PDF —
49 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura At-Tur pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura At-Tur pdf Kiswahili — Pakua Sura At-Tur Tafsiri. Sura At-Tur (Makka) 49 Aya.



49 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮞﮟ
52:1 Naapa kwa mlima wa T'ur,
ﮠﮡﮢ
52:2 Na Kitabu kilicho andikwa
ﮣﮤﮥﮦ
52:3 Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
ﮧﮨﮩ
52:4 Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
ﮪﮫﮬ
52:5 Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
ﮭﮮﮯ
52:6 Na kwa bahari iliyo jazwa,
ﮰﮱﯓﯔﯕ
52:7 Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
ﯖﯗﯘﯙﯚ
52:8 Hapana wa kuizuia.
ﯛﯜﯝﯞﯟ
52:9 Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
ﯠﯡﯢﯣ
52:10 Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
ﯤﯥﯦﯧ
52:11 Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
52:12 Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
52:13 Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
52:14 (Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
52:15 Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
52:16 Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
52:17 Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
52:18 Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
52:19 Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
52:20 Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
52:21 Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
52:22 Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
52:23 Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
52:24 Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
52:25 Wataelekeana wakiulizana.
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
52:26 Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
52:27 Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
52:28 Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
52:29 Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃ
52:30 Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
52:31 Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
52:32 Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
52:33 Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
52:34 Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
52:35 Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
52:36 Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
52:37 Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
52:38 Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
52:39 Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
52:40 Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
52:41 Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
52:42 Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
52:43 Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
52:44 Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
52:45 Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
52:46 Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
52:47 Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
52:48 Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
52:49 Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema