Sura At-Takwir
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura At-Takwir pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura At-Takwir pdf Kiswahili — Pakua Sura At-Takwir Tafsiri. At-Takwir (Makka) 29 Aya.
Related
- At-Takwir TafsiriKiswahili
- At-Takwir mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura At-Takwir

ﭙﭚﭛﭜ
Jua litakapo kunjwa,
ﭝﭞﭟﭠ
Na nyota zikazimwa,
ﭡﭢﭣﭤ
Na milima ikaondolewa,
ﭥﭦﭧﭨ
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
ﭩﭪﭫﭬ
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
ﭭﭮﭯﭰ
Na bahari zikawaka moto,
ﭱﭲﭳﭴ
Na nafsi zikaunganishwa,
ﭵﭶﭷﭸ
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
ﭹﭺﭻﭼ
Kwa kosa gani aliuliwa?
ﭽﭾﭿﮀ
Na madaftari yatakapo enezwa,
ﮁﮂﮃﮄ
Na mbingu itapo tanduliwa,
ﮅﮆﮇﮈ
Na Jahannamu itapo chochewa,
ﮉﮊﮋﮌ
Na Pepo ikasogezwa,
ﮍﮎﮏﮐﮑ
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
ﮒﮓﮔﮕ
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
ﮖﮗﮘ
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
ﮙﮚﮛﮜ
Na kwa usiku unapo pungua,
ﮝﮞﮟﮠ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
ﮡﮢﮣﮤﮥ
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬ
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
ﮭﮮﮯﮰ
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
ﮱﯓﯔﯕ
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
ﯖﯗﯘﯙﯚ
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
ﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦ
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
ﯧﯨﯩ
Basi mnakwenda wapi?
ﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽﯾ
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







