Sura Al-Ma'arij pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Ma'arij pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Ma'arij Tafsiri. Sura Al-Ma'arij (Makka) 44 Aya.
Related
- Sura Al-Ma'arij TafsiriKiswahili
- Sura Al-Ma'arij mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Ma'arij

ﮮﮯﮰﮱﯓ
70:1
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
ﯔﯕﯖﯗﯘ
70:2
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
ﯙﯚﯛﯜﯝ
70:3
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
70:4
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
ﯪﯫﯬﯭ
70:5
Basi subiri kwa subira njema.
ﯮﯯﯰﯱ
70:6
Hakika wao wanaiona iko mbali,
ﯲﯳﯴ
70:7
Na Sisi tunaiona iko karibu.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
70:8
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
ﯺﯻﯼﯽ
70:9
Na milima itakuwa kama sufi.
ﯾﯿﰀﰁﰂ
70:10
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
70:11
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
ﭜﭝﭞ
70:12
Na mkewe, na nduguye,
ﭟﭠﭡﭢ
70:13
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
70:14
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
ﭪﭫﭬﭭﭮ
70:15
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
ﭯﭰﭱ
70:16
Unao babua ngozi ya kichwa!
ﭲﭳﭴﭵﭶ
70:17
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
ﭷﭸﭹ
70:18
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
70:19
Hakika mtu ameumbwa na papara.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
70:20
Inapo mgusa shari hupapatika.
ﮅﮆﮇﮈﮉ
70:21
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
ﮊﮋﮌ
70:22
Isipo kuwa wanao sali,
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
70:23
Ambao wanadumisha Sala zao,
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
70:24
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
ﮙﮚﮛ
70:25
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
ﮜﮝﮞﮟﮠ
70:26
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
70:27
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
70:28
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
70:29
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
70:30
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
70:31
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
70:32
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
ﯭﯮﯯﯰﯱ
70:33
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
70:34
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
ﯸﯹﯺﯻﯼ
70:35
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
70:36
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
70:37
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
ﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
70:38
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘ
70:39
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
ﰙﰚﰛﰜﰝﰞﰟﰠ
70:40
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
70:41
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
70:42
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
70:43
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
70:44
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







