Al-Ahzab · 33/73
Tafsiri Uandishi wa sauti — Sura Al-Ahzab
وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ ۖ وَأَقِمْنَ الصَّلَاةَ وَآتِينَ الزَّكَاةَ وَأَطِعْنَ اللَّهَ وَرَسُولَهُ ۚ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ۝٣٣
Wa qarna fee bu yoo tikunna wa laa tabarrajna tabarrujal Jaahiliyyatil oolaa wa aqimnas Salaata w aaateenaz Zakaata wa ati`nal laaha wa Rasoolah; innamaa yureedul laahu liyuzhiba `ankumur rijsa Ahlal Bayti wa yutahhirakum tatheeraa
📖 Kwa Kiswahili
Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia ya kizamani. Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu, enyi Watu wa Nyumba ya Mtume, na kukusafisheni baarabara.

🎧 Sikiliza
📜

Tafsiri — Tafsir

Maana ya Maneno:

  • WaQarna: Kaa katika nyumba zenu kwa utulivu na usitoke nje isipokuwa kwa haja.
  • La Tabarrajna: Msijionyeshe kwa kufichua mapambo na urembo wenu kwa wanaume.
  • Al-Jahiliyyah al-Ula: Zama za ujahili wa kwanza kabla ya Uislamu, ambapo wanawake walikuwa wakijionyesha bila haya.
  • Ar-Rijs: Uchafu, dhambi, na maovu yote.

Tafsiri ya Aya:

Enyi wake za Mtume (SAW), kaeni nyumbani kwa utulivu, msitoke nje isipokuwa kwa haja ya dharura, wala msijionyeshe kwa kufichua mapambo na urembo wenu kwa wanaume wa kigeni kama walivyokuwa wakifanya wanawake wa zama za ujahili wa kwanza kabla ya Uislamu. Na zifanyeni sala kwa ukamilifu wake kwa wakati wake, toeni zakat ya mali zenu kama alivyoamrisha Mwenyezi Mungu, na mtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake katika kila amri na katazo. Hakika Mwenyezi Mungu anawatakasieni nyinyi, enyi Ahlul-Bayt (wake za Mtume na jamaa zake), na kuwaondolea kila uchafu, dhambi, na maovu, na kuitakasa roho zenu utakaso kamili usioacha chochote cha uchafu.


Faida Zinazotokana na Aya:

  1. Heshima na Utukufu wa Wanawake: Aya hii inaonyesha jinsi Uislamu unavyomheshimu mwanamke na kumlinda kutokana na kuonekana vibaya au kudharauliwa, kwa kumtaka akae nyumbani na asijionyeshe ovyo.
  2. Usafi wa Moyo na Roho: Mwenyezi Mungu anapenda kumtakasa mja wake kutokana na dhambi na maovu, na hii ni rehema kubwa kwetu sisi wote tunapojitahidi kufuata maelekezo Yake.
  3. Umuhimu wa Ibada: Kuamrisha sala na zakat pamoja na amri ya kukaa nyumbani kunathibitisha kwamba ibada ndio msingi wa maisha ya mwanamke Muislamu, na kwa kuzifanya anapata utulivu wa moyo na baraka za Mwenyezi Mungu.
  4. Utii kwa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake: Aya inatufundisha kwamba furaha ya kweli na usalama wa roho upo katika kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake (SAW), si katika kufuata anasa za dunia.
  5. Utakaso wa Ahlul-Bayt: Aya inaonyesha fadhila kubwa ya Ahlul-Bayt (wake za Mtume na jamaa zake), na hii inatufanya tuwapende na kuwaheshimu, na kujaribu kuiga tabia zao njema.
  6. Kujiepusha na Mambo ya Ujahili: Aya inatukumbusha kwamba tunapaswa kuepuka tabia za zama za ujahili, kama vile kujionyesha na kufichua mapambo, na badala yake tufuate mwongozo wa Kiislamu unaotutakasa na kutuheshimu.


📜 Aya 31-35 — Sura Al-Ahzab

31۞ وَمَن يَقْنُتْ مِنكُنَّ لِلَّهِ وَرَسُولِهِ وَتَعْمَلْ صَالِحًا نُّؤْتِهَا أَجْرَهَا مَرَّتَيْنِ وَأَعْتَدْنَا لَهَا رِزْقًا كَرِيمًا
NA MIONGONI mwenu atakeye mt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na akatenda mema, tutampa malipo yake mara mbili, na tutamwandalia riziki ya ukarimu.
32يَا نِسَاءَ النَّبِيِّ لَسْتُنَّ كَأَحَدٍ مِّنَ النِّسَاءِ ۚ إِنِ اتَّقَيْتُنَّ فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ مَرَضٌ وَقُلْنَ قَوْلًا مَّعْرُوفًا
Enyi wake wa Nabii! Nyinyi si kama yeyote katika wanawake wengine. Kama mnamcha Mungu basi msiregeze sauti zenu, akaingia tamaa mwenye maradhi katika moyo wake. Na semeni maneno mema.
33وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ ۖ وَأَقِمْنَ الصَّلَاةَ وَآتِينَ الزَّكَاةَ وَأَطِعْنَ اللَّهَ وَرَسُولَهُ ۚ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا
Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia ya kizamani. Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mt'iini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Hakika Mwenyezi Mungu anataka kukuondoleeni uchafu, enyi Watu wa Nyumba ya Mtume, na kukusafisheni baarabara.
34وَاذْكُرْنَ مَا يُتْلَىٰ فِي بُيُوتِكُنَّ مِنْ آيَاتِ اللَّهِ وَالْحِكْمَةِ ۚ إِنَّ اللَّهَ كَانَ لَطِيفًا خَبِيرًا
Na kumbukeni yasomwayo majumbani mwenu katika Aya za Mwenyezi Mungu na hikima. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo ya siri, na Mwenye khabari.
35إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ وَالْحَافِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَالْحَافِظَاتِ وَالذَّاكِرِينَ اللَّهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا
Hakika Waislamu wanaume na Waislamu wanawake, na Waumini wanaume na Waumini wanawake, na wat'iifu wanaume na wat'iifu wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanao subiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao sadaka wanaume na wanawake, na wanao funga wanaume na wanawake, na wanao jihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, na wanao mdhukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi wanaume na wanawake, Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na ujira mkubwa.
Al-AhzabFaharasa ya Qurani
73Aya
MadinaRevelation
33Aya

Tafsiri — Al-Ahzab 33

Sura Al-Ahzab Aya 33 - Soma, Sikiliza, Tafsiri, Kiswahili : Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia…

Sura Aya 33/73 — Sura Al-Ahzab الأحزاب (Madina). Soma Sikiliza Tafsiri (Kiswahili). Sikiliza: Sura Al-Ahzab Sikiliza, Sura Al-Ahzab Tafsiri, Sura Al-Ahzab mp3, Sura Al-Ahzab pdf. Aya 31–35. Kwa Kiswahili: Soomaali.




Kurani Tukufu


Monday, September 7, 2026

Usitusahau katika dua zako njema