Sura Al-Qamar
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Qamar pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Qamar pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qamar Tafsiri. Al-Qamar (Makka) 55 Aya.
Related
- Al-Qamar TafsiriKiswahili
- Al-Qamar mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Qamar

ﮬﮭﮮﮯﮰ
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
ﮙﮚﮛﮜﮝ
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
ﯬﯭﯮﯯ
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
ﭛﭜﭝﭞﭟ
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
ﭠﭡﭢﭣﭤ
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
ﭶﭷﭸﭹﭺ
Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
ﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
ﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
ﮥﮦﮧﮨ
Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯦﯧﯨﯩﯪ
Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
ﯱﯲﯳﯴﯵ
Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
ﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
ﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞ
Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
ﭥﭦﭧﭨﭩ
Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







