoni ya kwamba Sisi tunaifikia ardhi tukiipunguza ncha zake? Basi je! Hao ni wenye kushinda?
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Sema: Mimi nakuonyeni kwa Wahyi. Na viziwi hawasikii wito wanapo onywa.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Na wanapo guswa na mpulizo mmoja tu wa adhabu itokayo kwa Mola wako Mlezi, bila ya shaka wao husema: Ole wetu! Hakika tulikuwa wenye kudhulumu.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Nasi tutaweka mizani za uadilifu kwa Siku ya Kiyama. Basi nafsi haitadhulumiwa kitu chochote. Hata ikiwa ni uzito wa chembe ya khardali tutaileta. Nasi tunatosha kuwa washika hisabu.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na kwa yakini tuliwapa Musa na Haaruni kipambanuzi, na mwangaza, na makumbusho kwa wachamngu,
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Ambao wanamkhofu Mola wao Mlezi faraghani, na wanaiogopa Saa ya Kiyama.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Na haya ni makumbusho yaliyo barikiwa, tuliyo yateremsha. Basi je! Mnayakataa?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Na hakika tulikwisha mpa Ibrahim uwongofu wake zamani, na tulikuwa tunamjua.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Alipo mwambia baba yake na watu wake: Ni nini haya masanamu mnayo yashughulikia kuyaabudu?
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Wakasema: Tumewakuta baba zetu wakiyaabudu.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Akasema: Bila ya shaka nyinyi na baba zenu mmekuwa katika upotofu ulio dhaahiri.
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Wakasema: Je! Umetujia kwa maneno ya kweli au wewe ni katika wachezao tu?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Akasema: Bali Mola wenu Mlezi ni Mola Mlezi wa mbingu na ardhi ambaye ndiye aliye ziumba. Na mimi ni katika wenye kuyashuhudia hayo.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Na Wallahi! Nitayafanyia vitimbi masanamu yenu haya baada ya mkisha geuka kwenda zenu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Basi akayavunja vipande vipande, ila kubwa lao, ili wao walirudie.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Wakasema: Nani aliye ifanyia haya miungu yetu? Hakika huyu ni katika walio dhulumu.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Wakasema: Tumemsikia kijana mmoja akiwataja. Anaitwa Ibrahim.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Wakasema: Mleteni mbele ya macho ya watu, wapate kumshuhudia!
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Wakasema: Je! Wewe umeifanyia haya miungu yetu, ewe Ibrahim?
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Akasema: Bali amefanya hayo huyu mkubwa wao. Basi waulizeni ikiwa wanaweza kutamka.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Basi wakajirudi nafsi zao, wakasema: Hakika nyinyi mlikuwa madhaalimu!
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Kisha wakarejea kwenye ule ule upotovu wao wakasema: Wewe unajua kwamba hawa hawesemi.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Akasema: Basi nyinyi mnawaabudu asiye kuwa Mwenyezi Mungu wasio kufaini kitu wala kukudhuruni?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Aibu yenu nyinyi na hivyo mnavyo viabudu badala ya Mwenyezi Mungu! Basi nyinyi hamtii akilini?
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Wakasema: Mchomeni moto, na muinusuru miungu yenu, ikiwa nyinyi ni watendao jambo!
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Sisi tukasema: Ewe moto! Kuwa baridi na salama kwa Ibrahim!
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Wao walimkusudia maovu, lakini Sisi tukawafanya wao ndio walio khasiri.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Na tukamwokoa yeye na Luut'i tukawapeleka kwenye nchi tulio ibariki kwa ajili ya walimwengu wote.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Naye tukampa Is-haq, na Yaaqub kuwa ni ziada. Na wote tukawajaalia wawe watu wema.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Na tukawafanya maimamu wakiongoa watu kwa amri yetu. Na tukawafunulia watende kheri, na washike Sala, na watoe Zaka; na walikuwa wanatuabudu Sisi tu.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Na Luut'i tukampa hukumu na ilimu na tukamwokoa na ule mji ulio kuwa ukifanya maovu. Hakika hao walikuwa watu wabaya, wachafu.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na tukamuingiza katika rehema yetu. Hakika yeye ni miongoni mwa watenda mema.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Na Nuhu alipo ita zamani, nasi tukamuitikia, na tukamwokoa yeye na watu wake kutokana na shida kubwa.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Na tukamnusuru na watu walio zikanusha Ishara zetu. Hakika hao walikuwa watu wabaya. Basi tukawazamisha wote.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Na Daud na Suleiman walipo kata hukumu katika kadhiya ya konde walipo lisha humo mbuzi wa watu usiku. Na Sisi tulikuwa wenye kushuhudia hukumu yao hiyo.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
Tukamfahamisha Suleiman. Na kila mmoja wao tulimpa hukumu na ilimu. Na tuliifanya milima na ndege kuwa pamoja na Daud imnyenyekee na imtakase Mwenyezi Mungu. Na Sisi ndio tulio fanya hayo.
