Sura Al-Insan pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Insan pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Insan Tafsiri. Sura Al-Insan (Madina) 31 Aya.
Related
- Sura Al-Insan TafsiriKiswahili
- Sura Al-Insan mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Insan

ﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
76:1
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
76:2
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺ
76:3
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
ﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
76:4
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉﰊ
76:5
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
76:6
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
76:7
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
76:8
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
ﭩﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳ
76:9
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
ﭴﭵﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
76:10
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
76:11
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
76:12
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
76:13
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
76:14
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
76:15
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
ﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
76:16
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
ﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔ
76:17
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
ﯕﯖﯗﯘﯙ
76:18
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
ﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
76:19
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
76:20
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲﯳﯴﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻ
76:21
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
ﯼﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄ
76:22
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
ﰅﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
76:23
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
ﰌﰍﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕ
76:24
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
ﰖﰗﰘﰙﰚﰛ
76:25
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘ
76:26
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
ﭙﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
76:27
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
ﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩﭪﭫﭬ
76:28
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
76:29
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
ﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄ
76:30
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
76:31
Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







