Sura Al-Qalam
PDF —
Built right in your browser — download starts automatically
Sura Al-Qalam pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Qalam pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qalam Tafsiri. Al-Qalam (Makka) 52 Aya.
Related
- Al-Qalam TafsiriKiswahili
- Al-Qalam mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Qalam

ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
ﮠﮡﮢ
Karibu utaona, na wao wataona,
ﮣﮤﮥ
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
ﯓﯔﯕﯖ
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
ﯗﯘﯙﯚﯛ
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
ﯢﯣﯤﯥ
Mtapitapi, apitaye akifitini,
ﯦﯧﯨﯩﯪ
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
ﯫﯬﯭﯮﯯ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
ﯾﯿﰀﰁ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
ﭜﭝﭞ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
ﭧﭨﭩ
Likawa kama usiku wa giza.
ﭪﭫﭬ
Asubuhi wakaitana.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
ﭵﭶﭷﭸ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
ﮋﮌﮍﮎ
Bali tumenyimwa!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
ﯨﯩﯪﯫ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
ﯬﯭﯮﯯﯰ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
ﰊﰋﰌﰍﰎ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
ﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
ﰘﰙﰚﰛﰜﰝﰞﰟﰠﰡ
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
Kurani Tukufu
Tuesday, August 18, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







