PDF —
52 Aya Makka PDF
Built right in your browser — download starts automatically

Sura Al-Qalam pdf — Pakua (Kiswahili)

Sura Al-Qalam pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Qalam Tafsiri. Sura Al-Qalam (Makka) 52 Aya.



52 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
68:1 Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔ
68:2 Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
ﮕﮖﮗﮘﮙﮚ
68:3 Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
ﮛﮜﮝﮞﮟ
68:4 Na hakika wewe una tabia tukufu.
ﮠﮡﮢ
68:5 Karibu utaona, na wao wataona,
ﮣﮤﮥ
68:6 Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
68:7 Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
ﯓﯔﯕﯖ
68:8 Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
ﯗﯘﯙﯚﯛ
68:9 Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
ﯜﯝﯞﯟﯠﯡ
68:10 Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
ﯢﯣﯤﯥ
68:11 Mtapitapi, apitaye akifitini,
ﯦﯧﯨﯩﯪ
68:12 Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
ﯫﯬﯭﯮﯯ
68:13 Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
ﯰﯱﯲﯳﯴﯵ
68:14 Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
ﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼﯽ
68:15 Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
ﯾﯿﰀﰁ
68:16 Tutamtia kovu juu ya pua yake.
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
68:17 Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
ﭜﭝﭞ
68:18 Wala hawakusema: Mungu akipenda!
ﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
68:19 Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
ﭧﭨﭩ
68:20 Likawa kama usiku wa giza.
ﭪﭫﭬ
68:21 Asubuhi wakaitana.
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲﭳﭴ
68:22 Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
ﭵﭶﭷﭸ
68:23 Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾﭿ
68:24 Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
ﮀﮁﮂﮃﮄ
68:25 Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
68:26 Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
ﮋﮌﮍﮎ
68:27 Bali tumenyimwa!
ﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
68:28 Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
ﮗﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
68:29 Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
ﮞﮟﮠﮡﮢﮣ
68:30 Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
ﮤﮥﮦﮧﮨﮩ
68:31 Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
ﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱﯓﯔﯕ
68:32 Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝﯞﯟﯠ
68:33 Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
ﯡﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
68:34 Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
ﯨﯩﯪﯫ
68:35 Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
ﯬﯭﯮﯯﯰ
68:36 Mna nini? Mnahukumu vipi?
ﯱﯲﯳﯴﯵﯶ
68:37 Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
68:38 Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂﰃﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
68:39 Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
ﰊﰋﰌﰍﰎ
68:40 Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
ﰏﰐﰑﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
68:41 Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
ﰘﰙﰚﰛﰜﰝﰞﰟﰠﰡ
68:42 Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛﭜﭝ
68:43 Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣﭤﭥﭦﭧﭨﭩ
68:44 Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
ﭪﭫﭬﭭﭮﭯﭰ
68:45 Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
ﭱﭲﭳﭴﭵﭶﭷﭸ
68:46 Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
ﭹﭺﭻﭼﭽﭾ
68:47 Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
ﭿﮀﮁﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
68:48 Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
ﮋﮌﮍﮎﮏﮐﮑﮒﮓﮔﮕ
68:49 Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
ﮖﮗﮘﮙﮚﮛ
68:50 Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡﮢﮣﮤﮥﮦﮧﮨ
68:51 Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
ﮩﮪﮫﮬﮭﮮ
68:52 Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Kurani Tukufu


Wednesday, September 9, 2026

Usitusahau katika dua zako njema