Sura Al-Mutaffifin pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Mutaffifin pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Mutaffifin Tafsiri. Sura Al-Mutaffifin (Makka) 36 Aya.
Related
- Sura Al-Mutaffifin TafsiriKiswahili
- Sura Al-Mutaffifin mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Mutaffifin

ﯖﯗﯘ
83:1
Ole wao hao wapunjao!
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
83:2
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
83:3
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
83:4
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
ﭑﭒﭓ
83:5
Katika Siku iliyo kuu,
ﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
83:6
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
83:7
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
ﭡﭢﭣﭤﭥ
83:8
Unajua nini Sijjin?
ﭦﭧﭨ
83:9
Kitabu kilicho andikwa.
ﭩﭪﭫﭬ
83:10
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
ﭭﭮﭯﭰﭱ
83:11
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
83:12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
83:13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
83:14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
83:15
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ﮔﮕﮖﮗﮘ
83:16
Kisha wataingia Motoni!
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
83:17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
83:18
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
ﮨﮩﮪﮫﮬ
83:19
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
ﮭﮮﮯ
83:20
Kitabu kilicho andikwa.
ﮰﮱﯓ
83:21
Wanakishuhudia walio karibishwa.
ﯔﯕﯖﯗﯘ
83:22
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
ﯙﯚﯛﯜ
83:23
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
83:24
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
ﯣﯤﯥﯦﯧ
83:25
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
83:26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
ﯰﯱﯲﯳ
83:27
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
ﯴﯵﯶﯷﯸ
83:28
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
83:29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
ﰂﰃﰄﰅﰆ
83:30
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
83:31
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔ
83:32
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
ﰕﰖﰗﰘﰙ
83:33
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
83:34
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
ﭘﭙﭚﭛ
83:35
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
83:36
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







