Sura Adh-Dhariyat
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Adh-Dhariyat pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Adh-Dhariyat pdf Kiswahili — Pakua Sura Adh-Dhariyat Tafsiri. Adh-Dhariyat (Makka) 60 Aya.
Related
- Adh-Dhariyat TafsiriKiswahili
- Adh-Dhariyat mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Adh-Dhariyat

ﯤﯥﯦ
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
ﯧﯨﯩ
Na zinazo beba mizigo,
ﯪﯫﯬ
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
ﯭﯮﯯ
Na zinazo gawanya kwa amri,
ﯰﯱﯲﯳ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
ﯴﯵﯶﯷ
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
ﭑﭒﭓﭔ
Naapa kwa mbingu zenye njia,
ﭕﭖﭗﭘﭙ
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
ﭚﭛﭜﭝﭞ
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
ﭟﭠﭡ
Wazushi wameangamizwa.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
Ambao wameghafilika katika ujinga.
ﭨﭩﭪﭫﭬ
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
ﮓﮔﮕﮖ
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱ
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃ
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Tuwatupie mawe ya udongo,
ﭥﭦﭧﭨﭩ
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
ﯶﯷﯸﯹﯺ
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
ﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘﰙ
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







