Sura Al-Qiyama
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Qiyama pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Qiyama pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qiyama Tafsiri. Al-Qiyama (Makka) 40 Aya.
Related
- Al-Qiyama TafsiriKiswahili
- Al-Qiyama mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Qiyama

ﮊﮋﮌﮍﮎ
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
ﮬﮭﮮﮯ
Basi jicho litapo dawaa,
ﮰﮱﯓ
Na mwezi utapo patwa,
ﯔﯕﯖﯗ
Na likakusanywa jua na mwezi,
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
ﯞﯟﯠﯡ
La! Hapana pa kukimbilia!
ﯢﯣﯤﯥﯦ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
ﯴﯵﯶﯷ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
ﯿﰀﰁﰂﰃ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
ﰄﰅﰆﰇﰈ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
ﰉﰊﰋﰌﰍ
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
ﭖﭗﭘ
Na mnaacha maisha ya Akhera.
ﭙﭚﭛﭜ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
ﭝﭞﭟﭠ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
ﭡﭢﭣﭤ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
ﭫﭬﭭﭮﭯ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
ﭰﭱﭲﭳﭴ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
ﭵﭶﭷﭸ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
ﭹﭺﭻﭼ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
ﭽﭾﭿﮀﮁ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
ﮂﮃﮄﮅﮆ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
ﮇﮈﮉﮊ
Bali alikanusha, na akageuka.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
ﮑﮒﮓﮔ
Ole wako, ole wako!
ﮕﮖﮗﮘﮙ
Kisha Ole wako, ole wako!
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







