Sura Al-Qiyama pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Qiyama pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qiyama Tafsiri. Sura Al-Qiyama (Makka) 40 Aya.
Related
- Sura Al-Qiyama TafsiriKiswahili
- Sura Al-Qiyama mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Qiyama

ﮊﮋﮌﮍﮎ
75:1
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
ﮏﮐﮑﮒﮓ
75:2
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
75:3
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
75:4
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
75:5
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
75:6
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
ﮬﮭﮮﮯ
75:7
Basi jicho litapo dawaa,
ﮰﮱﯓ
75:8
Na mwezi utapo patwa,
ﯔﯕﯖﯗ
75:9
Na likakusanywa jua na mwezi,
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
75:10
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
ﯞﯟﯠﯡ
75:11
La! Hapana pa kukimbilia!
ﯢﯣﯤﯥﯦ
75:12
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
75:13
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
75:14
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
ﯴﯵﯶﯷ
75:15
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
75:16
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
ﯿﰀﰁﰂﰃ
75:17
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
ﰄﰅﰆﰇﰈ
75:18
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
ﰉﰊﰋﰌﰍ
75:19
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
75:20
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
ﭖﭗﭘ
75:21
Na mnaacha maisha ya Akhera.
ﭙﭚﭛﭜ
75:22
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
ﭝﭞﭟﭠ
75:23
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
ﭡﭢﭣﭤ
75:24
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
75:25
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
ﭫﭬﭭﭮﭯ
75:26
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
ﭰﭱﭲﭳﭴ
75:27
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
ﭵﭶﭷﭸ
75:28
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
ﭹﭺﭻﭼ
75:29
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
ﭽﭾﭿﮀﮁ
75:30
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
ﮂﮃﮄﮅﮆ
75:31
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
ﮇﮈﮉﮊ
75:32
Bali alikanusha, na akageuka.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
75:33
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
ﮑﮒﮓﮔ
75:34
Ole wako, ole wako!
ﮕﮖﮗﮘﮙ
75:35
Kisha Ole wako, ole wako!
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
75:36
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
75:37
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
75:38
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
75:39
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
75:40
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







