PDF —
19 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Infitar pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Infitar pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Infitar Tafsiri. Sura Al-Infitar (Makka) 19 Aya.



19 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭑﭒﭓﭔ
82:1 Mbingu itapo chanika,
ﭕﭖﭗﭘ
82:2 Na nyota zitapo tawanyika,
ﭙﭚﭛﭜ
82:3 Na bahari zitakapo pasuliwa,
ﭝﭞﭟﭠ
82:4 Na makaburi yatapo fukuliwa,
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
82:5 Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
82:6 Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
ﭮﭯﭰﭱﭲ
82:7 Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
82:8 Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
82:9 Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
ﭿﮀﮁﮂ
82:10 Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
ﮃﮄﮅ
82:11 Waandishi wenye hishima,
ﮆﮇﮈﮉ
82:12 Wanayajua mnayo yatenda.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
82:13 Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
82:14 Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
ﮔﮕﮖﮗ
82:15 Wataingia humo Siku ya Malipo.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
82:16 Na hawatoacha kuwamo humo.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
82:17 Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
82:18 Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
82:19 Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema