Sura As-Saffat pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura As-Saffat pdf Kiswahili — Pakua Sura As-Saffat Tafsiri. Sura As-Saffat (Makka) 182 Aya.
Related
- Sura As-Saffat TafsiriKiswahili
- Sura As-Saffat mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura As-Saffat

ﭑﭒﭓ
37:1
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
ﭔﭕﭖ
37:2
Na kwa wenye kukataza mabaya.
ﭗﭘﭙ
37:3
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
ﭚﭛﭜﭝ
37:4
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
37:5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
37:6
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
37:7
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
37:8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
37:9
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
37:10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
37:11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
ﮙﮚﮛﮜ
37:12
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
37:13
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
ﮢﮣﮤﮥﮦ
37:14
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
37:15
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
37:16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
ﯗﯘﯙ
37:17
Hata baba zetu wa zamani?
ﯚﯛﯜﯝﯞ
37:18
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
37:19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
37:20
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
37:21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
37:22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
37:23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
ﰆﰇﰈﰉﰊ
37:24
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:25
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
ﭖﭗﭘﭙﭚ
37:26
Bali hii leo, watasalimu amri.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
37:27
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
37:28
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
37:29
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
37:30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
37:31
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
ﮂﮃﮄﮅﮆ
37:32
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
37:33
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
ﮍﮎﮏﮐﮑ
37:34
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
37:35
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
37:36
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
37:37
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
37:38
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
37:39
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
ﯗﯘﯙﯚﯛ
37:40
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠ
37:41
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
ﯡﯢﯣﯤ
37:42
Matunda, nao watahishimiwa.
ﯥﯦﯧﯨ
37:43
Katika Bustani za neema.
ﯩﯪﯫﯬ
37:44
Wako juu ya viti wamekabiliana.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
37:45
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
ﯳﯴﯵﯶ
37:46
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
37:47
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
ﯿﰀﰁﰂﰃ
37:48
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
ﰄﰅﰆﰇ
37:49
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
ﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
37:50
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
37:51
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:52
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
37:53
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
37:54
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
37:55
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
37:56
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
37:57
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
ﭶﭷﭸﭹ
37:58
Je! Sisi hatutakufa,
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
37:59
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
37:60
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
ﮇﮈﮉﮊﮋ
37:61
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
37:62
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
ﮓﮔﮕﮖﮗ
37:63
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
37:64
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
ﮟﮠﮡﮢﮣ
37:65
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
37:66
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
37:67
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
37:68
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
ﯚﯛﯜﯝﯞ
37:69
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
37:70
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
37:71
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
ﯪﯫﯬﯭﯮ
37:72
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
37:73
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
37:74
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
37:75
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
37:76
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:77
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
ﭖﭗﭘﭙﭚ
37:78
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
37:79
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
ﭡﭢﭣﭤﭥ
37:80
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
ﭦﭧﭨﭩﭪ
37:81
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭫﭬﭭﭮ
37:82
Kisha tukawazamisha wale wengine.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
37:83
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
37:84
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
37:85
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
37:86
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
ﮈﮉﮊﮋﮌ
37:87
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﮍﮎﮏﮐﮑ
37:88
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
ﮒﮓﮔﮕ
37:89
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
ﮖﮗﮘﮙ
37:90
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
37:91
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
ﮡﮢﮣﮤﮥ
37:92
Mna nini hata hamsemi?
ﮦﮧﮨﮩﮪ
37:93
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
ﮫﮬﮭﮮ
37:94
Basi wakamjia upesi upesi.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
37:95
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
ﯕﯖﯗﯘﯙ
37:96
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
37:97
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
37:98
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
37:99
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
37:100
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
ﯵﯶﯷﯸ
37:101
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
37:102
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:103
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
ﭖﭗﭘﭙ
37:104
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
37:105
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
37:106
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
ﭩﭪﭫﭬ
37:107
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
ﭭﭮﭯﭰﭱ
37:108
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
ﭲﭳﭴﭵ
37:109
Iwe salama kwa Ibrahim!
ﭶﭷﭸﭹ
37:110
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
37:111
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
37:112
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
37:113
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
37:114
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
37:115
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
37:116
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
ﮢﮣﮤﮥ
37:117
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
ﮦﮧﮨﮩ
37:118
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
37:119
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
37:120
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
ﯕﯖﯗﯘﯙ
37:121
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
ﯚﯛﯜﯝﯞ
37:122
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
37:123
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
37:124
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
37:125
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
37:126
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
ﭑﭒﭓﭔ
37:127
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
ﭕﭖﭗﭘﭙ
37:128
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
ﭚﭛﭜﭝﭞ
37:129
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
37:130
Iwe salama kwa Ilyas.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
37:131
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
ﭩﭪﭫﭬﭭ
37:132
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
37:133
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
ﭳﭴﭵﭶﭷ
37:134
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
ﭸﭹﭺﭻﭼ
37:135
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
ﭽﭾﭿﮀ
37:136
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
ﮁﮂﮃﮄﮅ
37:137
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
ﮆﮇﮈﮉﮊ
37:138
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
ﮋﮌﮍﮎﮏ
37:139
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
37:140
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
ﮖﮗﮘﮙﮚ
37:141
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
37:142
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
37:143
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
37:144
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
37:145
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
37:146
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
37:147
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
ﯡﯢﯣﯤﯥ
37:148
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
37:149
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
37:150
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
37:151
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
ﯹﯺﯻﯼﯽ
37:152
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
ﯾﯿﰀﰁﰂ
37:153
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
ﭑﭒﭓﭔﭕ
37:154
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
ﭖﭗﭘ
37:155
Hamkumbuki?
ﭙﭚﭛﭜﭝ
37:156
Au mnayo hoja iliyo wazi?
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
37:157
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
37:158
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
37:159
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
ﭵﭶﭷﭸﭹ
37:160
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
ﭺﭻﭼﭽ
37:161
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
ﭾﭿﮀﮁﮂ
37:162
Hamwezi kuwapoteza
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
37:163
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
37:164
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
ﮐﮑﮒﮓ
37:165
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
ﮔﮕﮖﮗ
37:166
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
ﮘﮙﮚﮛ
37:167
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
37:168
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
ﮣﮤﮥﮦﮧ
37:169
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
37:170
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
37:171
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
ﯕﯖﯗﯘ
37:172
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
ﯙﯚﯛﯜﯝ
37:173
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
ﯞﯟﯠﯡﯢ
37:174
Basi waachilie mbali kwa muda.
ﯣﯤﯥﯦ
37:175
Na watazame, nao wataona.
ﯧﯨﯩ
37:176
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
37:177
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
ﯱﯲﯳﯴﯵ
37:178
Na waache kwa muda.
ﯶﯷﯸﯹ
37:179
Na tazama, na wao wataona.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
37:180
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
ﰁﰂﰃﰄ
37:181
Na Salamu juu ya Mitume.
ﰅﰆﰇﰈﰉ
37:182
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







