Sura Abasa pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Abasa pdf Kiswahili — Pakua Sura Abasa Tafsiri. Sura Abasa (Makka) 42 Aya.
Related
- Sura Abasa TafsiriKiswahili
- Sura Abasa mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Abasa

ﭑﭒﭓ
80:1
Alikunja kipaji na akageuka,
ﭔﭕﭖﭗ
80:2
Kwa sababu alimjia kipofu!
ﭘﭙﭚﭛﭜ
80:3
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
ﭝﭞﭟﭠﭡ
80:4
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
ﭢﭣﭤﭥ
80:5
Ama ajionaye hana haja,
ﭦﭧﭨﭩ
80:6
Wewe ndio unamshughulikia?
ﭪﭫﭬﭭﭮ
80:7
Na si juu yako kama hakutakasika.
ﭯﭰﭱﭲﭳ
80:8
Ama anaye kujia kwa juhudi,
ﭴﭵﭶ
80:9
Naye anaogopa,
ﭷﭸﭹﭺ
80:10
Ndio wewe unampuuza?
ﭻﭼﭽﭾ
80:11
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
ﭿﮀﮁﮂ
80:12
Basi anaye penda akumbuke.
ﮃﮄﮅﮆ
80:13
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
ﮇﮈﮉ
80:14
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
ﮊﮋﮌ
80:15
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
ﮍﮎﮏ
80:16
Watukufu, wema.
ﮐﮑﮒﮓﮔ
80:17
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
ﮕﮖﮗﮘﮙ
80:18
Kwa kitu gani amemuumba?
ﮚﮛﮜﮝﮞ
80:19
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
ﮟﮠﮡﮢ
80:20
Kisha akamsahilishia njia.
ﮣﮤﮥﮦ
80:21
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
80:22
Kisha apendapo atamfufua.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
80:23
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
80:24
Hebu mtu na atazame chakula chake.
ﯘﯙﯚﯛﯜ
80:25
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
ﯝﯞﯟﯠﯡ
80:26
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
ﯢﯣﯤﯥ
80:27
Kisha tukaotesha humo nafaka,
ﯦﯧﯨ
80:28
Na zabibu, na mimea ya majani,
ﯩﯪﯫ
80:29
Na mizaituni, na mitende,
ﯬﯭﯮ
80:30
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
ﯯﯰﯱ
80:31
Na matunda, na malisho ya wanyama;
ﯲﯳﯴﯵ
80:32
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
ﯶﯷﯸﯹ
80:33
Basi utakapo kuja ukelele,
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
80:34
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
ﰀﰁﰂ
80:35
Na mamaye na babaye,
ﰃﰄﰅ
80:36
Na mkewe na wanawe -
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
80:37
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
ﰍﰎﰏﰐ
80:38
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
ﰑﰒﰓ
80:39
Zitacheka, zitachangamka;
ﰔﰕﰖﰗﰘ
80:40
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
ﭑﭒﭓ
80:41
Giza totoro litazifunika,
ﭔﭕﭖﭗﭘ
80:42
Hao ndio makafiri watenda maovu.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







