PDF —
31 Aya Madina PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Insan pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Insan pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Insan Tafsiri. Sura Al-Insan (Madina) 31 Aya.



31 Aya · Madina · Kiswahili
bismillah
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
76:1 Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
76:2 Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
76:3 Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
76:4 Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
76:5 Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
76:6 Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
76:7 Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
76:8 Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
76:9 Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
76:10 Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
76:11 Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
76:12 Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
76:13 Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
76:14 Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
76:15 Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
76:16 Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
76:17 Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
ﯕﯖﯗﯘﯙ
76:18 Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
76:19 Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
76:20 Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
76:21 Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
76:22 Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
76:23 Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
76:24 Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛ
76:25 Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
76:26 Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
76:27 Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
76:28 Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
76:29 Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
76:30 Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
76:31 Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema