PDF —
11 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-'Adiyat pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-'Adiyat pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-'Adiyat Tafsiri. Sura Al-'Adiyat (Makka) 11 Aya.



11 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮱﯓﯔ
100:1 Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
ﯕﯖﯗ
100:2 Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
ﯘﯙﯚ
100:3 Wakishambulia wakati wa asubuhi,
ﯛﯜﯝﯞ
100:4 Huku wakitimua vumbi,
ﯟﯠﯡﯢ
100:5 Na wakijitoma kati ya kundi,
ﭑﭒﭓﭔﭕ
100:6 Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
ﭖﭗﭘﭙﭚ
100:7 Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
ﭛﭜﭝﭞﭟ
100:8 Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
ﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
100:9 Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
ﭩﭪﭫﭬﭭ
100:10 Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
ﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
100:11 Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema