Sura Al-Fajr
30 Aya · Makka · Kiswahili
bismillah
ﭤﭥ
Naapa kwa alfajiri,
ﭦﭧﭨ
Na kwa masiku kumi,
ﭩﭪﭫ
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
ﭬﭭﭮﭯ
Na kwa usiku unapo pita,
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
ﭾﭿﮀﮁ
Wa Iram, wenye majumba marefu?
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
ﮏﮐﮑﮒ
Na Firauni mwenye vigingi?
ﮓﮔﮕﮖﮗ
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
ﮘﮙﮚﮛ
Wakakithirisha humo ufisadi?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
ﮢﮣﮤﮥ
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
Wala hamhimizani kulisha masikini;
ﯫﯬﯭﯮﯯ
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
ﯰﯱﯲﯳﯴ
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
ﭜﭝﭞﭟﭠ
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
ﭧﭨﭩﭪﭫ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
ﭬﭭﭮﭯ
Ewe nafsi iliyo tua!
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
ﭶﭷﭸﭹ
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
ﭺﭻﭼ
Na ingia katika Pepo yangu.

Kurani Tukufu


Tuesday, August 18, 2026

Usitusahau katika dua zako njema