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Na tukamfundisha kuunda mavazi ya vita kwa ajili yenu ili yakuhifadhini katika kupigana kwenu. Je! Mtakuwa wenye kushukuru?
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Na tukamsahilishia Suleiman upepo wa kimbunga wendao kwa amri yake kwenye ardhi tuliyo ibarikia. Na Sisi ndio tunao jua kila kitu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Na pia mashet'ani wanao mpigia mbizi na kufanya kazi nyenginezo. Na Sisi tulikuwa walinzi wao.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Na Ayyubu, alipo mwita Mola wake Mlezi, akasema: Mimi yamenipata madhara. Na Wewe ndiye unaye rehemu kuliko wote wanao rehemu.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Basi tukamwitikia, na tukamwondolea madhara aliyo kuwa nayo, na tukampa watu wake na mfano wao pamoja nao kuwa ni rehema inayo toka kwetu, na ukumbusho kwa wafanyao ibada.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Na Ismail, na Idris, na Dhulkifli - wote walikuwa miongoni mwa wanao subiri.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Na tukawaingiza katika rehema yetu. Hakika wao walikuwa katika watu wema.
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhibika, na akadhani ya kwamba hatutakuwa na uwezo juu yake. Basi aliita katika giza: Hapana mungu isipo kuwa Wewe Subhanaka Uliye takasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Basi tukamwitikia na tukamwokoa kutokana na dhiki. Na hivyo ndivyo tunavyo waokoa Waumini.
ﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Na Zakariya alipo mwita Mola wake Mlezi: Mola wangu Mlezi! Usiniache peke yangu, na Wewe ndiye Mbora wa wanao rithi.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Basi tukamwitikia, na tukampa Yahya na tukamponyeshea mkewe. Hakika wao walikuwa wepesi wa kutenda mema, na wakituomba kwa shauku na khofu. Nao walikuwa wakitunyenyekea.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
Na mwanamke aliye linda uke wake, na tukampulizia katika roho yetu, na tukamfanya yeye na mwanawe kuwa ni Ishara kwa walimwengu.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Kwa hakika huu umma wenu ni umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi. Kwa hivyo niabuduni Mimi.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Nao wakalikata jambo lao hili mapande mapande baina yao. Wote watarudi kwetu.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Na atendaye mema naye ni Muumini basi haitakataliwa juhudi yake. Na hakika Sisi tunamwandikia.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Na haiwi kwa wana-mji tulio uangamiza, ya kwamba hawatarejea,
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Mpaka watapo funguliwa Juju na Maajuju wakawa wanateremka kutoka kila mlima;
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Na miadi ya haki ikakaribia. Hapo ndipo yatapo kodoka macho ya walio kufuru (na watasema:) Ole wetu! Bila ya shaka tulikuwa tumeghafilika na haya, bali tulikuwa wenye kudhulumu.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Hakika nyinyi na hao mnao waabudu badala ya Mwenyezi Mungu ni kuni za Jahannamu; huko mtaingia tu.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Lau kuwa hawa ni miungu, wasingeli ingia. Na wote watadumu humo.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Lao wao humo ni kupiga mayowe, na wala hawatasikia (jenginelo).
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Ama wale ambao wema wetu umewatangulia, hao watatenganishwa na hayo.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Hawatausikia mvumo wake, na wao watadumu katika yale zinayo yatamani nafsi zao.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
Hicho Kitisho Kikubwa hakito wahuzunisha. Na Malaika watawapokea (kwa kuwaambia): Hii ndiyo Siku yenu mliyo kuwa mkiahidiwa!
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Siku tutakapo zikunja mbingu kama mkunjo wa karatasi za vitabu. Kama tulivyo anza umbo la mwanzo tutalirudisha tena. Ni ahadi iliyo juu yetu. Hakika Sisi ni watendao.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Na hakika tulikwisha andika katika Zaburi baada ya Kumbukumbu, ya kwamba nchi watairithi waja wangu walio wema.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Hakika katika haya yapo mawaidha kwa watu wafanyao ibada.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Nasi hatukukutuma ila uwe ni Rehema kwa walimwengu wote.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Sema: Hakika imefunuliwa kwangu ya kwamba hakika Mungu wenu ni Mungu Mmoja tu. Je! Mmesilimu?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Na kama wakigeuka, basi sema: Nimekutangazieni sawa sawa, wala sijui yako karibu au mbali hayo mliyo ahidiwa.
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Hakika Yeye anajua kauli ya dhaahiri na anajua myafichayo.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Wala sijui pengine huu ni mtihani tu kwenu na starehe mpaka muda kidogo.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Sema: Mola wangu Mlezi! Hukumu kwa haki. Na Mola wetu Mlezi ni Mwingi wa Rehema, aombwaye msaada juu ya mnayo yazua.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







