Sura An-Naba pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura An-Naba pdf Kiswahili — Pakua Sura An-Naba Tafsiri. Sura An-Naba (Makka) 40 Aya.
Related
- Sura An-Naba TafsiriKiswahili
- Sura An-Naba mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura An-Naba

ﭑﭒﭓ
78:1
WANAULIZANA nini?
ﭔﭕﭖﭗ
78:2
Ile khabari kuu,
ﭘﭙﭚﭛﭜ
78:3
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
ﭝﭞﭟ
78:4
La! Karibu watakuja jua.
ﭠﭡﭢﭣ
78:5
Tena la! Karibu watakuja jua.
ﭤﭥﭦﭧﭨ
78:6
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
ﭩﭪﭫ
78:7
Na milima kama vigingi?
ﭬﭭﭮ
78:8
Na tukakuumbeni kwa jozi?
ﭯﭰﭱﭲ
78:9
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
ﭳﭴﭵﭶ
78:10
Na tukaufanya usiku ni nguo?
ﭷﭸﭹﭺ
78:11
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
ﭻﭼﭽﭾﭿ
78:12
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
ﮀﮁﮂﮃ
78:13
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
ﮄﮅﮆﮇﮈﮉ
78:14
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
ﮊﮋﮌﮍﮎ
78:15
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
ﮏﮐﮑ
78:16
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
78:17
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
78:18
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
ﮟﮠﮡﮢﮣ
78:19
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
ﮤﮥﮦﮧﮨ
78:20
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
ﮩﮪﮫﮬﮭ
78:21
Hakika Jahannamu inangojea!
ﮮﮯﮰ
78:22
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
ﮱﯓﯔﯕ
78:23
Wakae humo karne baada ya karne,
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
78:24
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
ﯝﯞﯟﯠ
78:25
Ila maji yamoto sana na usaha,
ﯡﯢﯣ
78:26
Ndio jaza muwafaka.
ﯤﯥﯦﯧﯨﯩ
78:27
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
ﯪﯫﯬﯭ
78:28
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
ﯮﯯﯰﯱﯲ
78:29
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
ﯳﯴﯵﯶﯷﯸ
78:30
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
ﭑﭒﭓﭔ
78:31
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
ﭕﭖﭗ
78:32
Mabustani na mizabibu,
ﭘﭙﭚ
78:33
Na wake walio lingana nao,
ﭛﭜﭝ
78:34
Na bilauri zilizo jaa,
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤ
78:35
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
ﭥﭦﭧﭨﭩﭪ
78:36
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
ﭫﭬﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
78:37
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆ
78:38
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑ
78:39
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
78:40
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







