An-Nisa · 22/176
Tafsiri Uandishi wa sauti — Sura An-Nisa
وَلَا تَنكِحُوا مَا نَكَحَ آبَاؤُكُم مِّنَ النِّسَاءِ إِلَّا مَا قَدْ سَلَفَ ۚ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَمَقْتًا وَسَاءَ سَبِيلًا ۝٢٢
Wa laa tankihoo maa nakaha aabaaa`ukum minan nisaaa`i illaa maa qad salaf; inahoo kaana faahishatanw wa maqtanw wa saaa`a sabeelaa
📖 Kwa Kiswahili
Wala msiwaoe wake walio waoa baba zenu, ila yaliyo kwisha pita. Hakika huo ni uchafu na uchukizo na ni njia mbaya.

🎧 Sikiliza
📜

Tafsiri — Tafsir

Maana ya Maneno:

  • Ma nakaḥa abāʾukum: Wanawake ambao baba zenu waliowaoa (ndoa halali au batili).
  • Illā mā qad salaf: Isipokuwa yale yaliyopita kabla ya Uislamu (katika enzi ya ujahili), hayana lawama.
  • Fāḥishah: Dhambi kubwa iliyojeuri na iliyochukiza sana.
  • Maqtan: Chuki kubwa ya Mwenyezi Mungu kwa mtendaji.
  • Sāʾa sabīlan: Ni njia mbaya na iliyochukiwa.

Ufafanuzi wa Aya:

Aya hii inakataza kabisa kuoa wanawake ambao baba zenu waliowaoa, iwe ndoa hiyo ilikamilika au la, kwa kuwa mara tu baba anapooa mwanamke kwa nikaha sahihi, mwanamke huyo anakuwa haramu kwa mwanawe. Hata hivyo, Mwenyezi Mungu amesamehe yale yaliyotangulia kabla ya Uislamu, kwa kuwa waliokuwa wamefanya hivyo katika enzi ya ujahili hawataadhibiwa, lakini baada ya kuja Uislamu, ni lazima waachane nao mara moja.

Mwenyezi Mungu anaeleza sababu ya kukataza huku kwa kusema kwamba jambo hili ni dhambi kubwa iliyochukiza sana, na ni chuki kubwa kwa Mwenyezi Mungu kwa anayelifanya, kwa sababu linavunja heshima ya baba na kuharibu uhusiano wa kifamilia. Pia ni njia mbaya na iliyopotoka, kwani inamletea mtu ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na kumfanya awe mbali na rehema Yake. Aya hii inasisitiza kwamba ndoa ya mwanamke na mwanawe baada ya baba yake ni jambo lililokatazwa kabisa, na ni mojawapo ya mambo makubwa ya dhambi yaliyokuwepo katika ujahili ambayo Uislamu ulikuja kuyafutilia mbali.

Faida Zinazotokana na Aya:

  1. Uislamu unalinda heshima ya familia na kuhifadhi uhusiano safi kati ya watu, kwa kukataza mambo yanayovunja heshima na kuleta chuki.
  2. Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa rehema na msamaha, kwani amesamehe yaliyopita kabla ya Uislamu, na hii inatoa fursa kwa kila mtu kurejea kwenye njia sahihi bila kuhisi kubebwa na mzigo wa zamani.
  3. Aya inafundisha kwamba kila jambo linalomchukiza Mwenyezi Mungu ni lazima liepukwe, hata kama lilikuwa likifanyika kwa muda mrefu, kwa sababu kumtii Mwenyezi Mungu ni bora kuliko kufuata mila za zamani.
  4. Inaonyesha uzito wa dhambi hii, kwamba Mwenyezi Mungu ameiita "fahisha" na "maqtan", na hii inatuonya tujiepushe na kila dhambi kubwa ili tupate ridhaa Yake na kuepuka ghadhabu Yake.


