Sura Abasa
42 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓ
Alikunja kipaji na akageuka,
ﭔﭕﭖﭗ
Kwa sababu alimjia kipofu!
ﭘﭙﭚﭛﭜ
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
ﭝﭞﭟﭠﭡ
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
ﭢﭣﭤﭥ
Ama ajionaye hana haja,
ﭦﭧﭨﭩ
Wewe ndio unamshughulikia?
ﭪﭫﭬﭭﭮ
Na si juu yako kama hakutakasika.
ﭯﭰﭱﭲﭳ
Ama anaye kujia kwa juhudi,
ﭴﭵﭶ
Naye anaogopa,
ﭷﭸﭹﭺ
Ndio wewe unampuuza?
ﭻﭼﭽﭾ
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
ﭿﮀﮁﮂ
Basi anaye penda akumbuke.
ﮃﮄﮅﮆ
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
ﮇﮈﮉ
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
ﮊﮋﮌ
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
ﮍﮎﮏ
Watukufu, wema.
ﮐﮑﮒﮓﮔ
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
ﮕﮖﮗﮘﮙ
Kwa kitu gani amemuumba?
ﮚﮛﮜﮝﮞ
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
ﮟﮠﮡﮢ
Kisha akamsahilishia njia.
ﮣﮤﮥﮦ
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
ﮧﮨﮩﮪﮫ
Kisha apendapo atamfufua.
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
ﯓﯔﯕﯖﯗ
Hebu mtu na atazame chakula chake.
ﯘﯙﯚﯛﯜ
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
ﯝﯞﯟﯠﯡ
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
ﯢﯣﯤﯥ
Kisha tukaotesha humo nafaka,
ﯦﯧﯨ
Na zabibu, na mimea ya majani,
ﯩﯪﯫ
Na mizaituni, na mitende,
ﯬﯭﯮ
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
ﯯﯰﯱ
Na matunda, na malisho ya wanyama;
ﯲﯳﯴﯵ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
ﯶﯷﯸﯹ
Basi utakapo kuja ukelele,
ﯺﯻﯼﯽﯾﯿ
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
ﰀﰁﰂ
Na mamaye na babaye,
ﰃﰄﰅ
Na mkewe na wanawe -
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
ﰍﰎﰏﰐ
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
ﰑﰒﰓ
Zitacheka, zitachangamka;
ﰔﰕﰖﰗﰘ
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
ﭑﭒﭓ
Giza totoro litazifunika,
ﭔﭕﭖﭗﭘ
Hao ndio makafiri watenda maovu.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema