Sura Al-Ma'arij
PDF —
44 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Ma'arij pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Ma'arij pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Ma'arij Tafsiri. Al-Ma'arij (Makka) 44 Aya.



Sura Al-Ma'arij
44 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮮﮯﮰﮱﯓ
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
ﯔﯕﯖﯗﯘ
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
ﯙﯚﯛﯜﯝ
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
ﯪﯫﯬﯭ
Basi subiri kwa subira njema.
ﯮﯯﯰﯱ
Hakika wao wanaiona iko mbali,
ﯲﯳﯴ
Na Sisi tunaiona iko karibu.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
ﯺﯻﯼﯽ
Na milima itakuwa kama sufi.
ﯾﯿﰀﰁﰂ
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
ﭜﭝﭞ
Na mkewe, na nduguye,
ﭟﭠﭡﭢ
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
ﭪﭫﭬﭭﭮ
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
ﭯﭰﭱ
Unao babua ngozi ya kichwa!
ﭲﭳﭴﭵﭶ
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
ﭷﭸﭹ
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Hakika mtu ameumbwa na papara.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
Inapo mgusa shari hupapatika.
ﮅﮆﮇﮈﮉ
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
ﮊﮋﮌ
Isipo kuwa wanao sali,
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Ambao wanadumisha Sala zao,
ﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
ﮙﮚﮛ
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
ﮜﮝﮞﮟﮠ
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
ﯭﯮﯯﯰﯱ
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
ﯸﯹﯺﯻﯼ
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
ﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
ﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗﰘ
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
ﰙﰚﰛﰜﰝﰞﰟﰠ
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema