PDF —
182 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura As-Saffat pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura As-Saffat pdf Kiswahili — Pakua Sura As-Saffat Tafsiri. Sura As-Saffat (Makka) 182 Aya.

← Ya-SinSura As-Saffat Sad →


182 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓ
37:1 Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
ﭔﭕﭖ
37:2 Na kwa wenye kukataza mabaya.
ﭗﭘﭙ
37:3 Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
ﭚﭛﭜﭝ
37:4 Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
37:5 Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
37:6 Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
37:7 Na kulinda na kila shet'ani a'si.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
37:8 Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
37:9 Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
37:10 Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
37:11 Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
ﮙﮚﮛﮜ
37:12 Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
37:13 Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
ﮢﮣﮤﮥﮦ
37:14 Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
37:15 Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
37:16 Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
ﯗﯘﯙ
37:17 Hata baba zetu wa zamani?
ﯚﯛﯜﯝﯞ
37:18 Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
37:19 Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
37:20 Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
37:21 Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
37:22 Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
37:23 Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
ﰆﰇﰈﰉﰊ
37:24 Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:25 Mna nini? Mbona hamsaidiani?
ﭖﭗﭘﭙﭚ
37:26 Bali hii leo, watasalimu amri.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
37:27 Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
37:28 Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
37:29 Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
37:30 Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
37:31 Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
ﮂﮃﮄﮅﮆ
37:32 Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
37:33 Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
ﮍﮎﮏﮐﮑ
37:34 Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
37:35 Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
37:36 Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
37:37 Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
37:38 Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
37:39 Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
ﯗﯘﯙﯚﯛ
37:40 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠ
37:41 Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
ﯡﯢﯣﯤ
37:42 Matunda, nao watahishimiwa.
ﯥﯦﯧﯨ
37:43 Katika Bustani za neema.
ﯩﯪﯫﯬ
37:44 Wako juu ya viti wamekabiliana.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
37:45 Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
ﯳﯴﯵﯶ
37:46 Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
37:47 Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
ﯿﰀﰁﰂﰃ
37:48 Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
ﰄﰅﰆﰇ
37:49 Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
ﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
37:50 Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
37:51 Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:52 Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
37:53 Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
37:54 Atasema: Je! Nyie mnawaona?
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
37:55 Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
37:56 Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
37:57 Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
ﭶﭷﭸﭹ
37:58 Je! Sisi hatutakufa,
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
37:59 Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
37:60 Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
ﮇﮈﮉﮊﮋ
37:61 Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
37:62 Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
ﮓﮔﮕﮖﮗ
37:63 Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
37:64 Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
ﮟﮠﮡﮢﮣ
37:65 Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
37:66 Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
37:67 Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
37:68 Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
ﯚﯛﯜﯝﯞ
37:69 Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
37:70 Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
37:71 Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
ﯪﯫﯬﯭﯮ
37:72 Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
37:73 Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
37:74 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
37:75 Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
37:76 Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:77 Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
ﭖﭗﭘﭙﭚ
37:78 Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
37:79 Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
ﭡﭢﭣﭤﭥ
37:80 Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
ﭦﭧﭨﭩﭪ
37:81 Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭫﭬﭭﭮ
37:82 Kisha tukawazamisha wale wengine.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
37:83 Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
37:84 Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
37:85 Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
37:86 Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
ﮈﮉﮊﮋﮌ
37:87 Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﮍﮎﮏﮐﮑ
37:88 Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
ﮒﮓﮔﮕ
37:89 Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
ﮖﮗﮘﮙ
37:90 Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
37:91 Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
ﮡﮢﮣﮤﮥ
37:92 Mna nini hata hamsemi?
ﮦﮧﮨﮩﮪ
37:93 Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
ﮫﮬﮭﮮ
37:94 Basi wakamjia upesi upesi.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
37:95 Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
ﯕﯖﯗﯘﯙ
37:96 Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
37:97 Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
37:98 Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
37:99 Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
37:100 Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
ﯵﯶﯷﯸ
37:101 Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
37:102 Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:103 Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
ﭖﭗﭘﭙ
37:104 Tulimwita: Ewe Ibrahim!
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
37:105 Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
37:106 Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
ﭩﭪﭫﭬ
37:107 Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
ﭭﭮﭯﭰﭱ
37:108 Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
ﭲﭳﭴﭵ
37:109 Iwe salama kwa Ibrahim!
ﭶﭷﭸﭹ
37:110 Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
37:111 Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
37:112 Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
37:113 Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
37:114 Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
37:115 Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
37:116 Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
ﮢﮣﮤﮥ
37:117 Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
ﮦﮧﮨﮩ
37:118 Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
37:119 Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
37:120 Iwe salama kwa Musa na Haruni!
ﯕﯖﯗﯘﯙ
37:121 Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
ﯚﯛﯜﯝﯞ
37:122 Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
37:123 Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
37:124 Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
37:125 Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
37:126 Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
ﭑﭒﭓﭔ
37:127 Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
ﭕﭖﭗﭘﭙ
37:128 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
ﭚﭛﭜﭝﭞ
37:129 Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
37:130 Iwe salama kwa Ilyas.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
37:131 Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
ﭩﭪﭫﭬﭭ
37:132 Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
37:133 Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
ﭳﭴﭵﭶﭷ
37:134 Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
ﭸﭹﭺﭻﭼ
37:135 Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
ﭽﭾﭿﮀ
37:136 Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
ﮁﮂﮃﮄﮅ
37:137 Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
ﮆﮇﮈﮉﮊ
37:138 Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
ﮋﮌﮍﮎﮏ
37:139 Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
37:140 Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
ﮖﮗﮘﮙﮚ
37:141 Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
37:142 Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
37:143 Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
37:144 Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
37:145 Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
37:146 Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
37:147 Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
ﯡﯢﯣﯤﯥ
37:148 Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
37:149 Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
37:150 Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
37:151 Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
ﯹﯺﯻﯼﯽ
37:152 Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
ﯾﯿﰀﰁﰂ
37:153 Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:154 Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
ﭖﭗﭘ
37:155 Hamkumbuki?
ﭙﭚﭛﭜﭝ
37:156 Au mnayo hoja iliyo wazi?
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
37:157 Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
37:158 Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
37:159 Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
ﭵﭶﭷﭸﭹ
37:160 Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
ﭺﭻﭼﭽ
37:161 Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
ﭾﭿﮀﮁﮂ
37:162 Hamwezi kuwapoteza
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
37:163 Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
37:164 Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
ﮐﮑﮒﮓ
37:165 Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
ﮔﮕﮖﮗ
37:166 Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
ﮘﮙﮚﮛ
37:167 Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
37:168 Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
ﮣﮤﮥﮦﮧ
37:169 Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
37:170 Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
37:171 Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
ﯕﯖﯗﯘ
37:172 Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
ﯙﯚﯛﯜﯝ
37:173 Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
ﯞﯟﯠﯡﯢ
37:174 Basi waachilie mbali kwa muda.
ﯣﯤﯥﯦ
37:175 Na watazame, nao wataona.
ﯧﯨﯩ
37:176 Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
37:177 Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
ﯱﯲﯳﯴﯵ
37:178 Na waache kwa muda.
ﯶﯷﯸﯹ
37:179 Na tazama, na wao wataona.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
37:180 Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
ﰁﰂﰃﰄ
37:181 Na Salamu juu ya Mitume.
ﰅﰆﰇﰈﰉ
37:182 Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema