Sura Al-Muddaththir kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Al-Muddaththir na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (56 Aya — مكية). Al-Muddaththir Sikiliza, Al-Muddaththir Tafsiri, Al-Muddaththir mp3, Al-Muddaththir pdf.

Soma na Sikiliza Sura Al-Muddaththir

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Ewe uliye jigubika!
قُمْ فَأَنذِرْ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Simama uonye!
وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Na nguo zako, zisafishe.
وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Na yaliyo machafu yahame!
وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
فَإِذَا نُقِرَ فِي النَّاقُورِ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Basi litapo pulizwa barugumu,
فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍ يَوْمٌ عَسِيرٌ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
عَلَى الْكَافِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Niache peke yangu na niliye muumba;
وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَّمْدُودًا ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
وَبَنِينَ شُهُودًا ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Na wana wanao onekana,
وَمَهَّدتُّ لَهُ تَمْهِيدًا ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Kisha anatumai nimzidishie!
كَلَّا ۖ إِنَّهُ كَانَ لِآيَاتِنَا عَنِيدًا ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
سَأُرْهِقُهُ صَعُودًا ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
إِنَّهُ فَكَّرَ وَقَدَّرَ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
ثُمَّ نَظَرَ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Kisha akatazama,
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
ثُمَّ أَدْبَرَ وَاسْتَكْبَرَ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
فَقَالَ إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ يُؤْثَرُ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
إِنْ هَٰذَا إِلَّا قَوْلُ الْبَشَرِ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
سَأُصْلِيهِ سَقَرَ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سَقَرُ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
لَا تُبْقِي وَلَا تَذَرُ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Haubakishi wala hausazi.
لَوَّاحَةٌ لِّلْبَشَرِ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Unababua ngozi iwe nyeusi.
عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Juu yake wapo kumi na tisa.
وَمَا جَعَلْنَا أَصْحَابَ النَّارِ إِلَّا مَلَائِكَةً ۙ وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا لِيَسْتَيْقِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَيَزْدَادَ الَّذِينَ آمَنُوا إِيمَانًا ۙ وَلَا يَرْتَابَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَالْمُؤْمِنُونَ ۙ وَلِيَقُولَ الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْكَافِرُونَ مَاذَا أَرَادَ اللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلًا ۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللَّهُ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ ۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
كَلَّا وَالْقَمَرِ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Hasha! Naapa kwa mwezi!
وَاللَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Na kwa usiku unapo kucha!
وَالصُّبْحِ إِذَا أَسْفَرَ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
إِنَّهَا لَإِحْدَى الْكُبَرِ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
نَذِيرًا لِّلْبَشَرِ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Ni onyo kwa binaadamu,
لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
إِلَّا أَصْحَابَ الْيَمِينِ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Isipo kuwa watu wa kuliani.
فِي جَنَّاتٍ يَتَسَاءَلُونَ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
عَنِ الْمُجْرِمِينَ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Khabari za wakosefu:
مَا سَلَكَكُمْ فِي سَقَرَ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
قَالُوا لَمْ نَكُ مِنَ الْمُصَلِّينَ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakisali.
وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ الْمِسْكِينَ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ الْخَائِضِينَ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ الدِّينِ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
حَتَّىٰ أَتَانَا الْيَقِينُ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Mpaka yakini ilipo tufikia.
فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَاعَةُ الشَّافِعِينَ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
فَمَا لَهُمْ عَنِ التَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
كَأَنَّهُمْ حُمُرٌ مُّسْتَنفِرَةٌ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Wanao mkimbia simba!
بَلْ يُرِيدُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًا مُّنَشَّرَةً ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
كَلَّا ۖ بَل لَّا يَخَافُونَ الْآخِرَةَ ۝٥٣
📖 Tafsiri Aya 53
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
كَلَّا إِنَّهُ تَذْكِرَةٌ ۝٥٤
📖 Tafsiri Aya 54
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ ۝٥٥
📖 Tafsiri Aya 55
Basi anaye taka atakumbuka.
وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّهُ ۚ هُوَ أَهْلُ التَّقْوَىٰ وَأَهْلُ الْمَغْفِرَةِ ۝٥٦
📖 Tafsiri Aya 56
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
← 73 Al-Muddaththir (74/114) 75 →
Soma Sura Al-Muddaththir kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

74المدثر Al-Muddaththir 📚 56 Aya مكية

Aya kwa aya – Sura Al-Muddaththir — 56 Aya




Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema