An-Nur · 32/64
Tafsiri Uandishi wa sauti — Sura An-Nur
وَأَنكِحُوا الْأَيَامَىٰ مِنكُمْ وَالصَّالِحِينَ مِنْ عِبَادِكُمْ وَإِمَائِكُمْ ۚ إِن يَكُونُوا فُقَرَاءَ يُغْنِهِمُ اللَّهُ مِن فَضْلِهِ ۗ وَاللَّهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ ۝٣٢
Wa ankihul ayaamaa minkum was saaliheena min `ibaadikum wa imaa`kum; iny-yakoonoo fuqaraaa`a yughni himul laahu min fadlih; wal laahu Waasi`un `Aleem
📖 Kwa Kiswahili
Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na wajakazi wenu. Wakiwa mafakiri Mwenyezi Mungu atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mwenye kujua.

🎧 Sikiliza
📜

Tafsiri — Tafsir

Maana za maneno:

  • Al-Ayamaa (الأَيَامَى): Watu ambao hawana wenzi wa ndoa, iwe wanaume au wanawake, iwe hawajaoa kabisa (waseja) au walioachwa/waliofiwa.
  • As-Saalihiin (الصَّالِحِينَ): Watu wema, wenye Imani na wachamungu.
  • Imaa' (إِمَائِكُمْ): Watumwa wanawake.
  • Waasi'un (وَاسِعٌ): Mwenye kumpa kila mtu riziki nyingi, ambaye hazina yake haiongezeki wala haipungui kwa kutoa.
  • Aliim (عَلِيمٌ): Mwenye kujua hali za waja wake wote, anajua nani anayestahili kupewa na nani asiyestahili.

Ufafanuzi wa Aya:

Enyi Waumini! Ozesheni wale ambao hawana wenzi wa ndoa miongoni mwenu, iwe wanaume au wanawake, waseja au walioachwa/waliofiwa. Pia ozeni waja wenu wema wa kiume na wa kike (watumwa na wajakazi) ambao wana Imani na wema. Muisilamu asikawie kuwaozesha watu hawa kwa sababu ya hofu ya umaskini au ukosefu wa mali. Kwa hakika, Mwenyezi Mungu Atawapa riziki kwa fadhila zake kubwa, na Atawawezesha kupata mahitaji yao kwa njia zisizotarajiwa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kumpa kila mtu riziki nyingi, haipunguki kitu kwa kuwapa waja wake, naye ni Mwenye kujua hali zao zote, Anajua nani anayestahili kupewa riziki nyingi na nani anayestahili kupewa kiasi, kwa hekima yake.


Faida na Mafunzo kutoka kwenye Aya hii:

  1. Kuhimizwa kwa ndoa na kuwasaidia wasio na wenzi: Aya hii inatuhimiza kuwasaidia vijana na watu wote wasio na wenzi kupata wenzi wao, kwa sababu ndoa ni njia ya kujikinga na dhambi na ni ibada inayompendeza Mwenyezi Mungu.
  2. Kutokuwa na wasiwasi kuhusu riziki: Muislamu asikawie kuoa au kuozesha kwa sababu ya umaskini, kwani Mwenyezi Mungu ameahidi kuwapa riziki wenye ndoa. Hili linatia moyo na kuondoa hofu ya umaskini.
  3. Usawa kati ya watu: Aya inasisitiza kwamba waja na wajakazi (watumwa) pia wanastahili kuozeshwa, ikionyesha kwamba kila mtu ana haki ya kuishi maisha ya heshima na kujenga familia, bila kujali hadhi yake ya kijamii.
  4. Kutegemea Mwenyezi Mungu: Aya inafundisha kwamba riziki iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu, na Yeye ndiye Mwenye kumpa kila mtu kwa kadiri ya hekima yake. Hivyo, Muislamu anapaswa kumtegemea Mwenyezi Mungu na kuamini ahadi zake.
  5. Kujenga jamii yenye Imani: Kuozesha watu wema na wachamungu kunasaidia kujenga jamii yenye maadili mema na Imani thabiti, kwani ndoa yenye misingi ya Imani huleta amani na baraka kwenye familia na jamii kwa ujumla.


📜 Aya 30-34 — Sura An-Nur

30قُل لِّلْمُؤْمِنِينَ يَغُضُّوا مِنْ أَبْصَارِهِمْ وَيَحْفَظُوا فُرُوجَهُمْ ۚ ذَٰلِكَ أَزْكَىٰ لَهُمْ ۗ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا يَصْنَعُونَ
Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao. Hili ni takaso bora kwao. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za wanayo yafanya.
31وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ ۖ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ ۚ وَتُوبُوا إِلَى اللَّهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ
Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, au wafwasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yaliyo khusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajuulikane mapambo waliyo yaficha. Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa.
32وَأَنكِحُوا الْأَيَامَىٰ مِنكُمْ وَالصَّالِحِينَ مِنْ عِبَادِكُمْ وَإِمَائِكُمْ ۚ إِن يَكُونُوا فُقَرَاءَ يُغْنِهِمُ اللَّهُ مِن فَضْلِهِ ۗ وَاللَّهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ
Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na wajakazi wenu. Wakiwa mafakiri Mwenyezi Mungu atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mwenye kujua.
33وَلْيَسْتَعْفِفِ الَّذِينَ لَا يَجِدُونَ نِكَاحًا حَتَّىٰ يُغْنِيَهُمُ اللَّهُ مِن فَضْلِهِ ۗ وَالَّذِينَ يَبْتَغُونَ الْكِتَابَ مِمَّا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ فَكَاتِبُوهُمْ إِنْ عَلِمْتُمْ فِيهِمْ خَيْرًا ۖ وَآتُوهُم مِّن مَّالِ اللَّهِ الَّذِي آتَاكُمْ ۚ وَلَا تُكْرِهُوا فَتَيَاتِكُمْ عَلَى الْبِغَاءِ إِنْ أَرَدْنَ تَحَصُّنًا لِّتَبْتَغُوا عَرَضَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۚ وَمَن يُكْرِههُّنَّ فَإِنَّ اللَّهَ مِن بَعْدِ إِكْرَاهِهِنَّ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Na wajizuilie na machafu wale wasio pata cha kuolea, mpaka Mwenyezi Mungu awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Mwenyezi Mungu aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi vyenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la maisha ya dunia, ilhali wao wanataka kujihishimu. Na atakaye walazimisha basi Mwenyezi Mungu baada ya kulazimishwa kwao huko, atawasamehe, kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.
34وَلَقَدْ أَنزَلْنَا إِلَيْكُمْ آيَاتٍ مُّبَيِّنَاتٍ وَمَثَلًا مِّنَ الَّذِينَ خَلَوْا مِن قَبْلِكُمْ وَمَوْعِظَةً لِّلْمُتَّقِينَ
Na kwa yakini tumekuteremshieni Ishara zilizo wazi na mifano kutokana na walio tangulia kabla yenu na mawaidha kwa wachamngu.
An-NurFaharasa ya Qurani
64Aya
MadinaRevelation
32Aya

Tafsiri — An-Nur 32

Sura An-Nur Aya 32 - Soma, Sikiliza, Tafsiri, Kiswahili : Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu…

Sura Aya 32/64 — Sura An-Nur النور (Madina). Soma Sikiliza Tafsiri (Kiswahili). Sikiliza: Sura An-Nur Sikiliza, Sura An-Nur Tafsiri, Sura An-Nur mp3, Sura An-Nur pdf. Aya 30–34. Kwa Kiswahili: Soomaali.




Kurani Tukufu


Monday, September 7, 2026

Usitusahau katika dua zako njema