Sura Al-Qalam pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Qalam pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qalam Tafsiri. Sura Al-Qalam (Makka) 52 Aya.
Related
- Sura Al-Qalam TafsiriKiswahili
- Sura Al-Qalam mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Qalam

ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
68:1
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
68:2
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
68:3
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
68:4
Na hakika wewe una tabia tukufu.
ﮠﮡﮢ
68:5
Karibu utaona, na wao wataona,
ﮣﮤﮥ
68:6
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
68:7
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
ﯓﯔﯕﯖ
68:8
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
ﯗﯘﯙﯚﯛ
68:9
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
68:10
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
ﯢﯣﯤﯥ
68:11
Mtapitapi, apitaye akifitini,
ﯦﯧﯨﯩﯪ
68:12
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
ﯫﯬﯭﯮﯯ
68:13
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
68:14
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
68:15
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
ﯾﯿﰀﰁ
68:16
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
68:17
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
ﭜﭝﭞ
68:18
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
68:19
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
ﭧﭨﭩ
68:20
Likawa kama usiku wa giza.
ﭪﭫﭬ
68:21
Asubuhi wakaitana.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
68:22
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
ﭵﭶﭷﭸ
68:23
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
68:24
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
68:25
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
68:26
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
ﮋﮌﮍﮎ
68:27
Bali tumenyimwa!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
68:28
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
68:29
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
68:30
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
68:31
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
68:32
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
68:33
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
68:34
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
ﯨﯩﯪﯫ
68:35
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
ﯬﯭﯮﯯﯰ
68:36
Mna nini? Mnahukumu vipi?
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
68:37
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
68:38
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
68:39
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
ﰊﰋﰌﰍﰎ
68:40
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
ﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
68:41
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
ﰘﰙﰚﰛﰜﰝﰞﰟﰠﰡ
68:42
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
68:43
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
68:44
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
68:45
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
68:46
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
68:47
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
68:48
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
68:49
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
68:50
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
68:51
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
68:52
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







