Sura At-Takwir pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura At-Takwir pdf Kiswahili — Pakua Sura At-Takwir Tafsiri. Sura At-Takwir (Makka) 29 Aya.
Related
- Sura At-Takwir TafsiriKiswahili
- Sura At-Takwir mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura At-Takwir

ﭙﭚﭛﭜ
81:1
Jua litakapo kunjwa,
ﭝﭞﭟﭠ
81:2
Na nyota zikazimwa,
ﭡﭢﭣﭤ
81:3
Na milima ikaondolewa,
ﭥﭦﭧﭨ
81:4
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
ﭩﭪﭫﭬ
81:5
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
ﭭﭮﭯﭰ
81:6
Na bahari zikawaka moto,
ﭱﭲﭳﭴ
81:7
Na nafsi zikaunganishwa,
ﭵﭶﭷﭸ
81:8
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
ﭹﭺﭻﭼ
81:9
Kwa kosa gani aliuliwa?
ﭽﭾﭿﮀ
81:10
Na madaftari yatakapo enezwa,
ﮁﮂﮃﮄ
81:11
Na mbingu itapo tanduliwa,
ﮅﮆﮇﮈ
81:12
Na Jahannamu itapo chochewa,
ﮉﮊﮋﮌ
81:13
Na Pepo ikasogezwa,
ﮍﮎﮏﮐﮑ
81:14
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
ﮒﮓﮔﮕ
81:15
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
ﮖﮗﮘ
81:16
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
ﮙﮚﮛﮜ
81:17
Na kwa usiku unapo pungua,
ﮝﮞﮟﮠ
81:18
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
ﮡﮢﮣﮤﮥ
81:19
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
81:20
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
ﮭﮮﮯﮰ
81:21
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
ﮱﯓﯔﯕ
81:22
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
ﯖﯗﯘﯙﯚ
81:23
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
81:24
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
81:25
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
ﯧﯨﯩ
81:26
Basi mnakwenda wapi?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
81:27
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
81:28
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
81:29
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







