Sura Al-Insan
PDF —
31 Aya Madina PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Insan pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Insan pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Insan Tafsiri. Al-Insan (Madina) 31 Aya.



Sura Al-Insan
31 Aya · Madina · Kiswahili
bismillah
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
ﯕﯖﯗﯘﯙ
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛ
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema