Sura As-Saffat
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura As-Saffat pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura As-Saffat pdf Kiswahili — Pakua Sura As-Saffat Tafsiri. As-Saffat (Makka) 182 Aya.
Related
- As-Saffat TafsiriKiswahili
- As-Saffat mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura As-Saffat

ﭑﭒﭓ
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
ﭔﭕﭖ
Na kwa wenye kukataza mabaya.
ﭗﭘﭙ
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
ﭚﭛﭜﭝ
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘ
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
ﮙﮚﮛﮜ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
ﮢﮣﮤﮥﮦ
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
ﯗﯘﯙ
Hata baba zetu wa zamani?
ﯚﯛﯜﯝﯞ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
ﰆﰇﰈﰉﰊ
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
ﭖﭗﭘﭙﭚ
Bali hii leo, watasalimu amri.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
ﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
ﮂﮃﮄﮅﮆ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
ﮍﮎﮏﮐﮑ
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
ﯗﯘﯙﯚﯛ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
ﯜﯝﯞﯟﯠ
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
ﯡﯢﯣﯤ
Matunda, nao watahishimiwa.
ﯥﯦﯧﯨ
Katika Bustani za neema.
ﯩﯪﯫﯬ
Wako juu ya viti wamekabiliana.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
ﯳﯴﯵﯶ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
ﯿﰀﰁﰂﰃ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
ﰄﰅﰆﰇ
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
ﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
ﭶﭷﭸﭹ
Je! Sisi hatutakufa,
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀ
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
ﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
ﮇﮈﮉﮊﮋ
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
ﮓﮔﮕﮖﮗ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
ﮟﮠﮡﮢﮣ
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
ﯚﯛﯜﯝﯞ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
ﯪﯫﯬﯭﯮ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
ﯵﯶﯷﯸﯹ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
ﭖﭗﭘﭙﭚ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
ﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
ﭡﭢﭣﭤﭥ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
ﭦﭧﭨﭩﭪ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭫﭬﭭﭮ
Kisha tukawazamisha wale wengine.
ﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺ
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
ﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
ﮈﮉﮊﮋﮌ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﮍﮎﮏﮐﮑ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
ﮒﮓﮔﮕ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
ﮖﮗﮘﮙ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
ﮡﮢﮣﮤﮥ
Mna nini hata hamsemi?
ﮦﮧﮨﮩﮪ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
ﮫﮬﮭﮮ
Basi wakamjia upesi upesi.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
ﯕﯖﯗﯘﯙ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
ﯵﯶﯷﯸ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
ﭖﭗﭘﭙ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
ﭩﭪﭫﭬ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
ﭭﭮﭯﭰﭱ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
ﭲﭳﭴﭵ
Iwe salama kwa Ibrahim!
ﭶﭷﭸﭹ
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
ﮝﮞﮟﮠﮡ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
ﮢﮣﮤﮥ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
ﮦﮧﮨﮩ
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
ﮪﮫﮬﮭﮮ
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
ﯕﯖﯗﯘﯙ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
ﯚﯛﯜﯝﯞ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
ﯟﯠﯡﯢﯣ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
ﭑﭒﭓﭔ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
ﭕﭖﭗﭘﭙ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
ﭚﭛﭜﭝﭞ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
Iwe salama kwa Ilyas.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
ﭩﭪﭫﭬﭭ
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ﭮﭯﭰﭱﭲ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
ﭳﭴﭵﭶﭷ
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
ﭸﭹﭺﭻﭼ
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
ﭽﭾﭿﮀ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
ﮁﮂﮃﮄﮅ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
ﮆﮇﮈﮉﮊ
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
ﮋﮌﮍﮎﮏ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
ﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
ﮖﮗﮘﮙﮚ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥ
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
ﯡﯢﯣﯤﯥ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
ﯹﯺﯻﯼﯽ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
ﯾﯿﰀﰁﰂ
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
ﭖﭗﭘ
Hamkumbuki?
ﭙﭚﭛﭜﭝ
Au mnayo hoja iliyo wazi?
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯ
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
ﭰﭱﭲﭳﭴ
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
ﭵﭶﭷﭸﭹ
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
ﭺﭻﭼﭽ
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
ﭾﭿﮀﮁﮂ
Hamwezi kuwapoteza
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
ﮐﮑﮒﮓ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
ﮔﮕﮖﮗ
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
ﮘﮙﮚﮛ
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
ﮣﮤﮥﮦﮧ
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
ﯕﯖﯗﯘ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
ﯙﯚﯛﯜﯝ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
ﯞﯟﯠﯡﯢ
Basi waachilie mbali kwa muda.
ﯣﯤﯥﯦ
Na watazame, nao wataona.
ﯧﯨﯩ
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
ﯱﯲﯳﯴﯵ
Na waache kwa muda.
ﯶﯷﯸﯹ
Na tazama, na wao wataona.
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀ
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
ﰁﰂﰃﰄ
Na Salamu juu ya Mitume.
ﰅﰆﰇﰈﰉ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







