Sura An-Najm kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura An-Najm na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (62 Aya — مكية). An-Najm Sikiliza, An-Najm Tafsiri, An-Najm mp3, An-Najm pdf.

Soma na Sikiliza Sura An-Najm

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
وَالنَّجْمِ إِذَا هَوَىٰ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Naapa kwa nyota inapo tua,
مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمْ وَمَا غَوَىٰ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Wala hatamki kwa matamanio.
إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
عَلَّمَهُ شَدِيدُ الْقُوَىٰ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
ذُو مِرَّةٍ فَاسْتَوَىٰ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Mwenye kutua, akatulia,
وَهُوَ بِالْأُفُقِ الْأَعْلَىٰ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Kisha akakaribia na akateremka.
فَكَانَ قَابَ قَوْسَيْنِ أَوْ أَدْنَىٰ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
فَأَوْحَىٰ إِلَىٰ عَبْدِهِ مَا أَوْحَىٰ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
مَا كَذَبَ الْفُؤَادُ مَا رَأَىٰ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
أَفَتُمَارُونَهُ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
وَلَقَدْ رَآهُ نَزْلَةً أُخْرَىٰ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Na akamwona mara nyingine,
عِندَ سِدْرَةِ الْمُنتَهَىٰ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Penye Mkunazi wa mwisho.
عِندَهَا جَنَّةُ الْمَأْوَىٰ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
إِذْ يَغْشَى السِّدْرَةَ مَا يَغْشَىٰ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
مَا زَاغَ الْبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
لَقَدْ رَأَىٰ مِنْ آيَاتِ رَبِّهِ الْكُبْرَىٰ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
أَفَرَأَيْتُمُ اللَّاتَ وَالْعُزَّىٰ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Je! Mmemuona Lata na Uzza?
وَمَنَاةَ الثَّالِثَةَ الْأُخْرَىٰ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Na Manaat, mwingine wa tatu?
أَلَكُمُ الذَّكَرُ وَلَهُ الْأُنثَىٰ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
تِلْكَ إِذًا قِسْمَةٌ ضِيزَىٰ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Huo ni mgawanyo wa dhulma!
إِنْ هِيَ إِلَّا أَسْمَاءٌ سَمَّيْتُمُوهَا أَنتُمْ وَآبَاؤُكُم مَّا أَنزَلَ اللَّهُ بِهَا مِن سُلْطَانٍ ۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا الظَّنَّ وَمَا تَهْوَى الْأَنفُسُ ۖ وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ الْهُدَىٰ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
أَمْ لِلْإِنسَانِ مَا تَمَنَّىٰ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
فَلِلَّهِ الْآخِرَةُ وَالْأُولَىٰ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
۞ وَكَم مِّن مَّلَكٍ فِي السَّمَاوَاتِ لَا تُغْنِي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا إِلَّا مِن بَعْدِ أَن يَأْذَنَ اللَّهُ لِمَن يَشَاءُ وَيَرْضَىٰ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
إِنَّ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ لَيُسَمُّونَ الْمَلَائِكَةَ تَسْمِيَةَ الْأُنثَىٰ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
وَمَا لَهُم بِهِ مِنْ عِلْمٍ ۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا الظَّنَّ ۖ وَإِنَّ الظَّنَّ لَا يُغْنِي مِنَ الْحَقِّ شَيْئًا ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
فَأَعْرِضْ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكْرِنَا وَلَمْ يُرِدْ إِلَّا الْحَيَاةَ الدُّنْيَا ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
ذَٰلِكَ مَبْلَغُهُم مِّنَ الْعِلْمِ ۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اهْتَدَىٰ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
وَلِلَّهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ لِيَجْزِيَ الَّذِينَ أَسَاءُوا بِمَا عَمِلُوا وَيَجْزِيَ الَّذِينَ أَحْسَنُوا بِالْحُسْنَى ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.
الَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَائِرَ الْإِثْمِ وَالْفَوَاحِشَ إِلَّا اللَّمَمَ ۚ إِنَّ رَبَّكَ وَاسِعُ الْمَغْفِرَةِ ۚ هُوَ أَعْلَمُ بِكُمْ إِذْ أَنشَأَكُم مِّنَ الْأَرْضِ وَإِذْ أَنتُمْ أَجِنَّةٌ فِي بُطُونِ أُمَّهَاتِكُمْ ۖ فَلَا تُزَكُّوا أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اتَّقَىٰ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.
أَفَرَأَيْتَ الَّذِي تَوَلَّىٰ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Je! Umemwona yule aliye geuka?
وَأَعْطَىٰ قَلِيلًا وَأَكْدَىٰ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?
أَعِندَهُ عِلْمُ الْغَيْبِ فَهُوَ يَرَىٰ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?
أَمْ لَمْ يُنَبَّأْ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
وَإِبْرَاهِيمَ الَّذِي وَفَّىٰ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?
أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَانِ إِلَّا مَا سَعَىٰ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?
وَأَنَّ سَعْيَهُ سَوْفَ يُرَىٰ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
ثُمَّ يُجْزَاهُ الْجَزَاءَ الْأَوْفَىٰ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.
وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ الْمُنتَهَىٰ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.
وَأَنَّهُ هُوَ أَضْحَكَ وَأَبْكَىٰ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.
وَأَنَّهُ هُوَ أَمَاتَ وَأَحْيَا ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.
وَأَنَّهُ خَلَقَ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
مِن نُّطْفَةٍ إِذَا تُمْنَىٰ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
وَأَنَّ عَلَيْهِ النَّشْأَةَ الْأُخْرَىٰ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
وَأَنَّهُ هُوَ أَغْنَىٰ وَأَقْنَىٰ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
وَأَنَّهُ هُوَ رَبُّ الشِّعْرَىٰ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
وَأَنَّهُ أَهْلَكَ عَادًا الْأُولَىٰ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
وَثَمُودَ فَمَا أَبْقَىٰ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Na Thamudi hakuwabakisha,
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا هُمْ أَظْلَمَ وَأَطْغَىٰ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
وَالْمُؤْتَفِكَةَ أَهْوَىٰ ۝٥٣
📖 Tafsiri Aya 53
Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
فَغَشَّاهَا مَا غَشَّىٰ ۝٥٤
📖 Tafsiri Aya 54
Vikaifunika vilivyo funika.
فَبِأَيِّ آلَاءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ ۝٥٥
📖 Tafsiri Aya 55
Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
هَٰذَا نَذِيرٌ مِّنَ النُّذُرِ الْأُولَىٰ ۝٥٦
📖 Tafsiri Aya 56
Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
أَزِفَتِ الْآزِفَةُ ۝٥٧
📖 Tafsiri Aya 57
Kiyama kimekaribia!
لَيْسَ لَهَا مِن دُونِ اللَّهِ كَاشِفَةٌ ۝٥٨
📖 Tafsiri Aya 58
Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
أَفَمِنْ هَٰذَا الْحَدِيثِ تَعْجَبُونَ ۝٥٩
📖 Tafsiri Aya 59
Je! Mnayastaajabia maneno haya?
وَتَضْحَكُونَ وَلَا تَبْكُونَ ۝٦٠
📖 Tafsiri Aya 60
Na mnacheka, wala hamlii?
وَأَنتُمْ سَامِدُونَ ۝٦١
📖 Tafsiri Aya 61
Nanyi mmeghafilika?
فَاسْجُدُوا لِلَّهِ وَاعْبُدُوا ۩ ۝٦٢
📖 Tafsiri Aya 62
Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
← 52 An-Najm (53/114) 54 →
Soma Sura An-Najm kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

53النجم An-Najm 📚 62 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema