Sura Al-Qalam kwa Kiarabu na Kiswahili

Soma Sura Al-Qalam na tafsiri kamili ya Kiswahili, maandishi na usomaji wa sauti. Tafsiri aya kwa aya. (52 Aya — مكية). Al-Qalam Sikiliza, Al-Qalam Tafsiri, Al-Qalam mp3, Al-Qalam pdf.

Soma na Sikiliza Sura Al-Qalam

🎧 Aya
M Mishary Rashid Alafasy
M Mahmoud Khalil Al-Husary
A Abdurrahman As-Sudais
M Mohamed Siddiq Al-Minshawi
A Abdul Basit Abdul Samad
A Ali Al-Hudhaify
A Ahmed ibn Ali al-Ajamy
A Abu Bakr Ash-Shaatree
M Muhammad Ayyoub
A Abdullah Basfar
A Abdullah Al-Juhani
M Maher Al Muaiqly
x1
ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ ۝١
📖 Tafsiri Aya 1
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ ۝٢
📖 Tafsiri Aya 2
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ ۝٣
📖 Tafsiri Aya 3
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ ۝٤
📖 Tafsiri Aya 4
Na hakika wewe una tabia tukufu.
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ ۝٥
📖 Tafsiri Aya 5
Karibu utaona, na wao wataona,
بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ ۝٦
📖 Tafsiri Aya 6
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ ۝٧
📖 Tafsiri Aya 7
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ ۝٨
📖 Tafsiri Aya 8
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ ۝٩
📖 Tafsiri Aya 9
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ ۝١٠
📖 Tafsiri Aya 10
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ ۝١١
📖 Tafsiri Aya 11
Mtapitapi, apitaye akifitini,
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ ۝١٢
📖 Tafsiri Aya 12
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ ۝١٣
📖 Tafsiri Aya 13
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ ۝١٤
📖 Tafsiri Aya 14
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ۝١٥
📖 Tafsiri Aya 15
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ ۝١٦
📖 Tafsiri Aya 16
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ ۝١٧
📖 Tafsiri Aya 17
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
وَلَا يَسْتَثْنُونَ ۝١٨
📖 Tafsiri Aya 18
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ ۝١٩
📖 Tafsiri Aya 19
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ ۝٢٠
📖 Tafsiri Aya 20
Likawa kama usiku wa giza.
فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ ۝٢١
📖 Tafsiri Aya 21
Asubuhi wakaitana.
أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ ۝٢٢
📖 Tafsiri Aya 22
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ ۝٢٣
📖 Tafsiri Aya 23
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ ۝٢٤
📖 Tafsiri Aya 24
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ ۝٢٥
📖 Tafsiri Aya 25
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ ۝٢٦
📖 Tafsiri Aya 26
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ ۝٢٧
📖 Tafsiri Aya 27
Bali tumenyimwa!
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ ۝٢٨
📖 Tafsiri Aya 28
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ ۝٢٩
📖 Tafsiri Aya 29
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ ۝٣٠
📖 Tafsiri Aya 30
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ ۝٣١
📖 Tafsiri Aya 31
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ ۝٣٢
📖 Tafsiri Aya 32
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ۝٣٣
📖 Tafsiri Aya 33
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ ۝٣٤
📖 Tafsiri Aya 34
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ ۝٣٥
📖 Tafsiri Aya 35
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ۝٣٦
📖 Tafsiri Aya 36
Mna nini? Mnahukumu vipi?
أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ ۝٣٧
📖 Tafsiri Aya 37
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ ۝٣٨
📖 Tafsiri Aya 38
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ ۝٣٩
📖 Tafsiri Aya 39
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ ۝٤٠
📖 Tafsiri Aya 40
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ ۝٤١
📖 Tafsiri Aya 41
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ ۝٤٢
📖 Tafsiri Aya 42
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ ۝٤٣
📖 Tafsiri Aya 43
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا الْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ ۝٤٤
📖 Tafsiri Aya 44
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
وَأُمْلِي لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ ۝٤٥
📖 Tafsiri Aya 45
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ ۝٤٦
📖 Tafsiri Aya 46
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ ۝٤٧
📖 Tafsiri Aya 47
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ ۝٤٨
📖 Tafsiri Aya 48
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ ۝٤٩
📖 Tafsiri Aya 49
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ ۝٥٠
📖 Tafsiri Aya 50
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ ۝٥١
📖 Tafsiri Aya 51
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ ۝٥٢
📖 Tafsiri Aya 52
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
← 67 Al-Qalam (68/114) 69 →
Soma Sura Al-Qalam kwa Kiswahili – Tafsiri na Sauti

68القلم Al-Qalam 📚 52 Aya مكية



Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema