Sura An-Nazi'at pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura An-Nazi'at pdf Kiswahili — Pakua Sura An-Nazi'at Tafsiri. Sura An-Nazi'at (Makka) 46 Aya.
Related
- Sura An-Nazi'at TafsiriKiswahili
- Sura An-Nazi'at mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura An-Nazi'at

ﮢﮣﮤ
79:1
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
ﮥﮦﮧ
79:2
Na kwa wanao toa kwa upole,
ﮨﮩﮪ
79:3
Na wanao ogelea,
ﮫﮬﮭ
79:4
Wakishindana mbio,
ﮮﮯﮰ
79:5
Wakidabiri mambo.
ﮱﯓﯔﯕ
79:6
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
ﯖﯗﯘ
79:7
Kifuate cha kufuatia.
ﯙﯚﯛﯜ
79:8
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
ﯝﯞﯟ
79:9
Macho yatainama chini.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
79:10
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
ﯦﯧﯨﯩﯪ
79:11
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
ﯫﯬﯭﯮﯯﯰ
79:12
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
ﯱﯲﯳﯴﯵ
79:13
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
ﯶﯷﯸﯹ
79:14
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
ﯺﯻﯼﯽﯾ
79:15
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
ﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅ
79:16
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
79:17
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
79:18
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
ﭞﭟﭠﭡﭢ
79:19
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
ﭣﭤﭥﭦ
79:20
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
ﭧﭨﭩ
79:21
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ﭪﭫﭬﭭ
79:22
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
ﭮﭯﭰ
79:23
Akakusanya watu akanadi.
ﭱﭲﭳﭴﭵ
79:24
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
ﭶﭷﭸﭹﭺﭻ
79:25
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
79:26
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
79:27
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
ﮋﮌﮍﮎ
79:28
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
ﮏﮐﮑﮒﮓ
79:29
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
ﮔﮕﮖﮗﮘ
79:30
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
ﮙﮚﮛﮜﮝ
79:31
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
ﮞﮟﮠ
79:32
Na milima akaisimamisha,
ﮡﮢﮣﮤ
79:33
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
ﮥﮦﮧﮨﮩ
79:34
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯ
79:35
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
ﮰﮱﯓﯔﯕ
79:36
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
ﯖﯗﯘﯙ
79:37
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
ﯚﯛﯜﯝ
79:38
Na akakhiari maisha ya dunia,
ﯞﯟﯠﯡﯢ
79:39
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
ﯣﯤﯥﯦﯧﯨﯩﯪﯫﯬ
79:40
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
ﯭﯮﯯﯰﯱ
79:41
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
ﯲﯳﯴﯵﯶﯷ
79:42
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
ﯸﯹﯺﯻﯼ
79:43
Una nini wewe hata uitaje?
ﯽﯾﯿﰀ
79:44
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
ﰁﰂﰃﰄﰅﰆ
79:45
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍﰎﰏﰐ
79:46
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







