Sura Al-Mursalat
PDF —
50 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Mursalat pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Mursalat pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Mursalat Tafsiri. Al-Mursalat (Makka) 50 Aya.



Sura Al-Mursalat
50 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮑﮒﮓ
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
ﮔﮕﮖ
Na zinazo vuma kwa kasi!
ﮗﮘﮙ
Na zikaeneza maeneo yote!
ﮚﮛﮜ
Na zinazo farikisha zikatawanya!
ﮝﮞﮟ
Na zinazo peleka mawaidha!
ﮠﮡﮢﮣ
Kwa kuudhuru au kuonya,
ﮤﮥﮦﮧ
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
ﮨﮩﮪﮫ
Wakati nyota zitakapo futwa,
ﮬﮭﮮﮯ
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
ﮰﮱﯓﯔ
Na milima itakapo peperushwa,
ﯕﯖﯗﯘ
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
ﯙﯚﯛﯜ
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
ﯝﯞﯟ
Kwa siku ya kupambanua!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
ﯦﯧﯨﯩ
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
ﯪﯫﯬﯭ
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
ﯮﯯﯰﯱ
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
ﯲﯳﯴﯵ
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
ﯶﯷﯸﯹ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
ﭗﭘﭙﭚﭛ
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
ﭜﭝﭞﭟ
Mpaka muda maalumu?
ﭠﭡﭢﭣ
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
ﭤﭥﭦﭧ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﭨﭩﭪﭫﭬ
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
ﭭﭮﭯ
Walio hai na maiti?
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
ﭸﭹﭺﭻ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
ﮑﮒﮓﮔﮕ
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
ﮖﮗﮘﮙ
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
ﮚﮛﮜﮝ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﮞﮟﮠﮡﮢ
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
ﮣﮤﮥﮦﮧ
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
ﮨﮩﮪﮫ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
ﯚﯛﯜﯝ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
ﯤﯥﯦﯧ
Na matunda wanayo yapenda,
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
ﯯﯰﯱﯲﯳ
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
ﯴﯵﯶﯷ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
ﯾﯿﰀﰁ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
ﰉﰊﰋﰌ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﰍﰎﰏﰐﰑ
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema