Sura Al-Bayyina
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Bayyina pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Bayyina pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Bayyina Tafsiri. Al-Bayyina (Madina) 8 Aya.
Related
- Al-Bayyina TafsiriKiswahili
- Al-Bayyina mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Bayyina

ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Hawakuwa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina waache walio nayo mpaka iwajie bayana,
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪ
Yaani Mtume aliye toka kwa Mwenyezi Mungu anaye wasomea kurasa zilizo takasika,
ﮫﮬﮭﮮ
Ndani yake mna maandiko yaliyo nyooka.
ﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa.
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yu radhi nao, na wao waradhi naye. Hayo ni kwa anaye mwogopa Mola wake Mlezi.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







