Sura Nuh
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Nuh pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Nuh pdf Kiswahili — Pakua Sura Nuh Tafsiri. Nuh (Makka) 28 Aya.
Related
- Nuh TafsiriKiswahili
- Nuh mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Nuh

ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
ﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰ
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
ﮱﯓﯔﯕﯖﯗ
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
ﯧﯨﯩﯪﯫ
Tena niliwaita kwa uwazi,
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
ﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?
ﭧﭨﭩﭪ
Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍ
Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
ﮎﮏﮐﮑﮒ
Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.
ﮡﮢﮣﮤ
Na wakapanga vitimbi vikubwa.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







