Sura Az-Zukhruf
PDF —
89 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Az-Zukhruf pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Az-Zukhruf pdf Kiswahili — Pakua Sura Az-Zukhruf Tafsiri. Az-Zukhruf (Makka) 89 Aya.



Sura Az-Zukhruf
89 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮀﮁ
H'a Mim
ﮂﮃﮄ
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri?
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha!
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu,
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
Na lau isinge kuwa watu watakuwa kundi moja tungeli wajaalia wanao mkufuru Rahmani wana nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazo pandia,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake,
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe!
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao.
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka.
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni?
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
ﮯﮰﮱﯓﯔ
Kisha tukawafanya kuwa watangulizi na mfano kwa wa baadaye.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Wala asikuzuilieni Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Ambao waliziamini Ishara zangu na walikuwa Waislamu.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhaalimu.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Kwa yakini tulikuleteeni Haki, lakini wengi katika nyinyi mlikuwa mnaichukia Haki.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Au waliweza kupitisha amri yao? Bali ni Sisi ndio tunao pitisha.
ﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Sema: Ingeli kuwa Rahmani ana mwana, basi mimi ningeli kuwa wa kwanza kumuabudu.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Ametakasika Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa A'rshi, na hayo wanayo msifia.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Basi waache wapige porojo wakicheza mpaka wakutwe na hiyo siku yao waliyo ahidiwa.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Na Yeye ndiye Mungu mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Wala hao mnao waomba badala yake Yeye hawana uweza wa kumwombea mtu, isipo kuwa anaye shuhudia kwa haki, na wao wanajua.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹ
Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu! Basi ni wapi wanako geuziwa?
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema