Sura Al-Buruj
22 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭛﭜﭝﭞ
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
ﭟﭠﭡ
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
ﭢﭣﭤ
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
ﭥﭦﭧﭨ
Wameangamizwa watu wa makhandaki
ﭩﭪﭫﭬ
Yenye moto wenye kuni nyingi,
ﭭﭮﭯﭰﭱ
Walipo kuwa wamekaa hapo,
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
ﯔﯕﯖﯗﯘ
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
ﯙﯚﯛﯜ
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
ﯝﯞﯟﯠ
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
ﯡﯢﯣﯤ
Atendaye ayatakayo.
ﯥﯦﯧﯨﯩ
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
ﯪﯫﯬ
Ya Firauni na Thamudi?
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
ﯳﯴﯵﯶﯷ
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
ﯸﯹﯺﯻﯼ
Bali hii ni Qur'ani tukufu
ﯽﯾﯿﰀ
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema