Sura Al-Mutaffifin kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Al-Mutaffifin na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (36 Aya — مكية). Al-Mutaffifin Sikiliza, Al-Mutaffifin Tafsiri, Al-Mutaffifin mp3, Al-Mutaffifin pdf.

Soma na Sikiliza Sura Al-Mutaffifin

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Ole wao hao wapunjao!
الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Unajua nini Sijjin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلَّا إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
← 82 Al-Mutaffifin (83/114) 84 →
Soma Sura Al-Mutaffifin kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

83المطففين Al-Mutaffifin 📚 36 Aya مكية

Aya kwa aya – Sura Al-Mutaffifin — 36 Aya




Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema