Sura Ad-Duha
11 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮉﮊ
Naapa kwa mchana!
ﮋﮌﮍﮎ
Na kwa usiku unapo tanda!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
ﮠﮡﮢﮣﮤ
Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
ﮥﮦﮧﮨ
Na akakukuta umepotea akakuongoa?
ﮩﮪﮫﮬ
Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
ﮭﮮﮯﮰﮱ
Basi yatima usimwonee!
ﯓﯔﯕﯖﯗ
Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
ﯘﯙﯚﯛﯜ
Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema