Sura Al-Mursalat pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Mursalat pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Mursalat Tafsiri. Sura Al-Mursalat (Makka) 50 Aya.
Related
- Sura Al-Mursalat TafsiriKiswahili
- Sura Al-Mursalat mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Mursalat

ﮑﮒﮓ
77:1
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
ﮔﮕﮖ
77:2
Na zinazo vuma kwa kasi!
ﮗﮘﮙ
77:3
Na zikaeneza maeneo yote!
ﮚﮛﮜ
77:4
Na zinazo farikisha zikatawanya!
ﮝﮞﮟ
77:5
Na zinazo peleka mawaidha!
ﮠﮡﮢﮣ
77:6
Kwa kuudhuru au kuonya,
ﮤﮥﮦﮧ
77:7
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
ﮨﮩﮪﮫ
77:8
Wakati nyota zitakapo futwa,
ﮬﮭﮮﮯ
77:9
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
ﮰﮱﯓﯔ
77:10
Na milima itakapo peperushwa,
ﯕﯖﯗﯘ
77:11
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
ﯙﯚﯛﯜ
77:12
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
ﯝﯞﯟ
77:13
Kwa siku ya kupambanua!
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
77:14
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
ﯦﯧﯨﯩ
77:15
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
ﯪﯫﯬﯭ
77:16
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
ﯮﯯﯰﯱ
77:17
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
ﯲﯳﯴﯵ
77:18
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
ﯶﯷﯸﯹ
77:19
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
77:20
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
ﭗﭘﭙﭚﭛ
77:21
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
ﭜﭝﭞﭟ
77:22
Mpaka muda maalumu?
ﭠﭡﭢﭣ
77:23
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
ﭤﭥﭦﭧ
77:24
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﭨﭩﭪﭫﭬ
77:25
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
ﭭﭮﭯ
77:26
Walio hai na maiti?
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷ
77:27
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
ﭸﭹﭺﭻ
77:28
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
77:29
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
77:30
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐ
77:31
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
ﮑﮒﮓﮔﮕ
77:32
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
ﮖﮗﮘﮙ
77:33
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
ﮚﮛﮜﮝ
77:34
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﮞﮟﮠﮡﮢ
77:35
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
ﮣﮤﮥﮦﮧ
77:36
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
ﮨﮩﮪﮫ
77:37
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓ
77:38
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
ﯔﯕﯖﯗﯘﯙ
77:39
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
ﯚﯛﯜﯝ
77:40
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣ
77:41
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
ﯤﯥﯦﯧ
77:42
Na matunda wanayo yapenda,
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮ
77:43
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
ﯯﯰﯱﯲﯳ
77:44
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
ﯴﯵﯶﯷ
77:45
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
77:46
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
ﯾﯿﰀﰁ
77:47
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈ
77:48
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
ﰉﰊﰋﰌ
77:49
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ﰍﰎﰏﰐﰑ
77:50
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







