Sura Sad
88 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
S'ad, Naapa kwa Qur'ani yenye mawaidha.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
ﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi.
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu.
ﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.
ﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓ
Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥ
Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye.
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hikima, na kukata hukumu.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻﭼ
Na je! Imekufikia khabari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani?
ﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno.
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia.
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Basi tukamsamehe kwa hayo. Naye kwa hakika anao mkaribisho mkubwa na marejeo mazuri kwetu.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖ
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa katika nchi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanao ipotea Njia ya Mwenyezi Mungu wakaiacha, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utao wapata.
ﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱ
Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu?
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Na Daudi tukamtunukia Suleiman. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Alipo pelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma.
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟ
(Akasema:) Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.
ﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu.
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika.
ﯥﯦﯧﯨﯩ
Na tukayafanya mashet'ani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.
ﯪﯫﯬﯭﯮ
Na wengine wafungwao kwa minyororo.
ﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hisabu.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.
ﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shet'ani amenifikishia udhia na adhabu.
ﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑ
(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iwe kumbusho kwa watu wenye akili.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu walio kuwa na nguvu na busara.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Sisi tumewakhusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora.
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋ
Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora.
ﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Huu ni ukumbusho. Na hakika wachamngu wana marudio mazuri.
ﮔﮕﮖﮗﮘﮙ
Bustani za milele zitazo funguliwa milango yao kwa ajili yao.
ﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji.
ﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao.
ﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.
ﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕﯖ
Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;
ﯞﯟﯠﯡﯢ
Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.
ﯣﯤﯥﯦﯧ
Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!
ﯨﯩﯪﯫﯬ
Na adhabu nyenginezo za namna hii.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa!
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒ
Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu?
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu hayawaoni?
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu,
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
ﭿﮀﮁﮂﮃ
Sema: Hii ni khabari kubwa kabisa.
ﮄﮅﮆﮇ
Ambayo nyinyi mnaipuuza.
ﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Sikuwa na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri.
ﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤ
Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.
ﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.
ﮯﮰﮱﯓﯔ
Basi Malaika wakat'ii wote pamoja.
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?
ﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃ
Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe.
ﰋﰌﰍﰎﰏ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,
ﰐﰑﰒﰓﰔ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
ﰕﰖﰗﰘﰙ
Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,
ﰚﰛﰜﰝﰞ
Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio khitariwa.
ﭑﭒﭓﭔﭕ
Akasema: Haki! Na haki ninaisema.
ﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao.
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Sema (Ewe Mtume): Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮ
Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.
ﭯﭰﭱﭲﭳ
Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema