Sura An-Nazi'at
PDF —
46 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura An-Nazi'at pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura An-Nazi'at pdf Kiswahili — Pakua Sura An-Nazi'at Tafsiri. An-Nazi'at (Makka) 46 Aya.



Sura An-Nazi'at
46 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮢﮣﮤ
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
ﮥﮦﮧ
Na kwa wanao toa kwa upole,
ﮨﮩﮪ
Na wanao ogelea,
ﮫﮬﮭ
Wakishindana mbio,
ﮮﮯﮰ
Wakidabiri mambo.
ﮱﯓﯔﯕ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
ﯖﯗﯘ
Kifuate cha kufuatia.
ﯙﯚﯛﯜ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
ﯝﯞﯟ
Macho yatainama chini.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
ﯦﯧﯨﯩﯪ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
ﯱﯲﯳﯴﯵ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
ﯶﯷﯸﯹ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
ﯺﯻﯼﯽﯾ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
ﭣﭤﭥﭦ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
ﭧﭨﭩ
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ﭪﭫﭬﭭ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
ﭮﭯﭰ
Akakusanya watu akanadi.
ﭱﭲﭳﭴﭵ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
ﮋﮌﮍﮎ
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
ﮔﮕﮖﮗﮘ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
ﮙﮚﮛﮜﮝ
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
ﮞﮟﮠ
Na milima akaisimamisha,
ﮡﮢﮣﮤ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
ﮥﮦﮧﮨﮩ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
ﮰﮱﯓﯔﯕ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
ﯖﯗﯘﯙ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
ﯚﯛﯜﯝ
Na akakhiari maisha ya dunia,
ﯞﯟﯠﯡﯢ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
ﯭﯮﯯﯰﯱ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
ﯸﯹﯺﯻﯼ
Una nini wewe hata uitaje?
ﯽﯾﯿﰀ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema