Sura Al-Qamar pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Qamar pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qamar Tafsiri. Sura Al-Qamar (Makka) 55 Aya.
Related
- Sura Al-Qamar TafsiriKiswahili
- Sura Al-Qamar mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Qamar

ﮬﮭﮮﮯﮰ
54:1
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
54:2
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
54:3
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
54:4
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
54:5
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
54:6
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
54:7
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
54:8
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
54:9
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
54:10
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
54:11
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
54:12
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
54:13
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
54:14
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
54:15
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
ﮙﮚﮛﮜﮝ
54:16
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
54:17
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
54:18
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
54:19
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
54:20
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
54:21
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
54:22
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
ﯬﯭﯮﯯ
54:23
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
54:24
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
54:25
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
54:26
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
54:27
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
54:28
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
ﭛﭜﭝﭞﭟ
54:29
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
ﭠﭡﭢﭣﭤ
54:30
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
54:31
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
54:32
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
ﭶﭷﭸﭹﭺ
54:33
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
54:34
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
54:35
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
54:36
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
54:37
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
54:38
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
ﮥﮦﮧﮨ
54:39
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
54:40
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
54:41
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
54:42
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯦﯧﯨﯩﯪ
54:43
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
54:44
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
ﯱﯲﯳﯴﯵ
54:45
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
54:46
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
54:47
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
54:48
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
ﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
54:49
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
54:50
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
54:51
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
54:52
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
54:53
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
54:54
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
54:55
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