📜 Aya 20-24 — Sura An-Nisa

20وَإِنْ أَرَدتُّمُ اسْتِبْدَالَ زَوْجٍ مَّكَانَ زَوْجٍ وَآتَيْتُمْ إِحْدَاهُنَّ قِنطَارًا فَلَا تَأْخُذُوا مِنْهُ شَيْئًا ۚ أَتَأْخُذُونَهُ بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا
Na mkitaka kubadilisha mke mahali pa mke, na hali mmoja wao mmempa chungu ya mali, basi msichukue katika hayo kitu chochote. Je, mtachukua kwa dhulma na kosa lilio wazi?
21وَكَيْفَ تَأْخُذُونَهُ وَقَدْ أَفْضَىٰ بَعْضُكُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ وَأَخَذْنَ مِنكُم مِّيثَاقًا غَلِيظًا
Na mtachukuaje na ilhali mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, na wao wanawake wamechukua kwenu ahadi iliyo madhubuti?
22وَلَا تَنكِحُوا مَا نَكَحَ آبَاؤُكُم مِّنَ النِّسَاءِ إِلَّا مَا قَدْ سَلَفَ ۚ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَمَقْتًا وَسَاءَ سَبِيلًا
Wala msiwaoe wake walio waoa baba zenu, ila yaliyo kwisha pita. Hakika huo ni uchafu na uchukizo na ni njia mbaya.
23حُرِّمَتْ عَلَيْكُمْ أُمَّهَاتُكُمْ وَبَنَاتُكُمْ وَأَخَوَاتُكُمْ وَعَمَّاتُكُمْ وَخَالَاتُكُمْ وَبَنَاتُ الْأَخِ وَبَنَاتُ الْأُخْتِ وَأُمَّهَاتُكُمُ اللَّاتِي أَرْضَعْنَكُمْ وَأَخَوَاتُكُم مِّنَ الرَّضَاعَةِ وَأُمَّهَاتُ نِسَائِكُمْ وَرَبَائِبُكُمُ اللَّاتِي فِي حُجُورِكُم مِّن نِّسَائِكُمُ اللَّاتِي دَخَلْتُم بِهِنَّ فَإِن لَّمْ تَكُونُوا دَخَلْتُم بِهِنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ وَحَلَائِلُ أَبْنَائِكُمُ الَّذِينَ مِنْ أَصْلَابِكُمْ وَأَن تَجْمَعُوا بَيْنَ الْأُخْتَيْنِ إِلَّا مَا قَدْ سَلَفَ ۗ إِنَّ اللَّهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا
Mmeharimishiwa mama zenu, na binti zenu, na dada zenu, na shangazi zenu, na khaalati zenu, na binti wa ndugu mume, na binti wa dada, na mama zenu walio kunyonyesheni, na dada zenu kwa kunyonya, na mama wa wake zenu, na watoto wenu wa kambo walio katika ulinzi wenu walio zaliwa na wake zenu mlio waingilia. Ikiwa hamkuwaingilia basi hapana lawama juu yenu. (Pia mmeharimishwa) wake wa watoto wenu walio toka katika migongo yenu. Na kuwaoa pamoja dada wawili isipo kuwa yale yaliyo kwisha pita. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
24۞ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ النِّسَاءِ إِلَّا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۖ كِتَابَ اللَّهِ عَلَيْكُمْ ۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَاءَ ذَٰلِكُمْ أَن تَبْتَغُوا بِأَمْوَالِكُم مُّحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ ۚ فَمَا اسْتَمْتَعْتُم بِهِ مِنْهُنَّ فَآتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةً ۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا تَرَاضَيْتُم بِهِ مِن بَعْدِ الْفَرِيضَةِ ۚ إِنَّ اللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا
NA WANAWAKE wenye waume, isipo kuwa walio milikiwa na mikono yenu ya kulia. Ndiyo Sharia ya Mwenyezi Mungu juu yenu. Na mmehalilishiwa wasio kuwa hao, mtafute kwa mali yenu kwa kuowa pasina kuzini. Kama mnavyo starehe nao, basi wapeni mahari yao kwa kuwa ni waajibu. Wala hapana lawama juu yenu kwa mtakacho kubaliana baada ya kutimiza waajibu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua na Mwenye hikima.
An-NisaFaharasa ya Qurani
176Aya
MadinaRevelation
22Aya

Tafsiri — An-Nisa 22

Sura An-Nisa Aya 22 - Soma, Sikiliza, Tafsiri, Kiswahili : Wala msiwaoe wake walio waoa baba zenu, ila yaliyo kwisha…

Sura Aya 22/176 — Sura An-Nisa النساء (Madina). Soma Sikiliza Tafsiri (Kiswahili). Sikiliza: Sura An-Nisa Sikiliza, Sura An-Nisa Tafsiri, Sura An-Nisa mp3, Sura An-Nisa pdf. Aya 20–24. Kwa Kiswahili: Soomaali.




Kurani Tukufu


Monday, September 7, 2026

Usitusahau katika dua zako njema