Sura Al-Buruj pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Buruj pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Buruj Tafsiri. Sura Al-Buruj (Makka) 22 Aya.
Related
- Sura Al-Buruj TafsiriKiswahili
- Sura Al-Buruj mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Buruj

ﭛﭜﭝﭞ
85:1
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
ﭟﭠﭡ
85:2
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
ﭢﭣﭤ
85:3
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
ﭥﭦﭧﭨ
85:4
Wameangamizwa watu wa makhandaki
ﭩﭪﭫﭬ
85:5
Yenye moto wenye kuni nyingi,
ﭭﭮﭯﭰﭱ
85:6
Walipo kuwa wamekaa hapo,
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
85:7
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁﮂ
85:8
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
85:9
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
85:10
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭ
85:11
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
ﮮﮯﮰﮱﯓ
85:12
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
ﯔﯕﯖﯗﯘ
85:13
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
ﯙﯚﯛﯜ
85:14
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
ﯝﯞﯟﯠ
85:15
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
ﯡﯢﯣﯤ
85:16
Atendaye ayatakayo.
ﯥﯦﯧﯨﯩ
85:17
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
ﯪﯫﯬ
85:18
Ya Firauni na Thamudi?
ﯭﯮﯯﯰﯱﯲ
85:19
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
ﯳﯴﯵﯶﯷ
85:20
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
ﯸﯹﯺﯻﯼ
85:21
Bali hii ni Qur'ani tukufu
ﯽﯾﯿﰀ
85:22
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







