PDF —
40 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Qiyama pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Qiyama pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qiyama Tafsiri. Sura Al-Qiyama (Makka) 40 Aya.



40 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮊﮋﮌﮍﮎ
75:1 Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
ﮏﮐﮑﮒﮓ
75:2 Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
75:3 Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
75:4 Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
75:5 Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
75:6 Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
ﮬﮭﮮﮯ
75:7 Basi jicho litapo dawaa,
ﮰﮱﯓ
75:8 Na mwezi utapo patwa,
ﯔﯕﯖﯗ
75:9 Na likakusanywa jua na mwezi,
ﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
75:10 Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
ﯞﯟﯠﯡ
75:11 La! Hapana pa kukimbilia!
ﯢﯣﯤﯥﯦ
75:12 Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
ﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
75:13 Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
ﯮﯯﯰﯱﯲﯳ
75:14 Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
ﯴﯵﯶﯷ
75:15 Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
75:16 Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
ﯿﰀﰁﰂﰃ
75:17 Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
ﰄﰅﰆﰇﰈ
75:18 Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
ﰉﰊﰋﰌﰍ
75:19 Kisha ni juu yetu kuubainisha.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
75:20 Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
ﭖﭗﭘ
75:21 Na mnaacha maisha ya Akhera.
ﭙﭚﭛﭜ
75:22 Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
ﭝﭞﭟﭠ
75:23 Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
ﭡﭢﭣﭤ
75:24 Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
75:25 Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
ﭫﭬﭭﭮﭯ
75:26 La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
ﭰﭱﭲﭳﭴ
75:27 Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
ﭵﭶﭷﭸ
75:28 Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
ﭹﭺﭻﭼ
75:29 Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
ﭽﭾﭿﮀﮁ
75:30 Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
ﮂﮃﮄﮅﮆ
75:31 Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
ﮇﮈﮉﮊ
75:32 Bali alikanusha, na akageuka.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
75:33 Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
ﮑﮒﮓﮔ
75:34 Ole wako, ole wako!
ﮕﮖﮗﮘﮙ
75:35 Kisha Ole wako, ole wako!
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
75:36 Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
75:37 Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
75:38 Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
75:39 Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
75:40 Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema