Sura Al-Infitar pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Infitar pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Infitar Tafsiri. Sura Al-Infitar (Makka) 19 Aya.
Related
- Sura Al-Infitar TafsiriKiswahili
- Sura Al-Infitar mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Infitar

ﭑﭒﭓﭔ
82:1
Mbingu itapo chanika,
ﭕﭖﭗﭘ
82:2
Na nyota zitapo tawanyika,
ﭙﭚﭛﭜ
82:3
Na bahari zitakapo pasuliwa,
ﭝﭞﭟﭠ
82:4
Na makaburi yatapo fukuliwa,
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
82:5
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
82:6
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
ﭮﭯﭰﭱﭲ
82:7
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
82:8
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
82:9
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
ﭿﮀﮁﮂ
82:10
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
ﮃﮄﮅ
82:11
Waandishi wenye hishima,
ﮆﮇﮈﮉ
82:12
Wanayajua mnayo yatenda.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
82:13
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
82:14
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
ﮔﮕﮖﮗ
82:15
Wataingia humo Siku ya Malipo.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
82:16
Na hawatoacha kuwamo humo.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
82:17
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
82:18
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
82:19
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







