Sura At-Tariq
17 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓ
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
ﭔﭕﭖﭗﭘ
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
ﭙﭚﭛ
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
ﭣﭤﭥﭦﭧ
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
ﭨﭩﭪﭫﭬ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
ﭳﭴﭵﭶﭷ
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
ﭸﭹﭺﭻ
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
ﮃﮄﮅﮆ
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
ﮇﮈﮉﮊ
Na kwa ardhi inayo pasuka!
ﮋﮌﮍﮎ
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
ﮏﮐﮑﮒ
Wala si mzaha.
ﮓﮔﮕﮖ
Hakika wao wanapanga mpango.
ﮗﮘﮙ
Na Mimi napanga mpango.
ﮚﮛﮜﮝﮞ
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema