Sura An-Naba
40 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓ
WANAULIZANA nini?
ﭔﭕﭖﭗ
Ile khabari kuu,
ﭘﭙﭚﭛﭜ
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
ﭝﭞﭟ
La! Karibu watakuja jua.
ﭠﭡﭢﭣ
Tena la! Karibu watakuja jua.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
ﭩﭪﭫ
Na milima kama vigingi?
ﭬﭭﭮ
Na tukakuumbeni kwa jozi?
ﭯﭰﭱﭲ
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
ﭳﭴﭵﭶ
Na tukaufanya usiku ni nguo?
ﭷﭸﭹﭺ
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
ﭻﭼﭽﭾﭿ
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
ﮀﮁﮂﮃ
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
ﮊﮋﮌﮍﮎ
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
ﮏﮐﮑ
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
ﮟﮠﮡﮢﮣ
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
ﮤﮥﮦﮧﮨ
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
Hakika Jahannamu inangojea!
ﮮﮯﮰ
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
ﮱﯓﯔﯕ
Wakae humo karne baada ya karne,
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
ﯝﯞﯟﯠ
Ila maji yamoto sana na usaha,
ﯡﯢﯣ
Ndio jaza muwafaka.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
ﯪﯫﯬﯭ
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
ﯮﯯﯰﯱﯲ
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
ﭑﭒﭓﭔ
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
ﭕﭖﭗ
Mabustani na mizabibu,
ﭘﭙﭚ
Na wake walio lingana nao,
ﭛﭜﭝ
Na bilauri zilizo jaa,
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema