Sura Al-Infitar
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Infitar pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Infitar pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Infitar Tafsiri. Al-Infitar (Makka) 19 Aya.
Related
- Al-Infitar TafsiriKiswahili
- Al-Infitar mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Infitar

ﭑﭒﭓﭔ
Mbingu itapo chanika,
ﭕﭖﭗﭘ
Na nyota zitapo tawanyika,
ﭙﭚﭛﭜ
Na bahari zitakapo pasuliwa,
ﭝﭞﭟﭠ
Na makaburi yatapo fukuliwa,
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
ﭧﭨﭩﭪﭫﭬﭭ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
ﭮﭯﭰﭱﭲ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
ﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
ﭺﭻﭼﭽﭾ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
ﭿﮀﮁﮂ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
ﮃﮄﮅ
Waandishi wenye hishima,
ﮆﮇﮈﮉ
Wanayajua mnayo yatenda.
ﮊﮋﮌﮍﮎ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
ﮏﮐﮑﮒﮓ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
ﮔﮕﮖﮗ
Wataingia humo Siku ya Malipo.
ﮘﮙﮚﮛﮜ
Na hawatoacha kuwamo humo.
ﮝﮞﮟﮠﮡﮢ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ﮣﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







