Sura Al-Mutaffifin
PDF —
36 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Mutaffifin pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Mutaffifin pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Mutaffifin Tafsiri. Al-Mutaffifin (Makka) 36 Aya.



Sura Al-Mutaffifin
36 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﯖﯗﯘ
Ole wao hao wapunjao!
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟ
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
ﯠﯡﯢﯣﯤﯥ
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
ﯦﯧﯨﯩﯪﯫ
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
ﭑﭒﭓ
Katika Siku iliyo kuu,
ﭔﭕﭖﭗﭘﭙ
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟﭠ
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
ﭡﭢﭣﭤﭥ
Unajua nini Sijjin?
ﭦﭧﭨ
Kitabu kilicho andikwa.
ﭩﭪﭫﭬ
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
ﭭﭮﭯﭰﭱ
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
ﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸﭹ
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
ﭺﭻﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊﮋﮌ
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓ
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ﮔﮕﮖﮗﮘ
Kisha wataingia Motoni!
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞﮟﮠ
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧ
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
ﮨﮩﮪﮫﮬ
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
ﮭﮮﮯ
Kitabu kilicho andikwa.
ﮰﮱﯓ
Wanakishuhudia walio karibishwa.
ﯔﯕﯖﯗﯘ
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
ﯙﯚﯛﯜ
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
ﯝﯞﯟﯠﯡﯢ
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
ﯣﯤﯥﯦﯧ
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭﯮﯯ
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
ﯰﯱﯲﯳ
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
ﯴﯵﯶﯷﯸ
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
ﯹﯺﯻﯼﯽﯾﯿﰀﰁ
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
ﰂﰃﰄﰅﰆ
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌﰍ
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓﰔ
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
ﰕﰖﰗﰘﰙ
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗ
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
ﭘﭙﭚﭛ
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡﭢ
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema