Sura Al-Layl
21 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮡﮢﮣﮤ
Naapa kwa usiku unapo funika!
ﮥﮦﮧﮨ
Na mchana unapo dhihiri!
ﮩﮪﮫﮬﮭ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
ﮮﮯﮰﮱ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
ﯘﯙﯚ
Na akaliwafiki lilio jema,
ﯛﯜﯝ
Tutamsahilishia yawe mepesi.
ﯞﯟﯠﯡﯢ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
ﯣﯤﯥ
Na akakanusha lilio jema,
ﭑﭒﭓ
Tutamsahilishia yawe mazito!
ﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
ﭛﭜﭝﭞ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
ﭟﭠﭡﭢﭣ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
ﭤﭥﭦﭧ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
ﭨﭩﭪﭫﭬ
Hatauingia ila mwovu kabisa!
ﭭﭮﭯﭰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
ﭱﭲﭳ
Na mchamngu ataepushwa nao,
ﭴﭵﭶﭷﭸ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
ﮀﮁﮂﮃﮄﮅ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
ﮆﮇﮈ
Naye atakuja ridhika!

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema