Sura At-Tur pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura At-Tur pdf Kiswahili — Pakua Sura At-Tur Tafsiri. Sura At-Tur (Makka) 49 Aya.
Related
- Sura At-Tur TafsiriKiswahili
- Sura At-Tur mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura At-Tur

ﮞﮟ
52:1
Naapa kwa mlima wa T'ur,
ﮠﮡﮢ
52:2
Na Kitabu kilicho andikwa
ﮣﮤﮥﮦ
52:3
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
ﮧﮨﮩ
52:4
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
ﮪﮫﮬ
52:5
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
ﮭﮮﮯ
52:6
Na kwa bahari iliyo jazwa,
ﮰﮱﯓﯔﯕ
52:7
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
ﯖﯗﯘﯙﯚ
52:8
Hapana wa kuizuia.
ﯛﯜﯝﯞﯟ
52:9
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
ﯠﯡﯢﯣ
52:10
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
ﯤﯥﯦﯧ
52:11
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
52:12
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
52:13
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
52:14
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
52:15
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
52:16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
52:17
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
ﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
52:18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
52:19
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
52:20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
52:21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
52:22
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
52:23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
52:24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘ
52:25
Wataelekeana wakiulizana.
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
52:26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
52:27
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
52:28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
52:29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃ
52:30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
52:31
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
52:32
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
52:33
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
52:34
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
52:35
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
52:36
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃ
52:37
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
52:38
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
52:39
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
52:40
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
52:41
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
52:42
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
52:43
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
52:44
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
52:45
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
52:46
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
52:47
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
52:48
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
52:49
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







