Sura Al-Fajr pdf — Pakua (Kiswahili)
Sura Al-Fajr pdf Kiswahili — Pakua Sura Al-Fajr Tafsiri. Sura Al-Fajr (Makka) 30 Aya.
Related
- Sura Al-Fajr TafsiriKiswahili
- Sura Al-Fajr mp3Sikiliza
- Quran Index Kiswahili114
More Sura PDF
Sura Al-Fajr

ﭤﭥ
89:1
Naapa kwa alfajiri,
ﭦﭧﭨ
89:2
Na kwa masiku kumi,
ﭩﭪﭫ
89:3
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
ﭬﭭﭮﭯ
89:4
Na kwa usiku unapo pita,
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵﭶ
89:5
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
ﭷﭸﭹﭺﭻﭼﭽ
89:6
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
ﭾﭿﮀﮁ
89:7
Wa Iram, wenye majumba marefu?
ﮂﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
89:8
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
ﮉﮊﮋﮌﮍﮎ
89:9
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
ﮏﮐﮑﮒ
89:10
Na Firauni mwenye vigingi?
ﮓﮔﮕﮖﮗ
89:11
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
ﮘﮙﮚﮛ
89:12
Wakakithirisha humo ufisadi?
ﮜﮝﮞﮟﮠﮡ
89:13
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
ﮢﮣﮤﮥ
89:14
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
89:15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
ﯓﯔﯕﯖﯗﯘﯙﯚﯛﯜﯝ
89:16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
ﯞﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
89:17
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
ﯥﯦﯧﯨﯩﯪ
89:18
Wala hamhimizani kulisha masikini;
ﯫﯬﯭﯮﯯ
89:19
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
ﯰﯱﯲﯳﯴ
89:20
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
ﯵﯶﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
89:21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
89:22
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖﭗﭘﭙﭚﭛ
89:23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
ﭜﭝﭞﭟﭠ
89:24
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
ﭡﭢﭣﭤﭥﭦ
89:25
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
ﭧﭨﭩﭪﭫ
89:26
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
ﭬﭭﭮﭯ
89:27
Ewe nafsi iliyo tua!
ﭰﭱﭲﭳﭴﭵ
89:28
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
ﭶﭷﭸﭹ
89:29
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
ﭺﭻﭼ
89:30
Na ingia katika Pepo yangu.
Kurani Tukufu
Wednesday, September 9, 2026
Usitusahau katika dua zako njema







