Sura Az-Zukhruf pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Az-Zukhruf pdf Kiswahili — Pakua Sura Az-Zukhruf Tafsiri. Sura Az-Zukhruf (Makka) 89 Aya.
Related
- Sura Az-Zukhruf TafsiriKiswahili
- Sura Az-Zukhruf mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Az-Zukhruf

ﮀﮁ
43:1
H'a Mim
ﮂﮃﮄ
43:2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
43:3
Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
43:4
Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
43:5
Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri?
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
43:6
Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
43:7
Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
43:8
Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
43:9
Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
43:10
Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
43:11
Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
43:12
Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
43:13
Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
43:14
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
43:15
Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
43:16
Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
43:17
Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
43:18
Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
43:19
Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
43:20
Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
43:21
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
43:22
Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
43:23
Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
43:24
Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
43:25
Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha!
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
43:26
Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu,
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
43:27
Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
43:28
Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
43:29
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
43:30
Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
43:31
Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
43:32
Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
43:33
Na lau isinge kuwa watu watakuwa kundi moja tungeli wajaalia wanao mkufuru Rahmani wana nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazo pandia,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
43:34
Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake,
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
43:35
Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
43:36
Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
43:37
Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
43:38
Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe!
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
43:39
Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
43:40
Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
43:41
Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
43:42
Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
43:43
Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
43:44
Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
43:45
Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
43:46
Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
43:47
Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
43:48
Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
43:49
Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
43:50
Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
43:51
Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni?
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
43:52
Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
43:53
Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
43:54
Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
43:55
Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
ﮯﮰﮱﯓﯔ
43:56
Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
43:57
Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
43:58
Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
43:59
Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
43:60
Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
43:61
Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
43:62
Wala asikuzuilieni Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
43:63
Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
43:64
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
43:65
Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
43:66
Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
43:67
Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
43:68
Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
43:69
Ambao waliziamini Ishara zangu na walikuwa Waislamu.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
43:70
Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
43:71
Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
43:72
Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
43:73
Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
43:74
Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
43:75
Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
43:76
Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhaalimu.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
43:77
Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
43:78
Kwa yakini tulikuleteeni Haki, lakini wengi katika nyinyi mlikuwa mnaichukia Haki.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
43:79
Au waliweza kupitisha amri yao? Bali ni Sisi ndio tunao pitisha.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
43:80
Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
43:81
Sema: Ingeli kuwa Rahmani ana mwana, basi mimi ningeli kuwa wa kwanza kumuabudu.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
43:82
Ametakasika Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa A'rshi, na hayo wanayo msifia.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
43:83
Basi waache wapige porojo wakicheza mpaka wakutwe na hiyo siku yao waliyo ahidiwa.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
43:84
Na Yeye ndiye Mungu mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
43:85
Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
43:86
Wala hao mnao waomba badala yake Yeye hawana uweza wa kumwombea mtu, isipo kuwa anaye shuhudia kwa haki, na wao wanajua.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
43:87
Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu! Basi ni wapi wanako geuziwa?
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
43:88
Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
43:89
Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







